< Marko 9 >

1 Na alisema kwao, “Hakika nasema kwenu, baadhi yenu kuna watu waliosimama hapa hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
And he said to them, 'Verily I say to you, That there are certain of those standing here, who may not taste of death till they see the reign of God having come in power.'
2 Na baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana pamoja naye mlimani, pekee yao. Ndipo alianza kubadilika mbele yao.
And after six days doth Jesus take Peter, and James, and John, and bringeth them up to a high mount by themselves, alone, and he was transfigured before them,
3 Mavazi yake yakaanza kung'aa sana, meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.
and his garments became glittering, white exceedingly, as snow, so as a fuller upon the earth is not able to whiten [them].
4 Ndipo Eliya pamoja na Musa walitokea mbele yao, na walikuwa wakiongea na Yesu.
And there appeared to them Elijah with Moses, and they were talking with Jesus.
5 Petro alijibu akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vyema sisi kuwa hapa, na tujenge vibanda vitatu, kimoja kwa ajili yako, kimoja kwa ajili Musa na kingine kwa ajili ya Eliya.”
And Peter answering saith to Jesus, 'Rabbi, it is good to us to be here; and we may make three booths, for thee one, and for Moses one, and for Elijah one:'
6 (Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana.)
for he was not knowing what he might say, for they were greatly afraid.
7 Wingu lilitokea na kuwafunika. Ndipo sauti ikatoka mawinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
And there came a cloud overshadowing them, and there came a voice out of the cloud, saying, 'This is My Son — the Beloved, hear ye him;'
8 Ghafla, walipokuwa wakitazama, hawakumuona yeyote pamoja nao, isipokuwa Yesu tu.
and suddenly, having looked around, they saw no one any more, but Jesus only with themselves.
9 Walipokuwa wanateremka kutoka mlimani, aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
And as they are coming down from the mount, he charged them that they may declare to no one the things that they saw, except when the Son of Man may rise out of the dead;
10 Ndipo waliyatunza mambo wao wenyewe. Lakini walijadiliana wao kwa wao ni nini maana yake “kufufuliwa kutoka kwa wafu”
and the thing they kept to themselves, questioning together what the rising out of the dead is.
11 Walimwuliza Yesu,”Kwa nini waandishi husema lazima Eliya aje kwanza?”
And they were questioning him, saying, that the scribes say that Elijah it behoveth to come first.
12 Akawaambia, “hakika Eliya atakuja kwanza kuokoa vitu vyote. Kwa nini imeandikwa Mwana wa Adamu lazima apate mateso mengi na achukiwe?
And he answering said to them, 'Elijah indeed, having come first, doth restore all things; and how hath it been written concerning the Son of Man, that many things he may suffer, and be set at nought?
13 Lakini nasema kwenu Eliya alikwisha kuja, na walimfanya kama walivyopenda, kama vile maandiko yasemavyo kuhusu yeye.”
But I say to you, That also Elijah hath come, and they did to him what they willed, as it hath been written of him.'
14 Na waliporudi kwa wanafunzi, waliona kundi kubwa limewazunguka na Masadukayo walikuwa wanabishana nao.
And having come unto the disciples, he saw a great multitude about them, and scribes questioning with them,
15 Na mara walipomwona, kundi lote lilishangaa na kumkimbilia kumsalimia.
and immediately, all the multitude having seen him, were amazed, and running near, were saluting him.
16 Aliwauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao juu ya nini?”
And he questioned the scribes, 'What dispute ye with them?'
17 Mmoja wao katika kundi alimjibu, “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako; ana roho chafu ambayo humfanya asiweze kuongea,
and one out of the multitude answering said, 'Teacher, I brought my son unto thee, having a dumb spirit;
18 na humsababishia kutetemeka na kumwangusha chini, na kutoka povu mdomoni na kusaga meno na kukakamaa. Niliwaomba wanafunzi wako kumtoa pepo, lakini hawakuweza.
and wherever it doth seize him, it doth tear him, and he foameth, and gnasheth his teeth, and pineth away; and I spake to thy disciples that they may cast it out, and they were not able.'
