< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those days, when there was again a great multitude, and they had nothing to eat, he called unto him his disciples, and saith unto them,
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
I have compassion on the multitude, because they continue with me now three days, and have nothing to eat:
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
and if I send them away fasting to their home, they will faint in the way; and some of them are come from far.
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
And his disciples answered him, Whence shall one be able to fill these men with bread here in a desert place?
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
And he asked them, How many loaves have ye? And they said, Seven.
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
And he commandeth the multitude to sit down on the ground: and he took the seven loaves, and having given thanks, he brake, and gave to his disciples, to set before them; and they set them before the multitude.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
And they had a few small fishes: and having blessed them, he commanded to set these also before them.
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
And they did eat, and were filled: and they took up, of broken pieces that remained over, seven baskets.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
And they were about four thousand: and he sent them away.
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
And straightway he entered into the boat with his disciples, and came into the parts of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
And the Pharisees came forth, and began to question with him, seeking of him a sign from heaven, tempting him.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
And he sighed deeply in his spirit, and saith, Why doth this generation seek a sign? verily I say unto you, There shall no sign be given unto this generation.
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
And he left them, and again entering into [the boat] departed to the other side.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
And they forgot to take bread; and they had not in the boat with them more than one loaf.
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
And he charged them, saying, Take heed, beware of the leaven of the Pharisees and the leaven of Herod.
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
And they reasoned one with another, saying, We have no bread.
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
And Jesus perceiving it saith unto them, Why reason ye, because ye have no bread? do ye not yet perceive, neither understand? have ye your heart hardened?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
Having eyes, see ye not? and having ears, hear ye not? and do ye not remember?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
When I brake the five loaves among the five thousand, how many baskets full of broken pieces took ye up? They say unto him, Twelve.
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
And when the seven among the four thousand, how many basketfuls of broken pieces took ye up? And they say unto him, Seven.
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
And he said unto them, Do ye not yet understand?
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
And they come unto Bethsaida. And they bring to him a blind man, and beseech him to touch him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
And he took hold of the blind man by the hand, and brought him out of the village; and when he had spit on his eyes, and laid his hands upon him, he asked him, Seest thou aught?
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
And he looked up, and said, I see men; for I behold [them] as trees, walking.
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
Then again he laid his hands upon his eyes; and he looked stedfastly, and was restored, and saw all things clearly.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
And he sent him away to his home, saying, Do not even enter into the village.
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
And Jesus went forth, and his disciples, into the villages of Caesarea Philippi: and in the way he asked his disciples, saying unto them, Who do men say that I am?
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
And they told him, saying, John the Baptist: and others, Elijah; but others, One of the prophets.
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
And he asked them, But who say ye that I am? Peter answereth and saith unto him, Thou art the Christ.
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
And he charged them that they should tell no man of him.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
And he began to teach them, that the Son of man must suffer many things, and be rejected by the elders, and the chief priests, and the scribes, and be killed, and after three days rise again.
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
And he spake the saying openly. And Peter took him, and began to rebuke him.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
But he turning about, and seeing his disciples, rebuked Peter, and saith, Get thee behind me, Satan: for thou mindest not the things of God, but the things of men.
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
And he called unto him the multitude with his disciples, and said unto them, If any man would come after me, let him deny himself, and take up his cross, and follow me.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
For whosoever would save his life shall lose it; and whosoever shall lose his life for my sake and the gospel’s shall save it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
For what doth it profit a man, to gain the whole world, and forfeit his life?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
For what should a man give in exchange for his life?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
For whosoever shall be ashamed of me and of my words in this adulterous and sinful generation, the Son of man also shall be ashamed of him, when he cometh in the glory of his Father with the holy angels.

< Marko 8 >