< Mathayo 1 >

1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
Généalogie de Jésus-Christ, fils de David, fils d'Abraham.
2 Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.
Abraham engendra Isaac; Isaac, Jacob; Jacob, Juda et ses frères;
3 Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.
Juda, Phares et Zara, qu'il eut de Thamar; Phares, Esrom; Esrom, Aram;
4 Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.
Aram, Aminabad; Aminabad, Naasson; Naasson, Salmon;
5 Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,
Salmon, Booz, qu'il eut de Rahab; Booz, Jobed, qu'il eut de Ruth;
6 Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.
Jobed, Issaï; Issaï, le roi David. David engendra Salomon qu'il eut de la femme d'Urie;
7 Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.
Salomon, Roboam; Roboam, Abia; Abia, Asa;
8 Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.
Asa, Josaphat; - Josaphat, Joram; Joram, Ozias;
9 Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.
Ozias, Joatham; Joatham, Achez; Achez, Ezéchias;
10 Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.
Ezéchias, Manassé; Manassé, Amos; Amos, Josias;
11 Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.
Josias, Jéchonias et ses frères, lors de l'émigration à Babylone.
12 Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
Après l'émigration à Babylone, Jéchonias engendra Salathiel; Salathiél, Zorobabel;
13 Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.
Zorobabel, Abioud; Abioud, Eliacim; Eliacim, Azor;
14 Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.
Azor, Sadoc; Sadoc, Achim; Achim, Elioud;
15 Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.
Elioud, Eléazar; Eléazar, Matthan; Matthan, Jacob;
16 Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.
Jacob, Joseph, le mari de Marie, de laquelle naquit Jésus, qu'on appelle Christ.
17 Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.
Il y a donc, en tout, quatorze générations d'Abraham à David; quatorze, de David à l'émigration à Babylone, et quatorze, de l'émigration jusqu’à Christ.
18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Or, voici de quelle manière Jésus-Christ vint au monde. Marie, sa mère, ayant été fiancée à Joseph, se trouva enceinte par l'effet du Saint-Esprit, avant qu'ils eussent habité ensemble.
19 Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.
Joseph, son mari, étant un homme de bien, et ne voulant pas l'exposer à la honte, résolut de la répudier secrètement.
20 Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,'' Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
Il y pensait, lorsqu'un ange du Seigneur lui apparut en songe, et lui dit: «Joseph, fils de David, ne crains point de prendre chez toi Marie, ta femme; car l'enfant qu'elle a conçu est du Saint-Esprit.
21 Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.''
Elle mettra au monde un fils, et tu lui donneras le nom de Jésus, parce que c'est lui qui sauvera son peuple de ses péchés.»
22 Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,
Tout cela arriva, afin que s'accomplît ce qu'avait dit le Seigneur par le prophète:
23 “Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”— maana yake, “Mungu pamoja nasi.”
«Voici, la vierge sera enceinte; elle mettra au monde un fils à qui l’on donnera le nom d'Emmanuel, » ce qui signifie «Dieu avec nous.»
24 Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.
A son réveil, Joseph fit comme l'ange du Seigneur le lui avait commandé: il prit sa femme chez lui.
25 Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
Et il ne la connut point, jusqu’à ce qu'elle eût mis au monde un fils, et il lui donna le nom de Jésus.

< Mathayo 1 >