< Marko 9 >

1 Na alisema kwao, “Hakika nasema kwenu, baadhi yenu kuna watu waliosimama hapa hawataonja mauti kabla ya kuuona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
And he said to them, “Truly I say to you, there are some standing here who will certainly not taste death until they see the kingdom of God come with power.”
2 Na baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana pamoja naye mlimani, pekee yao. Ndipo alianza kubadilika mbele yao.
After six days Jesus took Peter, James, and John, and led them up on a high mountain by themselves. There he was transfigured before them.
3 Mavazi yake yakaanza kung'aa sana, meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.
His garments became radiant and extremely white, like snow, such as no launderer on earth could whiten them.
4 Ndipo Eliya pamoja na Musa walitokea mbele yao, na walikuwa wakiongea na Yesu.
Then Elijah appeared to them with Moses, and they were talking with Jesus.
5 Petro alijibu akamwambia Yesu, “Mwalimu, ni vyema sisi kuwa hapa, na tujenge vibanda vitatu, kimoja kwa ajili yako, kimoja kwa ajili Musa na kingine kwa ajili ya Eliya.”
So Peter said to Jesus, “Rabbi, it is good for us to be here. Let us make three shelters, one for yoʋ, one for Moses, and one for Elijah.”
6 (Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana.)
(For they were terrified, and he did not know what to say.)
7 Wingu lilitokea na kuwafunika. Ndipo sauti ikatoka mawinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni yeye.”
Then a cloud came and overshadowed them, and a voice came from the cloud: “This is my beloved Son; listen to him!”
8 Ghafla, walipokuwa wakitazama, hawakumuona yeyote pamoja nao, isipokuwa Yesu tu.
And suddenly, when they looked around, they no longer saw anyone with them but Jesus.
9 Walipokuwa wanateremka kutoka mlimani, aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
As they were coming down from the mountain, Jesus ordered them to tell no one what they had seen until the Son of Man had risen from the dead.
10 Ndipo waliyatunza mambo wao wenyewe. Lakini walijadiliana wao kwa wao ni nini maana yake “kufufuliwa kutoka kwa wafu”
So they kept the matter to themselves, discussing what this “rising from the dead” could mean.
11 Walimwuliza Yesu,”Kwa nini waandishi husema lazima Eliya aje kwanza?”
Then they asked him, “Why do the scribes say that Elijah must come first?”
12 Akawaambia, “hakika Eliya atakuja kwanza kuokoa vitu vyote. Kwa nini imeandikwa Mwana wa Adamu lazima apate mateso mengi na achukiwe?
He answered them, “Elijah does indeed come first to restore all things. How then is it written that the Son of Man must suffer many things and be treated with contempt?
13 Lakini nasema kwenu Eliya alikwisha kuja, na walimfanya kama walivyopenda, kama vile maandiko yasemavyo kuhusu yeye.”
But I tell you that Elijah has indeed come, and they did to him whatever they wanted, just as it is written about him.”
14 Na waliporudi kwa wanafunzi, waliona kundi kubwa limewazunguka na Masadukayo walikuwa wanabishana nao.
When Jesus came back to the other disciples, he saw a large crowd around them, and some scribes arguing with them.
15 Na mara walipomwona, kundi lote lilishangaa na kumkimbilia kumsalimia.
When the whole crowd saw him, they were greatly amazed and immediately ran up and greeted him.
16 Aliwauliza wanafunzi wake, “Mnabishana nao juu ya nini?”
Then he asked the scribes, “What are you arguing with them about?”
17 Mmoja wao katika kundi alimjibu, “Mwalimu, nilimleta mwanangu kwako; ana roho chafu ambayo humfanya asiweze kuongea,
One man from among the crowd answered, “Teacher, I brought yoʋ my son, who has a spirit that makes him mute.
18 na humsababishia kutetemeka na kumwangusha chini, na kutoka povu mdomoni na kusaga meno na kukakamaa. Niliwaomba wanafunzi wako kumtoa pepo, lakini hawakuweza.
