< Marko 9 >
1 Na alisema kwao, “Hakika nasema kwenu, baadhi yenu kuna watu waliosimama hapa hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
And he seide to hem, Treuli Y seie to you, that there ben summen stondynge here, whiche schulen not taste deth, til thei seen the rewme of God comynge in vertu.
2 Na baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana pamoja naye mlimani, pekee yao. Ndipo alianza kubadilika mbele yao.
And aftir sixe daies Jhesus took Petre, and James, and Joon, and ledde hem bi hem silf aloone in to an hiy hille; and he was transfigurid bifor hem.
3 Mavazi yake yakaanza kung'aa sana, meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.
And hise clothis weren maad ful schynynge and white as snow, whiche maner white clothis a fuller may not make on erthe.
4 Ndipo Eliya pamoja na Musa walitokea mbele yao, na walikuwa wakiongea na Yesu.
And Helie with Moises apperide to hem, and thei spaken with Jhesu.
5 Petro alijibu akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vyema sisi kuwa hapa, na tujenge vibanda vitatu, kimoja kwa ajili yako, kimoja kwa ajili Musa na kingine kwa ajili ya Eliya.”
And Petre answeride, and seide to Jhesu, Maister, it is good vs to be here; and make we here thre tabernaclis, oon to thee, oon to Moyses, and oon to Helie.
6 (Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana.)
For he wiste not what he schulde seie; for thei weren agaste bi drede.
7 Wingu lilitokea na kuwafunika. Ndipo sauti ikatoka mawinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
And ther was maad a cloude overschadewynge hem; and a vois cam of the cloude, and seide, This is my moost derworth sone, here ye hym.
8 Ghafla, walipokuwa wakitazama, hawakumuona yeyote pamoja nao, isipokuwa Yesu tu.
And anoon thei bihelden aboute, and sayn no more ony man, but Jhesu oonli with hem.
9 Walipokuwa wanateremka kutoka mlimani, aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
And whanne thei camen doun fro the hille, he comaundide hem, that thei schulden not telle to ony man tho thingis that thei hadden seen, but whanne mannus sone hath risun ayen fro deeth.
10 Ndipo waliyatunza mambo wao wenyewe. Lakini walijadiliana wao kwa wao ni nini maana yake “kufufuliwa kutoka kwa wafu”
And thei helden the word at hem silf, sekynge what this schulde be, whanne he hadde risun ayen fro deth.
11 Walimwuliza Yesu,”Kwa nini waandishi husema lazima Eliya aje kwanza?”
And thei axiden hym, and seiden, What thanne seien Farisees and scribis, for it bihoueth `Helie to come first.
12 Akawaambia, “hakika Eliya atakuja kwanza kuokoa vitu vyote. Kwa nini imeandikwa Mwana wa Adamu lazima apate mateso mengi na achukiwe?
And he answeride, and seide to hem, Whanne Helie cometh, he schal first restore alle thingis; and as it is writun of mannus sone, that he suffre many thingis, and be dispisid.
13 Lakini nasema kwenu Eliya alikwisha kuja, na walimfanya kama walivyopenda, kama vile maandiko yasemavyo kuhusu yeye.”
And Y seie to you, that Helie is comun, and thei diden to hym what euer thingis thei wolden, as it is writun of hym.
14 Na waliporudi kwa wanafunzi, waliona kundi kubwa limewazunguka na Masadukayo walikuwa wanabishana nao.
And he comynge to hise disciplis, saiy a greet cumpany aboute hem, and scribis disputynge with hem.
15 Na mara walipomwona, kundi lote lilishangaa na kumkimbilia kumsalimia.
And anoon al the puple seynge Jhesu, was astonyed, and thei dredden; and thei rennynge gretten hym.
16 Aliwauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao juu ya nini?”
And he axide hem, What disputen ye among you?
17 Mmoja wao katika kundi alimjibu, “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako; ana roho chafu ambayo humfanya asiweze kuongea,
And oon of the cumpany answerde, and seide, Mayster, Y haue brouyt to thee my sone, that hath a doumbe spirit; and where euer he takith hym,
18 na humsababishia kutetemeka na kumwangusha chini, na kutoka povu mdomoni na kusaga meno na kukakamaa. Niliwaomba wanafunzi wako kumtoa pepo, lakini hawakuweza.
he hurtlith hym doun, and he fometh, and betith togidir with teeth, and wexith drye. And Y seide to thi disciplis, that thei schulden caste hym out, and thei myyten not.
