< Marko 7 >

1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
Kui siis variserid ja mõned Jeruusalemmast tulnud kirjatundjad kogunesid Jeesuse juurde,
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
märkasid nad mõnda tema jüngritest pühitsemata, see tähendab pesemata kätega söömas.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
(Variserid, nagu kõik juudid, söövad ju alles pärast seda, kui on peotäie veega käsi pesnud, pidades nõnda kinni esivanemate pärimusest.
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
Nad ei söö ka midagi turult toodut enne, kui on seda veega pesnud, ja nad peavad kinni veel mitmetest muudest tavadest: karikate, kannude ja vaskkatelde pesemisest.)
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
Nüüd variserid ja kirjatundjad küsisid Jeesuselt: „Miks sinu jüngrid ei toimi esivanemate pärimuse järgi, vaid söövad leiba pühitsemata kätega?“
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
Jeesus vastas: „Jesajal oli õigus, kui ta teie, silmakirjatsejate, kohta ennustas; nõnda nagu on kirjutatud: „See rahvas austab mind oma huultega, nende süda on aga minust kaugel.
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
Ilmaaegu nad teenivad mind, õpetades õpetusi, mis on vaid inimeste reeglid.“
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
Te jätate kõrvale Jumala käsud ja järgite inimeste kombeid.“
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
Ja ta jätkas: „Kui osavalt te heidate Jumala käsud kõrvale, et järgida oma pärimust!
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
Mooses ütles ju: „Austa oma isa ja ema!“ning „Kes oma isa või ema neab, peab surema.“
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
Kuid teie ütlete, et kui keegi kuulutab oma isale või emale: „Mis toetust sa iganes minu käest saad, on korban“(see tähendab templile pühendatud ohvriandi),
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
ei lase teie neil enam midagi oma isa või ema heaks teha.
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
Te teete Jumala sõna tühjaks oma pärimuse kaudu, mille te olete pärinud. Ja te teete veel palju muudki niisugust!“
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
Ja kui Jeesus oli taas rahva enda juurde kutsunud, ütles ta neile: „Kuulge mind kõik ja mõistke!
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
Miski, mis läheb väljastpoolt inimest tema sisse, ei või teda rüvetada; aga mis läheb inimesest välja, see rüvetab inimest.
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
Kellel kõrvad on, see kuulgu!“
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
Kui Jeesus läks rahva juurest ära ühte majja, küsisid jüngrid temalt selle tähendamissõna mõtet.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
Jeesus ütles neile: „Kas teiegi olete taipamatud? Kas te ei saa aru, et miski väljast inimesse tulev ei saa teda rüvetada,
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
sest see ei lähe tema südamesse, vaid kõhtu, ja heidetakse jälle välja?“Sel viisil kuulutas Jeesus puhtaks kõik toidud.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
Aga ta ütles veel: „Mis inimesest välja tuleb, see rüvetab teda.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
Sest seest, inimese südamest, lähtuvad kurjad mõtted, kõlvatu suguelu, vargused, mõrvad,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
abielurikkumine, ahnus, kurjus, kavalus, nilbus, kadedus, laim, ülbus, rumalus.
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
Kõik need pahed tulevad seestpoolt ja rüvetavad inimest.“
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
Ja Jeesus läks sealt Tüürose alale. Ta astus sisse ühte majja, soovides, et keegi sellest teada ei saaks, kuid ta ei saanud jääda märkamatuks.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
Temast kuulis keegi naine, kelle väikest tütart vaevas rüve vaim, ja ta tuli otsekohe ning langes Jeesuse jalge ette.
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
Ta oli kreeklanna, pärit Sürofoiniikiast. Naine palus Jeesust, et ta ajaks kurja vaimu tema tütrest välja.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
Kuid Jeesus ütles talle: „Lase esmalt lastel saada söönuks! Ei sobi võtta laste leiba ja visata see koertele!“
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
Naine aga vastas: „Jah, Issand, aga koerad söövad ju laua all laste raasukesi!“
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
„Kui sa nii ütled, siis mine!“ütles Jeesus. „Kuri vaim on sinu tütrest välja läinud!“
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
Ja naine läks koju ning leidis lapse voodis magamas. Kuri vaim oli temast lahkunud.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
Jeesus lahkus Tüürose alalt ja tuli Siidoni kaudu Galilea mere äärde Dekapolise aladele.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
Tema juurde toodi kurt, kes vaevu rääkida suutis, ning paluti, et ta paneks oma käe tema peale.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
Jeesus viis mehe rahvahulgast eemale, pistis oma sõrmed ta kõrvadesse, sülitas ja puudutas ta keelt
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
ning üles taeva poole vaadates õhkas ja ütles talle: „Effataa!“, see tähendab „Mine lahti!“
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
Mehe kõrvad avanesid sedamaid ja ta keel pääses kütkest valla ning ta rääkis korralikult.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
Jeesus ei lubanud neil sellest kellelegi rääkida. Aga mida enam ta neid keelas, seda enam nad jutustasid.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
Ning kuulajad ütlesid suures hämmastuses: „Kõik on ta teinud hästi! Ta paneb isegi kurdid kuulma ja keeletud rääkima!“

< Marko 7 >