< Marko 9 >

1 Na alisema kwao, “Hakika nasema kwenu, baadhi yenu kuna watu waliosimama hapa hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
Et il ajouta: «En vérité je vous le dis, quelques-uns de ceux qui sont ici présents, ne goûteront point la mort, qu'ils n'aient vu le royaume de Dieu inauguré avec puissance.»
2 Na baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana pamoja naye mlimani, pekee yao. Ndipo alianza kubadilika mbele yao.
Six jours après, Jésus, ayant pris avec lui Pierre, Jacques et Jean, les mena sur une haute montagne, seuls, à l'écart, et il fut transfiguré devant eux:
3 Mavazi yake yakaanza kung'aa sana, meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.
ses vêtements devinrent éblouissants d'une blancheur telle, qu'il n'est pas un foulon sur la terre qui puisse blanchir ainsi.
4 Ndipo Eliya pamoja na Musa walitokea mbele yao, na walikuwa wakiongea na Yesu.
Puis Elie leur apparut avec Moïse; ils s'entretenaient avec Jésus.
5 Petro alijibu akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vyema sisi kuwa hapa, na tujenge vibanda vitatu, kimoja kwa ajili yako, kimoja kwa ajili Musa na kingine kwa ajili ya Eliya.”
Pierre, prenant la parole, dit à Jésus: «Rabbi, il est bon que nous soyons ici; dressons trois tentes, une pour toi, une pour Moïse, et une pour Élie.»
6 (Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana.)
Il ne savait ce qu'il disait: l'effroi les avait saisis tous trois.
7 Wingu lilitokea na kuwafunika. Ndipo sauti ikatoka mawinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
Une nuée survint qui les enveloppa, et il sortit de la nuée une voix: «Celui-ci est mon fils bien-aimé; écoutez-le.»
8 Ghafla, walipokuwa wakitazama, hawakumuona yeyote pamoja nao, isipokuwa Yesu tu.
Soudain, ayant jeté les regards autour d'eux, ils ne virent plus personne que Jésus, seul avec eux.
9 Walipokuwa wanateremka kutoka mlimani, aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
Comme ils descendaient de la montagne, Jésus leur recommanda de ne raconter à personne ce qu'ils avaient vu, avant que le Fils de l'homme fût ressuscité des morts.
10 Ndipo waliyatunza mambo wao wenyewe. Lakini walijadiliana wao kwa wao ni nini maana yake “kufufuliwa kutoka kwa wafu”
Les disciples retinrent cette recommandation, tout en discutant entre eux pour savoir ce que signifiait ce mot «être ressuscité des morts; »
11 Walimwuliza Yesu,”Kwa nini waandishi husema lazima Eliya aje kwanza?”
et ils adressèrent à Jésus cette question: «Pourquoi les scribes disent-ils qu'Elie doit venir premièrement?»
12 Akawaambia, “hakika Eliya atakuja kwanza kuokoa vitu vyote. Kwa nini imeandikwa Mwana wa Adamu lazima apate mateso mengi na achukiwe?
Il leur répondit: «Elie doit venir premièrement, et rétablir toutes choses! et d'où vient qu'il est écrit, que c'est afin que le Fils de l'homme souffre beaucoup, et qu'il soit rejeté avec mépris.
13 Lakini nasema kwenu Eliya alikwisha kuja, na walimfanya kama walivyopenda, kama vile maandiko yasemavyo kuhusu yeye.”
Mais je vous dis qu'Elie est venu, et qu'ils lui ont fait tout ce qu'ils ont voulu, selon qu'il est écrit à son sujet.»
14 Na waliporudi kwa wanafunzi, waliona kundi kubwa limewazunguka na Masadukayo walikuwa wanabishana nao.
Quand il arriva vers ses disciples, il vit une grande foule autour d'eux, et des scribes qui disputaient avec eux.
15 Na mara walipomwona, kundi lote lilishangaa na kumkimbilia kumsalimia.
Toute la foule fut surprise de le voir, et elle accourut pour le saluer.
16 Aliwauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao juu ya nini?”
Il leur demanda: «De quoi disputez-vous avec eux?»
17 Mmoja wao katika kundi alimjibu, “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako; ana roho chafu ambayo humfanya asiweze kuongea,
Et un homme de la foule lui répondit: «Maître, je t'ai amené mon fils qui est possédé d'un esprit muet:
18 na humsababishia kutetemeka na kumwangusha chini, na kutoka povu mdomoni na kusaga meno na kukakamaa. Niliwaomba wanafunzi wako kumtoa pepo, lakini hawakuweza.
en quelque lieu que cet esprit s'empare de lui, il le jette par terre; l'enfant écume, grince des dents, et dépérit. J'ai prié tes disciples de chasser l'esprit, et ils ne l'ont pu.»