19 Aliwajibu, “Kizazi kisichoamini, nitakaa nanyi kwa muda gani? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni kwangu.”
And he answeride to hem, and seide, A! thou generacioun out of bileue, hou longe schal Y be among you, hou longe schal Y suffre you? Brynge ye hym to me.
20 Walimleta mtoto wake. Roho mchafu alipomwona Yesu, ghafla ilimtia katika kutetemeka. Mvulana alianguka chini na kutoa povu mdomoni.
And thei brouyten hym. And whanne he had seyn him, anoon the spirit troublide him; and was throw doun to grounde, and walewide, and fomede.
21 Yesu alimwuliza baba yake, “Amekuwa katika hali hii kwa muda gani?” Baba alisema, “Tangu utoto.
And he axide his fadir, Hou longe `is it, sith this `hath falle to hym? And he seide, Fro childhode;
22 Mara nyingine huanguka katika moto au kwenye maji, na kujaribu kumwangamiza. Kama unaweza kufanya chochote tuhurumie na utusaidie.”
and ofte he hath put hym in to fier, and in to watir, to leese hym; but if thou maiste ony thing, helpe vs, and haue merci on vs.
23 Yesu alimwambia, “Kama uko tayari? Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.”
And Jhesus seide to hym, If thou maiste bileue, alle thingis ben possible to man that bileueth.
24 Ghafla baba wa mtoto alilia na kusema, “Naamini! Nisaidie kutokuamini kwangu.”
And anoon the fadir of the child criede with teeris, and seide, Lord, Y bileue; Lord, helpe thou myn vnbileue.
25 Wakati Yesu alipoona kundi linakimbilia kwao, alimkemea roho mchafu na kusema, “wewe roho bubu na kiziwi, nakuamuru mwache, usiingie kwake tena.”
And whanne Jhesus hadde seyn the puple rennynge togidere, he manasside the vnclene spirit, and seide to hym, Thou deef and doumbe spirit, Y comaunde thee, go out fro hym, and entre no more in to hym.
26 Alilia kwa nguvu na kumhangaisha mtoto na roho alimtoka. Mtoto alionekana kama amekufa, Ndipo wengi walisema, “Amekufa,”
And he criynge, and myche to breidynge him, wente out fro hym; and he was maad as deed, so that many seiden, that he was deed.
27 Lakini Yesu alimchukua kwa mkono akamwinua, na mtoto alisimama.
And Jhesus helde his hoond, and lifte hym vp; and he roos.
28 Wakati Yesu alipoingia ndani, wanafunzi wake walimwuliza faragha, “Kwa nini hatukuweza kumtoa?”
And whanne he hadde entrid in to an hous, hise disciplis axiden hym priueli, Whi myyten not we caste hym out?
29 Aliwaambia, “kwa namna hii hatoki isipokuwa kwa maombi.”
And he seide to hem, This kynde in no thing may go out, but in preier and fastyng.
30 Walitoka pale na kupitia Galilaya. Hakutaka mtu yeyote ajue walipo,
And thei yeden fro thennus, and wente forth in to Galile; and thei wolden not, that ony man wiste.
31 kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Adamu atafikishwa mikononi mwa watu, na watamuua. Atakapokuwa amekufa, baada ya siku tatu atafufuka tena.”
And he tauyte hise disciplis, and seide to hem, For mannus sone schal be bitrayed in to the hondis of men, and thei schulen sle hym, and he slayn schal ryse ayen on the thridde day.
32 Lakini hawakuelewa maelezo haya, na waliogopa kumwuliza.
And thei knewen not the word, and dredden to axe hym.
33 Ndipo walifika Karperinaumu. Wakati akiwa ndani ya nyumba aliwauliza, ''Mlikuwa mnajadili nini njiani”?
And thei camen to Cafarnaum. And whanne thei weren in the hous, he axide hem, What tretiden ye in the weie?
