< Mathayo 1 >
1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
Pleme Isusa Hrista, sina Davida Avraamova sina.
2 Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.
Avraam rodi Isaka. A Isak rodi Jakova. A Jakov rodi Judu i braæu njegovu.
3 Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.
A Juda rodi Faresa i Zaru s Tamarom. A Fares rodi Esroma. A Esrom rodi Arama.
4 Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.
A Aram rodi Aminadava. A Aminadav rodi Naasona. A Naason rodi Salmona.
5 Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,
A Salmon rodi Vooza s Rahavom. A Vooz rodi Ovida s Rutom. A Ovid rodi Jeseja.
6 Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.
A Jesej rodi Davida cara. A David car rodi Solomuna s Urijnicom.
7 Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.
A Solomun rodi Rovoama. A Rovoam rodi Aviju. A Avija rodi Asu.
8 Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.
A Asa rodi Josafata. A Josafat rodi Jorama. A Joram rodi Oziju.
9 Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.
A Ozija rodi Joatama. A Joatam rodi Ahaza. A Ahaz rodi Ezekiju.
10 Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.
A Ezekija rodi Manasiju. A Manasija rodi Amona. A Amon rodi Josiju.
11 Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.
A Josija rodi Jehoniju i braæu njegovu, u seobi Vavilonskoj.
12 Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
A po seobi Vavilonskoj, Jehonija rodi Salatiila. A Salatiilo rodi Zorovavela.
13 Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.
A Zorovavel rodi Aviuda. A Aviud rodi Eliakima. A Eliakim rodi Azora.
14 Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.
A Azor rodi Sadoka. A Sadok rodi Ahima. A Ahim rodi Eliuda.
15 Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.
A Eliud rodi Eleazara. A Eleazar rodi Matana. A Matan rodi Jakova.
16 Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.
A Jakov rodi Josifa, muža Marije, koja rodi Isusa prozvanoga Hrista.
17 Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.
Svega dakle koljena od Avraama do Davida, koljena èetrnaest, a od Davida do seobe Vavilonske, koljena èetrnaest, a od seobe Vavilonske do Hrista, koljena èetrnaest.
18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
A roðenje Isusa Hrista bilo je ovako: kad je Marija, mati njegova, bila isprošena za Josifa, a još dok se nijesu bili sastali, naðe se da je ona trudna od Duha svetoga.
19 Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.
A Josif muž njezin, buduæi pobožan, i ne hoteæi je javno sramotiti, namisli je tajno pustiti.
20 Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,'' Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
No kad on tako pomisli, a to mu se javi u snu anðeo Gospodnji govoreæi: Josife, sine Davidov! ne boj se uzeti Marije žene svoje; jer ono što se u njoj zaèelo od Duha je svetoga.
21 Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.''
Pa æe roditi sina, i nadjeni mu ime Isus; jer æe on izbaviti svoj narod od grijeha njihovijeh.
22 Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,
A ovo je sve bilo da se izvrši što je Gospod kazao preko proroka koji govori:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”— maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
Eto, djevojka æe zatrudnjeti, i rodiæe sina, i nadjenuæe mu ime Emanuilo, koje æe reæi: s nama Bog.
24 Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.
Kad se Josif probudi od sna, uèini kao što mu je zapovjedio anðeo Gospodnji, i uzme ženu svoju.
25 Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
I ne znadijaše za nju dok ne rodi sina svojega prvenca, i nadjede mu ime Isus.