Whenever it seizes him, it throws him down, and he foams at the mouth, grinds his teeth, and becomes rigid. I asked yoʋr disciples to cast it out, but they were not able to do so.”
19 Aliwajibu, “Kizazi kisichoamini, nitakaa nanyi kwa muda gani? Nitachukuliana nanyi hadi lini? Mleteni kwangu.”
Jesus answered him, “O faithless generation, how long shall I be with you? How long shall I bear with you? Bring him to me.”
20 Walimleta mtoto wake. Roho mchafu alipomwona Yesu, ghafla ilimtia katika kutetemeka. Mvulana alianguka chini na kutoa povu mdomoni.
So they brought the boy to him. When the spirit saw Jesus, it immediately threw the boy into convulsions, and he fell on the ground and rolled around, foaming at the mouth.
21 Yesu alimwuliza baba yake, “Amekuwa katika hali hii kwa muda gani?” Baba alisema, “Tangu utoto.
Then Jesus asked the boy's father, “How long has this been happening to him?” The father said, “From childhood.
22 Mara nyingine huanguka katika moto au kwenye maji, na kujaribu kumwangamiza. Kama unaweza kufanya chochote tuhurumie na utusaidie.”
It often throws him into the fire and into the water, to destroy him. But if yoʋ are able to do anything, help us and have compassion on us.”
23 Yesu alimwambia, “Kama uko tayari? Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.”
Jesus said to him, “The question is whether yoʋ are able to believe. All things are possible for the one who believes.”
24 Ghafla baba wa mtoto alilia na kusema, “Naamini! Nisaidie kutokuamini kwangu.”
Immediately the child's father cried out and said with tears, “I believe, Lord; help my unbelief!”
25 Wakati Yesu alipoona kundi linakimbilia kwao, alimkemea roho mchafu na kusema, “wewe roho bubu na kiziwi, nakuamuru mwache, usiingie kwake tena.”
When Jesus saw that a crowd came running together, he rebuked the unclean spirit and said to it, “Yoʋ spirit that makes this boy mute and deaf, I command yoʋ, come out of him and never enter him again!”
26 Alilia kwa nguvu na kumhangaisha mtoto na roho alimtoka. Mtoto alionekana kama amekufa, Ndipo wengi walisema, “Amekufa,”
After crying out, the spirit convulsed the boy greatly and came out, and the boy became as though he were dead, so that many said, “He is dead!”
27 Lakini Yesu alimchukua kwa mkono akamwinua, na mtoto alisimama.
But Jesus took him by the hand and raised him up, and the boy arose.
28 Wakati Yesu alipoingia ndani, wanafunzi wake walimwuliza faragha, “Kwa nini hatukuweza kumtoa?”
Now when Jesus came into the house, his disciples asked him privately, “Why could we not cast it out?”
29 Aliwaambia, “kwa namna hii hatoki isipokuwa kwa maombi.”
He said to them, “This kind cannot come out by anything except prayer and fasting.”
30 Walitoka pale na kupitia Galilaya. Hakutaka mtu yeyote ajue walipo,
Then they went away from there and passed through Galilee, but Jesus did not want anyone to know it.
31 kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake. Aliwaambia, “Mwana wa Adamu atafikishwa mikononi mwa watu, na watamuua. Atakapokuwa amekufa, baada ya siku tatu atafufuka tena.”
For he was teaching his disciples and telling them, “The Son of Man is going to be delivered up into the hands of men, and they will kill him. Yet after he has been killed, he will rise on the third day.”
32 Lakini hawakuelewa maelezo haya, na waliogopa kumwuliza.
But they did not understand what this meant, and they were afraid to ask him about it.
33 Ndipo walifika Karperinaumu. Wakati akiwa ndani ya nyumba aliwauliza, ''Mlikuwa mnajadili nini njiani”?
Then Jesus came to Capernaum, and when he was in the house, he asked the disciples, “What were you discussing among yourselves on the way?”