34 Lakini walikuwa kimya. Kwani walikuwa wanabishana njiani kwamba nani alikuwa mkubwa zaidi.
And thei weren stille; for thei disputiden among hem in the weie, who of hem schulde be grettest.
35 Alikaa chini akawaita kumi na wawili pamoja, na alisema nao, “Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
And he sat, and clepide the twelue, and seide to hem, If ony man wole be the firste among you, he schal be the laste of alle, and the mynyster of alle.
36 Alimchukua mtoto mdogo akamweka katikati yao. Akamchukua katika mikono yake, akasema,
And he took a child, and sette hym in the myddil of hem; and whanne he hadde biclippid hym, he seide to hem,
37 “Yeyote ampokeaye mtoto kama huyu kwa jina langu, pia amenipokea mimi, na ikiwa mtu amenipokea, hanipokei mimi tu, lakini pia aliyenituma.”
Who euer resseyueth oon of such children in my name, he resseyueth me; and who euer resseyueth me, he resseyueth not me aloone, but hym that sente me.
38 Yohana alimwambia, “Mwalimu tulimwona mtu anatoa pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu hatufuati.”
Joon answeride to hym, and seide, Maister, we sayn oon castynge out feendis in thi name, which sueth not vs, and we han forbodun hym.
39 Lakini Yesu alisema, “Msimzuie, kwa kuwa hakuna atakayefanya kazi kubwa kwa jina langu na ndipo baadaye aseme neno baya lolote juu yangu.
And Jhesus seide, Nyle ye forbede him; for ther is no man that doith vertu in my name, and may soone speke yuel of me.
40 Yeyote asiyekuwa kinyume nasi yuko upande wetu.
He that is not ayens vs, is for vs.
41 Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo, kweli nawaambia, hatapoteza thawabu yake.
And who euer yyueth you a cuppe of coold water to drynke in my name, for ye ben of Crist, treuli Y seie to you, he schal not leese his mede.
42 Yeyote anayewakosesha hawa wadogo waniaminio mimi, ingekuwa vyema kwake kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa baharini.
And who euer schal sclaundre oon of these litle that bileuen in me, it were betere to hym that a mylne stoon `of assis were don aboute his necke, and he were cast in to the see.
43 Kama mkono wako ukikukosesha ukate. Ni heri kuingia katika uzima bila mkono kuliko kuingia kwenye hukumu ukiwa na mikono yote. Katika moto “usiozimika”. (Geenna )
And if thin hoond sclaundre thee, kitte it awey; it is betere to thee to entre feble in to lijf, than haue two hondis, and go in to helle, in to fier that neuer schal be quenchid, (Geenna )
44 (Zingatia: Mstari hii, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usiozimika.” haumo katika nakala za kale).
where the worm of hem dieth not, and the fier is not quenchid.
45 Kama mguu wako ukikukosesha, ukate. Ni vyema kwako kuingia uzimani ukiwa kilema, kuliko kutupwa hukumuni na miguu miwili. (Geenna )
And if thi foote sclaundre thee, kitte it of; it is betere to thee to entre crokid in to euerlastynge lijf, than haue twei feet, and be sent in to helle of fier, that neuer schal be quenchid, (Geenna )
46 (Zingatia: Mstari huu, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usioweza kuzimika” haumo kwenye nakala za kale).
where the worme of hem dieth not, and the fier is not quenchid.
47 Kama jicho lako likikukosesha ling'oe. Ni vyema kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa kuzimu. (Geenna )
That if thin iye sclaundre thee, cast it out; it is betere to thee to entre gogil iyed in to the reume of God, than haue twey iyen, and be sent in to helle of fier, where the worme of hem dieth not, (Geenna )
48 Mahali palipo na funza wasiokufa, na moto usiozimika.
and the fier is not quenchid.
49 Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.
And euery man schal be saltid with fier, and euery slayn sacrifice schal be maad sauery with salt.
50 Chumvi ni nzuri, kama chumvi ikipoteza ladha yake, utaifanyaje iwe na ladha yake tena? Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe, na muwe na amani kwa kila mmoja.”
Salt is good; if salt be vnsauery, in what thing schulen ye make it sauery? Haue ye salt among you, and haue ye pees among you.