< Marko 8 >
1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
About that time there was again an immense crowd, and they found themselves with nothing to eat. So He called His disciples to Him.
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
"My heart yearns over the people," He said; "for this is now the third day they have remained with me, and they have nothing to eat.
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
If I were to send them home hungry, they would faint on the way, some of them having come a great distance."
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
"Where can we possibly get bread here in this remote place to satisfy such a crowd?" answered His disciples.
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
"How many loaves have you?" He asked. "Seven," they said.
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
So He passed the word to the people to sit down on the ground. Then taking the seven loaves He blessed them, and broke them into portions and proceeded to give them to His disciples for them to distribute, and they distributed them to the people.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
They had also a few small fish. He blessed them, and He told His disciples to distribute these also.
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
So the people ate an abundant meal; and what remained over they picked up and carried away--seven hampers of broken pieces.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
The number fed were about 4,000. Then He sent them away,
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
and at once going on board with His disciples He came into the district of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
The Pharisees followed Him and began to dispute with Him, asking Him for a sign in the sky, to make trial of Him.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
Heaving a deep and troubled sigh, He said, "Why do the men of to-day ask for a sign? In solemn truth I tell you that no sign will be given to the men of to-day."
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
So He left them, went on board again, and came away to the other side.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
Now they had forgotten to take bread, nor had they more than a single loaf with them in the boat;
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
and when He admonished them, "See to it, be on your guard against the yeast of the Pharisees and the yeast of Herod,"
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
they explained His words to one another by saying, "We have no bread!"
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
He perceived what they were saying, and He said to them, "What is this discussion of yours about having no bread? Do you not yet see and understand? Are your minds so dull of comprehension?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
You have eyes! can you not see? You have ears! can you not hear? and have you no memory?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
When I broke up the five loaves for the 5,000 men, how many baskets did you carry away full of broken portions?" "Twelve," they said.
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
"And when the seven for the 4,000, how many hampers full of portions did you take away?" "Seven," they answered.
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
"Do you not yet understand?" He said.
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
And they came to Bethsaida. And a blind man was brought to Jesus and they entreated Him to touch him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
So He took the blind man by the arm and brought him out of the village, and spitting into his eyes He put His hands on him and asked him, "Can you see anything?"
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
He looked up and said, "I can see the people: I see them like trees--only walking."
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
Then for the second time He put His hands on the man's eyes, and the man, looking steadily, recovered his sight and saw everything distinctly.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
So He sent him home, and added, "Do not even go into the village."
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
From that place Jesus and His disciples went to the villages belonging to Caesarea Philippi. On the way He began to ask His disciples, "Who do people say that I am?"
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
"John the Baptist," they replied, "but others say Elijah, and others, that it is one of the Prophets."
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
Then He asked them pointedly, "But you yourselves, who do you say that I am?" "You are the Christ," answered Peter.
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
And He strictly forbad them to tell this about Him to any one.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
And now for the first time He told them, "The Son of Man must endure much suffering, and be rejected by the Elders and the High Priests and the Scribes, and be put to death, and after two days rise to life."
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
This He told them plainly; whereupon Peter took Him and began to remonstrate with Him.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
But turning round and seeing His disciples, He rebuked Peter. "Get behind me, Adversary," He said, "for your thoughts are not God's thoughts, but men's."
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
Then calling to Him the crowd and also His disciples, He said to them, "If any one is desirous of following me, let him ignore self and take up his cross, and so be my follower.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
For whoever is bent on securing his life will lose it, but he who loses his life for my sake, and for the sake of the Good News, will secure it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
Why, what does it benefit a man to gain the whole world and forfeit his life?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
For what could a man give to buy back his life?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
Every one, however, who has been ashamed of me and of my teachings in this faithless and sinful age, of him the Son of Man also will be ashamed when He comes in His Father's glory with the holy angels."