19 Aliwajibu, “Kizazi kisichoamini, nitakaa nanyi kwa muda gani? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni kwangu.”
And he answering him, said, 'O generation unbelieving, till when shall I be with you? till when shall I suffer you? bring him unto me;'
20 Walimleta mtoto wake. Roho mchafu alipomwona Yesu, ghafla ilimtia katika kutetemeka. Mvulana alianguka chini na kutoa povu mdomoni.
and they brought him unto him, and he having seen him, immediately the spirit tare him, and he, having fallen upon the earth, was wallowing — foaming.
21 Yesu alimwuliza baba yake, “Amekuwa katika hali hii kwa muda gani?” Baba alisema, “Tangu utoto.
And he questioned his father, 'How long time is it since this came to him?' and he said, 'From childhood,
22 Mara nyingine huanguka katika moto au kwenye maji, na kujaribu kumwangamiza. Kama unaweza kufanya chochote tuhurumie na utusaidie.”
and many times also it cast him into fire, and into water, that it might destroy him; but if thou art able to do anything, help us, having compassion on us.'
23 Yesu alimwambia, “Kama uko tayari? Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.”
And Jesus said to him, 'If thou art able to believe! all things are possible to the one that is believing;'
24 Ghafla baba wa mtoto alilia na kusema, “Naamini! Nisaidie kutokuamini kwangu.”
and immediately the father of the child, having cried out, with tears said, 'I believe, sir; be helping mine unbelief.'
25 Wakati Yesu alipoona kundi linakimbilia kwao, alimkemea roho mchafu na kusema, “wewe roho bubu na kiziwi, nakuamuru mwache, usiingie kwake tena.”
Jesus having seen that a multitude doth run together, rebuked the unclean spirit, saying to it, 'Spirit — dumb and deaf — I charge thee, come forth out of him, and no more thou mayest enter into him;'
26 Alilia kwa nguvu na kumhangaisha mtoto na roho alimtoka. Mtoto alionekana kama amekufa, Ndipo wengi walisema, “Amekufa,”
and having cried, and rent him much, it came forth, and he became as dead, so that many said that he was dead,
27 Lakini Yesu alimchukua kwa mkono akamwinua, na mtoto alisimama.
but Jesus, having taken him by the hand, lifted him up, and he arose.
28 Wakati Yesu alipoingia ndani, wanafunzi wake walimwuliza faragha, “Kwa nini hatukuweza kumtoa?”
And he having come into the house, his disciples were questioning him by himself — 'Why were we not able to cast it forth?'
29 Aliwaambia, “kwa namna hii hatoki isipokuwa kwa maombi.”
And he said to them, 'This kind is able to come forth with nothing except with prayer and fasting.'
30 Walitoka pale na kupitia Galilaya. Hakutaka mtu yeyote ajue walipo,
And having gone forth thence, they were passing through Galilee, and he did not wish that any may know,
31 kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Adamu atafikishwa mikononi mwa watu, na watamuua. Atakapokuwa amekufa, baada ya siku tatu atafufuka tena.”
for he was teaching his disciples, and he said to them, 'The Son of Man is being delivered to the hands of men, and they shall kill him, and having been killed the third day he shall rise,'
32 Lakini hawakuelewa maelezo haya, na waliogopa kumwuliza.
but they were not understanding the saying, and they were afraid to question him.
33 Ndipo walifika Karperinaumu. Wakati akiwa ndani ya nyumba aliwauliza, ''Mlikuwa mnajadili nini njiani”?
And he came to Capernaum, and being in the house, he was questioning them, 'What were ye reasoning in the way among yourselves?'
