< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
And gathered together unto him are the Pharisees, and certain of the scribes, having come from Jerusalem,
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
and having seen certain of his disciples with defiled hands — that is, unwashed — eating bread, they found fault;
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
for the Pharisees, and all the Jews, if they do not wash the hands to the wrist, do not eat, holding the tradition of the elders,
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
and, [coming] from the market-place, if they do not baptize themselves, they do not eat; and many other things there are that they received to hold, baptisms of cups, and pots, and brazen vessels, and couches.
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
Then question him do the Pharisees and the scribes, 'Wherefore do thy disciples not walk according to the tradition of the elders, but with unwashed hands do eat the bread?'
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
and he answering said to them — 'Well did Isaiah prophesy concerning you, hypocrites, as it hath been written, This people with the lips doth honour Me, and their heart is far from Me;
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
and in vain do they worship Me, teaching teachings, commands of men;
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
for, having put away the command of God, ye hold the tradition of men, baptisms of pots and cups; and many other such like things ye do.'
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
And he said to them, 'Well do ye put away the command of God that your tradition ye may keep;
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
for Moses said, Honour thy father and thy mother; and, He who is speaking evil of father or mother — let him die the death;
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
and ye say, If a man may say to father or to mother, Korban (that is, a gift), [is] whatever thou mayest be profited out of mine,
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
and no more do ye suffer him to do anything for his father or for his mother,
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
setting aside the word of God for your tradition that ye delivered; and many such like things ye do.'
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
And having called near all the multitude, he said to them, 'Hearken to me, ye all, and understand;
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
there is nothing from without the man entering into him that is able to defile him, but the things coming out from him, those are the things defiling the man.
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
If any hath ears to hear — let him hear.'
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
And when he entered into a house from the multitude, his disciples were questioning him about the simile,
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
and he saith to them, 'So also ye are without understanding! Do ye not perceive that nothing from without entering into the man is able to defile him?
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
because it doth not enter into his heart, but into the belly, and into the drain it doth go out, purifying all the meats.'
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
And he said — 'That which is coming out from the man, that doth defile the man;
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
for from within, out of the heart of men, the evil reasonings do come forth, adulteries, whoredoms, murders,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
thefts, covetous desires, wickedness, deceit, arrogance, an evil eye, evil speaking, pride, foolishness;
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
all these evils do come forth from within, and they defile the man.'
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
And from thence having risen, he went away to the borders of Tyre and Sidon, and having entered into the house, he wished none to know, and he was not able to be hid,
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
for a woman having heard about him, whose little daughter had an unclean spirit, having come, fell at his feet, —
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
and the woman was a Greek, a Syro-Phenician by nation — and was asking him, that the demon he may cast forth out of her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
And Jesus said to her, 'Suffer first the children to be filled, for it is not good to take the children's bread, and to cast [it] to the little dogs.'
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
And she answered and saith to him, 'Yes, sir; for the little dogs also under the table do eat of the children's crumbs.'
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
And he said to her, 'Because of this word go; the demon hath gone forth out of thy daughter;'
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
and having come away to her house, she found the demon gone forth, and the daughter laid upon the couch.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
And again, having gone forth from the coasts of Tyre and Sidon, he came unto the sea of Galilee, through the midst of the coasts of Decapolis,
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
and they bring to him a deaf, stuttering man, and they call on him that he may put the hand on him.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
And having taken him away from the multitude by himself, he put his fingers to his ears, and having spit, he touched his tongue,
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
and having looked to the heaven, he sighed, and saith to him, 'Ephphatha,' that is, 'Be thou opened;'
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
and immediately were his ears opened, and the string of his tongue was loosed, and he was speaking plain.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
And he charged them that they may tell no one, but the more he was charging them, the more abundantly they were proclaiming [it],
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
and they were being beyond measure astonished, saying, 'Well hath he done all things; both the deaf he doth make to hear, and the dumb to speak.'