34 Lakini walikuwa kimya. Kwani walikuwa wanabishana njiani kwamba nani alikuwa mkubwa zaidi.
But they were silent, because on the way they had been arguing with one another about who was greater.
35 Alikaa chini akawaita kumi na wawili pamoja, na alisema nao, “Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.”
So Jesus sat down, called the twelve over, and said to them, “If anyone wants to be first, he must be last of all and a servant to all.”
36 Alimchukua mtoto mdogo akamweka katikati yao. Akamchukua katika mikono yake, akasema,
Then he took a child and placed him before them. And taking the child in his arms, he said to them,
37 “Yeyote ampokeaye mtoto kama huyu kwa jina langu, pia amenipokea mimi, na ikiwa mtu amenipokea, hanipokei mimi tu, lakini pia aliyenituma.”
“Whoever receives one child such as this in my name receives me; and whoever receives me, receives not me, but him who sent me.”
38 Yohana alimwambia, “Mwalimu tulimwona mtu anatoa pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu hatufuati.”
John said to him in response, “Teacher, we saw someone who does not follow us casting out demons in yoʋr name, and we told him to stop because he does not follow us.”
39 Lakini Yesu alisema, “Msimzuie, kwa kuwa hakuna atakayefanya kazi kubwa kwa jina langu na ndipo baadaye aseme neno baya lolote juu yangu.
But Jesus said, “Do not stop him, for no one who does a miracle in my name will be able to speak evil of me soon afterward.
40 Yeyote asiyekuwa kinyume nasi yuko upande wetu.
For whoever is not against you is for you.
41 Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo, kweli nawaambia, hatapoteza thawabu yake.
Truly I say to you, whoever gives you a cup of water to drink in my name, because you belong to Christ, will certainly not lose his reward.
42 Yeyote anayewakosesha hawa wadogo waniaminio mimi, ingekuwa vyema kwake kufungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa baharini.
“If anyone causes one of these little ones who believe in me to stumble, it would be better for him if a millstone were hung around his neck and he were thrown into the sea.
43 Kama mkono wako ukikukosesha ukate. Ni heri kuingia katika uzima bila mkono kuliko kuingia kwenye hukumu ukiwa na mikono yote. Katika moto “usiozimika”. (Geenna g1067)
If yoʋr hand causes yoʋ to stumble, cut it off. It is better for yoʋ to enter life crippled than to have two hands and go into hell, into the unquenchable fire, (Geenna g1067)
44 (Zingatia: Mstari hii, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usiozimika.” haumo katika nakala za kale).
‘where their worm does not die and the fire is not quenched.’
45 Kama mguu wako ukikukosesha, ukate. Ni vyema kwako kuingia uzimani ukiwa kilema, kuliko kutupwa hukumuni na miguu miwili. (Geenna g1067)
And if yoʋr foot causes yoʋ to stumble, cut it off. It is better for yoʋ to enter life lame than to have two feet and be thrown into hell, into the unquenchable fire, (Geenna g1067)
46 (Zingatia: Mstari huu, “Mahali ambapo funza hawafi na moto usioweza kuzimika” haumo kwenye nakala za kale).
‘where their worm does not die and the fire is not quenched.’
47 Kama jicho lako likikukosesha ling'oe. Ni vyema kwako kuingia katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili na kutupwa kuzimu. (Geenna g1067)
And if yoʋr eye causes yoʋ to stumble, tear it out. It is better for yoʋ to enter the kingdom of God with one eye than to have two eyes and be thrown into the fires of hell, (Geenna g1067)
48 Mahali palipo na funza wasiokufa, na moto usiozimika.
‘where their worm does not die and the fire is not quenched.’
49 Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.
For everyone will be salted with fire, and every sacrifice will be seasoned with salt.
50 Chumvi ni nzuri, kama chumvi ikipoteza ladha yake, utaifanyaje iwe na ladha yake tena? Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe, na muwe na amani kwa kila mmoja.”
Salt is good, but if it becomes unsalty, with what shall you season it? Have salt in yourselves, and be at peace with one another.”

< Marko 9 >