< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those days the crowd once again became very large, and they had nothing to eat. Jesus called the disciples to Him and said,
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
“I have compassion for this crowd, because they have already been with Me three days and have nothing to eat.
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
If I send them home hungry, they will faint along the way. For some of them have come a great distance.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
His disciples replied, “Where in this desolate place could anyone find enough bread to feed all these people?”
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
“How many loaves do you have?” Jesus asked. “Seven,” they replied.
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
And He instructed the crowd to sit down on the ground. Then He took the seven loaves, gave thanks and broke them, and gave them to His disciples to set before the people. And they distributed them to the crowd.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
They also had a few small fish, and Jesus blessed them and ordered that these be set before them as well.
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
The people ate and were satisfied, and the disciples picked up seven basketfuls of broken pieces that were left over.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
And about four thousand men were present. As soon as Jesus had dismissed the crowd,
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
He got into the boat with His disciples and went to the district of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
Then the Pharisees came and began to argue with Jesus, testing Him by demanding from Him a sign from heaven.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
Jesus sighed deeply in His spirit and said, “Why does this generation demand a sign? Truly I tell you, no sign will be given to this generation.”
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
And He left them, got back into the boat, and crossed to the other side.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
Now the disciples had forgotten to take bread, except for one loaf they had with them in the boat.
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
“Watch out!” He cautioned them. “Beware of the leaven of the Pharisees and of Herod.”
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
So they began to discuss with one another the fact that they had no bread.
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
Aware of their conversation, Jesus asked them, “Why are you debating about having no bread? Do you still not see or understand? Do you have such hard hearts?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
‘Having eyes, do you not see? And having ears, do you not hear?’ And do you not remember?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
When I broke the five loaves for the five thousand, how many basketfuls of broken pieces did you collect?” “Twelve,” they answered.
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
“And when I broke the seven loaves for the four thousand, how many basketfuls of broken pieces did you collect?” “Seven,” they said.
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
Then He asked them, “Do you still not understand?”
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
When they arrived at Bethsaida, some people brought a blind man and begged Jesus to touch him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
So He took the blind man by the hand and led him out of the village. Then He spit on the man’s eyes and placed His hands on him. “Can you see anything?” He asked.
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
The man looked up and said, “I can see the people, but they look like trees walking around.”
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
Once again Jesus placed His hands on the man’s eyes, and when he opened them his sight was restored, and he could see everything clearly.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
Jesus sent him home and said, “Do not go back into the village.”
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
Then Jesus and His disciples went on to the villages around Caesarea Philippi. On the way, He questioned His disciples: “Who do people say I am?”
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
They replied, “Some say John the Baptist; others say Elijah; and still others, one of the prophets.”
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
“But what about you?” Jesus asked. “Who do you say I am?” Peter answered, “You are the Christ.”
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
And Jesus warned them not to tell anyone about Him.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
Then He began to teach them that the Son of Man must suffer many things and be rejected by the elders, chief priests, and scribes, and that He must be killed and after three days rise again.
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
He spoke this message quite frankly, and Peter took Him aside and began to rebuke Him.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
But Jesus, turning and looking at His disciples, rebuked Peter and said, “Get behind Me, Satan! For you do not have in mind the things of God, but the things of men.”
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
Then Jesus called the crowd to Him along with His disciples, and He told them, “If anyone wants to come after Me, he must deny himself and take up his cross and follow Me.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
For whoever wants to save his life will lose it, but whoever loses his life for My sake and for the gospel will save it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
What does it profit a man to gain the whole world, yet forfeit his soul?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
Or what can a man give in exchange for his soul?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
If anyone is ashamed of Me and My words in this adulterous and sinful generation, the Son of Man will also be ashamed of him when He comes in His Father’s glory with the holy angels.”

< Marko 8 >