< Mathayo 1 >
1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
Księga rodu Jezusa Chrystusa, syna Dawida, syna Abrahama.
2 Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.
Abraham spłodził Izaaka, a Izaak spłodził Jakuba, a Jakub spłodził Judę i jego braci.
3 Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.
A Juda spłodził z Tamar Faresa i Zarę, a Fares spłodził Ezroma, a Ezrom spłodził Arama.
4 Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.
A Aram spłodził Aminadaba, a Aminadab spłodził Naasona, a Naason spłodził Salmona.
5 Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,
A Salmon spłodził z Rachab Booza, a Booz spłodził z Rut Obeda, a Obed spłodził Jessego.
6 Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.
A Jesse spłodził króla Dawida, a król Dawid spłodził Salomona z tej, która [była żoną] Uriasza.
7 Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.
A Salomon spłodził Roboama, a Roboam spłodził Abiasza, a Abiasz spłodził Azę.
8 Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.
A Aza spłodził Jozafata, a Jozafat spłodził Jorama, a Joram spłodził Ozjasza.
9 Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.
A Ozjasz spłodził Joatama, a Joatam spłodził Achaza, a Achaz spłodził Ezechiasza.
10 Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.
A Ezechiasz spłodził Manassesa, a Manasses spłodził Amona, a Amon spłodził Jozjasza.
11 Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.
A Jozjasz spłodził Jechoniasza i jego braci w czasie uprowadzenia do Babilonu.
12 Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
A po uprowadzeniu do Babilonu Jechoniasz spłodził Salatiela, a Salatiel spłodził Zorobabela.
13 Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.
A Zorobabel spłodził Abiuda, a Abiud spłodził Eliakima, a Eliakim spłodził Azora.
14 Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.
A Azor spłodził Sadoka, a Sadok spłodził Achima, a Achim spłodził Eliuda.
15 Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.
A Eliud spłodził Eleazara, a Eleazar spłodził Matana, a Matan spłodził Jakuba.
16 Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.
A Jakub spłodził Józefa, męża Marii, z której narodził się Jezus, zwany Chrystusem.
17 Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.
Tak więc wszystkich pokoleń od Abrahama aż do Dawida [jest] czternaście; a od Dawida aż do uprowadzenia do Babilonu – pokoleń czternaście; a od uprowadzenia do Babilonu aż do Chrystusa – pokoleń czternaście.
18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
A z narodzeniem Jezusa Chrystusa było tak: Gdy Maria, jego matka, została zaślubiona Józefowi, zanim się zeszli, okazało się, że jest brzemienna z Ducha Świętego.
19 Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.
Ale Józef, jej mąż, będąc sprawiedliwym i nie chcąc jej zniesławić, chciał ją potajemnie oddalić.
20 Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,'' Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
A gdy o tym rozmyślał, oto anioł Pana ukazał mu się we śnie i powiedział: Józefie, synu Dawida, nie bój się przyjąć Marii, twojej żony. To bowiem, co się w niej poczęło, jest z Ducha Świętego.
21 Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.''
I urodzi syna, któremu nadasz imię Jezus. On bowiem zbawi swój lud od jego grzechów.
22 Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,
A to wszystko się stało, aby się wypełniło, co powiedział Pan przez proroka:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”— maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
Oto dziewica będzie brzemienna i urodzi syna, któremu nadadzą imię Emmanuel, co się tłumaczy: Bóg z nami.
24 Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.
Wtedy Józef, obudziwszy się ze snu, uczynił tak, jak mu rozkazał anioł Pana, i przyjął swoją żonę.
25 Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
Ale nie obcował z nią, dopóki nie urodziła swego pierworodnego syna, któremu nadał imię Jezus.