19 Aliwajibu, “Kizazi kisichoamini, nitakaa nanyi kwa muda gani? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni kwangu.”
Jésus répondit, et leur dit: «Race incrédule, jusqu’à quand serai-je avec vous, jusqu’à quand vous supporterai-je?... Amenez-le moi.»
20 Walimleta mtoto wake. Roho mchafu alipomwona Yesu, ghafla ilimtia katika kutetemeka. Mvulana alianguka chini na kutoa povu mdomoni.
Et on le lui amena. Aussitôt que l'enfant vit Jésus, il fut jeté par l'esprit dans des convulsions, il tomba par terre et se roulait en écumant.
21 Yesu alimwuliza baba yake, “Amekuwa katika hali hii kwa muda gani?” Baba alisema, “Tangu utoto.
Jésus demanda au père: «Combien y a-t-il de temps que cela lui arrive?» — «Depuis son enfance, dit-il;
22 Mara nyingine huanguka katika moto au kwenye maji, na kujaribu kumwangamiza. Kama unaweza kufanya chochote tuhurumie na utusaidie.”
et souvent l'esprit l'a jeté soit dans le feu, soit dans l'eau, afin de le faire périr; mais si tu le peux, viens à notre secours par pitié pour nous.»
23 Yesu alimwambia, “Kama uko tayari? Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.”
Jésus lui répliqua: «Si je le peux! Tout est possible envers celui qui croit.»
24 Ghafla baba wa mtoto alilia na kusema, “Naamini! Nisaidie kutokuamini kwangu.”
Aussitôt le père de l'enfant s'écria: «Je crois; viens au secours de mon incrédulité!»
25 Wakati Yesu alipoona kundi linakimbilia kwao, alimkemea roho mchafu na kusema, “wewe roho bubu na kiziwi, nakuamuru mwache, usiingie kwake tena.”
Jésus, voyant la foule accourir, tança l'esprit impur, et lui dit: «Esprit muet et sourd, je te le commande, moi, sors de cet enfant, et n'y rentre plus.»
26 Alilia kwa nguvu na kumhangaisha mtoto na roho alimtoka. Mtoto alionekana kama amekufa, Ndipo wengi walisema, “Amekufa,”
Alors, ayant poussé un cri et causé de violentes convulsions, l'esprit sortit, et l'enfant devint comme un cadavre, au point que la plupart disaient: «Il est mort.»
27 Lakini Yesu alimchukua kwa mkono akamwinua, na mtoto alisimama.
Mais Jésus, le saisissant par la main, le releva, et il se tint debout.
28 Wakati Yesu alipoingia ndani, wanafunzi wake walimwuliza faragha, “Kwa nini hatukuweza kumtoa?”
Jésus étant rentré chez lui, ses disciples lui demandèrent en particulier: «Pourquoi n'avons-nous pu chasser cet esprit?»
29 Aliwaambia, “kwa namna hii hatoki isipokuwa kwa maombi.”
Il leur dit: «Rien, excepté la prière, ne peut faire sortir cette espèce de démons.»
30 Walitoka pale na kupitia Galilaya. Hakutaka mtu yeyote ajue walipo,
Etant partis de là, ils cheminèrent à travers la Galilée, et Jésus ne voulait pas qu'on le sût,
31 kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Adamu atafikishwa mikononi mwa watu, na watamuua. Atakapokuwa amekufa, baada ya siku tatu atafufuka tena.”
parce qu'il enseignait ses disciples. Il leur disait: «Le Fils de l'homme va être livré entre les mains des hommes, et ils le mettront à mort; mais, lorsqu'il aura été mis à mort, trois jours après, il ressuscitera.»
32 Lakini hawakuelewa maelezo haya, na waliogopa kumwuliza.
Mais eux ne comprenaient point cette parole, et ils craignaient de l'interroger.
33 Ndipo walifika Karperinaumu. Wakati akiwa ndani ya nyumba aliwauliza, ''Mlikuwa mnajadili nini njiani”?
Jésus rentra à Capernaoum. Quand il fut chez lui, il leur demanda: «De quoi vous entreteniez-vous en chemin?»
