< Marko 8 >
1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those dayes, when there was a very great multitude, and had nothing to eate, Iesus called his disciples to him, and said vnto them,
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
I haue compassion on the multitude, because they haue nowe continued with mee three dayes, and haue nothing to eate.
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
And if I sende them away fasting to their owne houses, they woulde faint by the way: for some of them came from farre.
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
Then his disciples answered him, Whence can a man satisfie these with bread here in the wildernes?
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
And hee asked them, Howe many loaues haue ye? And they said, Seuen.
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
Then he commanded the multitude to sit downe on the grounde: and hee tooke the seuen loaues, and gaue thankes, brake them, and gaue to his disciples to set before them, and they did set them before the people.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
They had also a few small fishes: and when he had giuen thankes, he commanded them also to be set before them.
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
So they did eate, and were sufficed, and they tooke vp of the broken meate that was left, seuen baskets full.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
(And they that had eaten, were about foure thousand) so he sent them away.
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
And anon he entred into a ship with his disciples, and came into the parts of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
And the Pharises came foorth, and began to dispute with him, seeking of him a signe from heauen, and tempting him.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
Then hee sighed deepely in his spirit, and saide, Why doeth this generation seeke a signe? Verely I say vnto you, a signe shall not be giuen vnto this generation.
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
So he left them, and went into the ship againe, and departed to the other side.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
And they had forgotten to take bread, neither had they in the shippe with them, but one loafe.
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
And he charged them, saying, Take heede, and beware of the leauen of the Pharises, and of the leauen of Herod.
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
And they reasoned among themselues, saying, It is, because we haue no bread.
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
And when Iesus knew it, he said vnto them, Why reason you thus, because ye haue no bread? perceiue ye not yet, neither vnderstande? haue ye your hearts yet hardened?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
Haue yee eyes, and see not? and haue yee eares, and heare not? and doe ye not remember?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
When I brake the fiue loaues among fiue thousand, how many baskets full of broken meate tooke ye vp? They said vnto him, Twelue.
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
And when I brake seuen among foure thousande, howe many baskets of the leauings of broken meate tooke ye vp? And they said, Seuen.
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
Then he saide vnto them, Howe is it that ye vnderstand not?
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
And hee came to Bethsaida, and they brought a blinde man vnto him, and desired him to touch him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
Then he tooke the blinde by the hand, and ledde him out of the towne, and spat in his eyes, and put his handes vpon him, and asked him, if he sawe ought.
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
And he looked vp, and said, I see men: for I see them walking like trees.
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
After that, he put his hands againe vpon his eyes, and made him looke againe. And hee was restored to his sight, and sawe euery man a farre off clearely.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
And hee sent him home to his house, saying, Neither goe into the towne, nor tell it to any in the towne.
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
And Iesus went out, and his disciples into the townes of Cesarea Philippi. And by the way hee asked his disciples, saying vnto them, Whome doe men say that I am?
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
And they answered, Some say, Iohn Baptist: and some, Elias: and some, one of the Prophets.
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
And he said vnto them, But whome say ye that I am? Then Peter answered, and saide vnto him, Thou art that Christ.
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
And he sharpely charged them, that concerning him they should tell no man.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
Then hee began to teache them that the Sonne of man must suffer many things, and should be reproued of the Elders, and of the hie Priestes, and of the Scribes, and be slaine, and within three dayes rise againe.
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
And he spake that thing boldly. Then Peter tooke him aside, and began to rebuke him.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
Then he turned backe, and looked on his disciples, and rebuked Peter, saying, Get thee behinde me, Satan: for thou vnderstandest not the things that are of God, but the things that are of men.
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
And hee called the people vnto him with his disciples, and saide vnto them, Whosoeuer will follow me, let him forsake himselfe, and take vp his crosse, and follow me.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
For whosoeuer will saue his life, shall lose it: but whosoeuer shall lose his life for my sake and the Gospels, he shall saue it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
For what shall it profite a man, though he should winne the whole world, if he lose his soule?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
Or what exchange shall a man giue for his soule?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
For whosoeuer shall be ashamed of mee, and of my wordes among this adulterous and sinfull generation, of him shall the Sonne of man be ashamed also, when he commeth in the glorie of his Father with the holy Angels.