34 Lakini walikuwa kimya. Kwani walikuwa wanabishana njiani kwamba nani alikuwa mkubwa zaidi.
and they were silent, for with one another they did reason in the way who is greater;
35 Alikaa chini akawaita kumi na wawili pamoja, na alisema nao, “Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
and having sat down he called the twelve, and he saith to them, 'If any doth will to be first, he shall be last of all, and minister of all.'
36 Alimchukua mtoto mdogo akamweka katikati yao. Akamchukua katika mikono yake, akasema,
And having taken a child, he set him in the midst of them, and having taken him in his arms, said to them,
37 “Yeyote ampokeaye mtoto kama huyu kwa jina langu, pia amenipokea mimi, na ikiwa mtu amenipokea, hanipokei mimi tu, lakini pia aliyenituma.”
'Whoever may receive one of such children in my name, doth receive me, and whoever may receive me, doth not receive me, but Him who sent me.'
38 Yohana alimwambia, “Mwalimu tulimwona mtu anatoa pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu hatufuati.”
And John did answer him, saying, 'Teacher, we saw a certain one in thy name casting out demons, who doth not follow us, and we forbade him, because he doth not follow us.'
39 Lakini Yesu alisema, “Msimzuie, kwa kuwa hakuna atakayefanya kazi kubwa kwa jina langu na ndipo baadaye aseme neno baya lolote juu yangu.
And Jesus said, 'Forbid him not, for there is no one who shall do a mighty work in my name, and shall be able readily to speak evil of me:
40 Yeyote asiyekuwa kinyume nasi yuko upande wetu.
for he who is not against us is for us;
41 Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo, kweli nawaambia, hatapoteza thawabu yake.
for whoever may give you to drink a cup of water in my name, because ye are Christ's, verily I say to you, he may not lose his reward;
42 Yeyote anayewakosesha hawa wadogo waniaminio mimi, ingekuwa vyema kwake kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa baharini.
and whoever may cause to stumble one of the little ones believing in me, better is it for him if a millstone is hanged about his neck, and he hath been cast into the sea.
43 Kama mkono wako ukikukosesha ukate. Ni heri kuingia katika uzima bila mkono kuliko kuingia kwenye hukumu ukiwa na mikono yote. Katika moto “usiozimika”. (Geenna g1067)
'And if thy hand may cause thee to stumble, cut it off; it is better for thee maimed to enter into the life, than having the two hands, to go away to the gehenna, to the fire — the unquenchable — (Geenna g1067)
44 (Zingatia: Mstari hii, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usiozimika.” haumo katika nakala za kale).
where their worm is not dying, and the fire is not being quenched.
45 Kama mguu wako ukikukosesha, ukate. Ni vyema kwako kuingia uzimani ukiwa kilema, kuliko kutupwa hukumuni na miguu miwili. (Geenna g1067)
'And if thy foot may cause thee to stumble, cut it off; it is better for thee to enter into the life lame, than having the two feet to be cast to the gehenna, to the fire — the unquenchable — (Geenna g1067)
46 (Zingatia: Mstari huu, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usioweza kuzimika” haumo kwenye nakala za kale).
where their worm is not dying, and the fire is not being quenched.
47 Kama jicho lako likikukosesha ling'oe. Ni vyema kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa kuzimu. (Geenna g1067)
And if thine eye may cause thee to stumble, cast it out; it is better for thee one-eyed to enter into the reign of God, than having two eyes, to be cast to the gehenna of the fire — (Geenna g1067)
48 Mahali palipo na funza wasiokufa, na moto usiozimika.
where their worm is not dying, and the fire is not being quenched;
49 Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.
for every one with fire shall be salted, and every sacrifice with salt shall be salted.
50 Chumvi ni nzuri, kama chumvi ikipoteza ladha yake, utaifanyaje iwe na ladha yake tena? Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe, na muwe na amani kwa kila mmoja.”
The salt [is] good, but if the salt may become saltless, in what will ye season [it]? Have in yourselves salt, and have peace in one another.'

< Marko 9 >