< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those days, when there was a large crowd, and they had nothing to eat, he called the disciples to himself, and said to them,
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
"I have compassion on the crowd, because they have stayed with me now three days, and have nothing to eat.
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
If I send them away fasting to their home, they will faint on the way, and some of them have come a long way."
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
His disciples answered him, "From where could one satisfy these people with bread here in a deserted place?"
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
He asked them, "How many loaves do you have?" They said, "Seven."
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
He commanded the crowd to sit down on the ground, and he took the seven loaves. Having given thanks, he broke them, and gave them to his disciples to serve, and they served the crowd.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
They had a few small fish. Having blessed them, he said to serve these also.
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
They ate, and were filled. They took up seven baskets of broken pieces that were left over.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
Now they were about four thousand. Then he sent them away.
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
Immediately he entered into the boat with his disciples, and came into the region of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
The Pharisees came out and began to question him, seeking from him a sign from heaven, and testing him.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
He sighed deeply in his spirit, and said, "Why does this generation seek a sign? Truly I tell you, no sign will be given to this generation."
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
And he left them, and got into the boat again, and went to the other side.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
Now they forgot to take bread; and they did not have more than one loaf in the boat with them.
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
He warned them, saying, "Watch out; guard yourselves against the yeast of the Pharisees and the yeast of Herod."
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
And they began discussing among themselves that they had no bread.
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
He, perceiving it, said to them, "Why do you reason that it's because you have no bread? Do you not perceive yet, neither understand? Are your hearts hardened?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
Having eyes, do you not see? Having ears, do you not hear? Do you not remember?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
When I broke the five loaves among the five thousand, how many baskets full of broken pieces did you take up?" They told him, "Twelve."
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
"When the seven loaves fed the four thousand, how many baskets full of broken pieces did you take up?" And they said, "Seven."
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
He asked them, "Do you not yet understand?"
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
He came to Bethsaida. They brought a blind man to him, and begged Jesus to touch him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
He took hold of the blind man by the hand, and brought him out of the village. When he had spit on his eyes, and laid his hands on him, he asked him if he saw anything.
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
He looked up, and said, "I see people; they look like trees walking."
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
Then again he laid his hands on his eyes. He made him look up, and was restored, and saw everything clearly.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
He sent him away to his house, saying, "Do not enter into the village."
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
Jesus went out, with his disciples, into the villages of Caesarea Philippi. On the way he asked his disciples, "Who do people say that I am?"
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
And they said to him, saying, "John the Baptist, and others say Elijah, but others: one of the prophets."
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
He said to them, "But who do you say that I am?" Peter answered and said to him, "You are the Christ."
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
He commanded them that they should tell no one about him.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
He began to teach them that the Son of Man must suffer many things, and be rejected by the elders, the chief priests, and the scribes, and be killed, and after three days rise again.
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
He spoke to them openly. Peter took him, and began to rebuke him.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
But he, turning around, and seeing his disciples, rebuked Peter, and said, "Get behind me, Satan. For you have in mind not the things of God, but the things of humans."
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
He called the crowd to himself with his disciples, and said to them, "If anyone wants to come after me, let him deny himself, and take up his cross, and follow me.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
For whoever wants to save his life will lose it; and whoever will lose his life for my sake and the sake of the Good News will save it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
For what does it profit a person to gain the whole world, and forfeit his soul?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
Or what will a person give in exchange for his soul?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
For whoever will be ashamed of me and of my words in this adulterous and sinful generation, the Son of Man also will be ashamed of him, when he comes in the glory of his Father with the holy angels."

< Marko 8 >