34 Lakini walikuwa kimya. Kwani walikuwa wanabishana njiani kwamba nani alikuwa mkubwa zaidi.
Mais ils gardèrent le silence, parce qu'en chemin ils avaient débattu entre eux cette question: «Qui est le plus grand?»
35 Alikaa chini akawaita kumi na wawili pamoja, na alisema nao, “Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
Jésus s'étant assis, appela les Douze, et leur dit: «Si quelqu'un veut être le premier, il sera le dernier de tous et le serviteur de tous.»
36 Alimchukua mtoto mdogo akamweka katikati yao. Akamchukua katika mikono yake, akasema,
Puis, il prit un petit enfant, le plaça au milieu d'eux, et, l'ayant embrassé, il leur dit:
37 “Yeyote ampokeaye mtoto kama huyu kwa jina langu, pia amenipokea mimi, na ikiwa mtu amenipokea, hanipokei mimi tu, lakini pia aliyenituma.”
«Celui qui reçoit un de ces enfants-là en mon nom, me reçoit; et celui qui me reçoit, reçoit non, pas moi, mais celui qui m'a envoyé.»
38 Yohana alimwambia, “Mwalimu tulimwona mtu anatoa pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu hatufuati.”
Jean, prenant la parole, lui dit: «Maître, nous avons vu un homme qui ne va pas avec nous, chasser les démons en ton nom, et nous l'en avons empêché, parce qu'il ne va pas avec nous.»
39 Lakini Yesu alisema, “Msimzuie, kwa kuwa hakuna atakayefanya kazi kubwa kwa jina langu na ndipo baadaye aseme neno baya lolote juu yangu.
Mais Jésus dit: «Ne l'en empêchez pas, car il n'est personne qui, après avoir fait un miracle en mon nom, puisse, aussitôt après, dire du mal de moi.
40 Yeyote asiyekuwa kinyume nasi yuko upande wetu.
Qui n'est pas contre nous est pour nous.
41 Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo, kweli nawaambia, hatapoteza thawabu yake.
Car celui qui vous donnera un verre d'eau pour le nom de Christ à qui vous êtes, je vous dis en vérité qu'il ne perdra point sa récompense.
42 Yeyote anayewakosesha hawa wadogo waniaminio mimi, ingekuwa vyema kwake kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa baharini.
Si quelqu'un devait être une occasion de chute pour un seul des petits qui ont la foi, il vaudrait mieux pour lui, qu'on lui mît une pierre de moulin autour du cou, et qu'on le jetât dans la mer.
43 Kama mkono wako ukikukosesha ukate. Ni heri kuingia katika uzima bila mkono kuliko kuingia kwenye hukumu ukiwa na mikono yote. Katika moto “usiozimika”. (Geenna g1067)
Si ta main est pour toi une occasion de chute, coupe-la; il te vaut mieux entrer manchot dans la vie, que d'avoir deux mains, et d'aller dans la Géhenne, dans le feu qui ne s'éteint point. (Geenna g1067)
44 (Zingatia: Mstari hii, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usiozimika.” haumo katika nakala za kale).
45 Kama mguu wako ukikukosesha, ukate. Ni vyema kwako kuingia uzimani ukiwa kilema, kuliko kutupwa hukumuni na miguu miwili. (Geenna g1067)
Si ton pied est pour toi une occasion de chute, coupe-le; il te vaut mieux entrer boiteux dans la vie, que d'avoir deux pieds, et d'être jeté dans la Géhenne. (Geenna g1067)
46 (Zingatia: Mstari huu, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usioweza kuzimika” haumo kwenye nakala za kale).
47 Kama jicho lako likikukosesha ling'oe. Ni vyema kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa kuzimu. (Geenna g1067)
Si ton oeil est pour toi une occasion de chute, arrache-le; il te vaut mieux entrer borgne dans le royaume de Dieu, que d'avoir deux yeux, et d'être jeté dans la Géhenne, (Geenna g1067)
48 Mahali palipo na funza wasiokufa, na moto usiozimika.
«où le ver ne meurt point, et on le feu ne s'éteint point.»
49 Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.
Car tout homme sera salé par le feu, et tout sacrifice sera salé avec du sel.
50 Chumvi ni nzuri, kama chumvi ikipoteza ladha yake, utaifanyaje iwe na ladha yake tena? Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe, na muwe na amani kwa kila mmoja.”
C'est une bonne chose que le sel; mais s'il devient insipide, avec quoi lui donnerez-vous de la saveur? Gardez bien le sel en vous, et soyez en paix les uns avec les autres.»

< Marko 9 >