< Marko 7 >

1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
Then the Pharisees, with certain Scribes who had come from Jerusalem, came to Him in a body.
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
They had noticed that some of His disciples were eating their food with 'unclean' (that is to say, unwashed) hands.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
(For the Pharisees and all the Jews--being, as they are, zealous for the traditions of the Elders--never eat without first carefully washing their hands,
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
and when they come from market they will not eat without bathing first; and they have a good many other customs which they have received traditionally and cling to, such as the rinsing of cups and pots and of bronze utensils, and the washing of beds.)
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
So the Pharisees and Scribes put the question to Him: "Why do your disciples transgress the traditions of the Elders, and eat their food with unclean hands?"
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
"Rightly did Isaiah prophesy of you hypocrites," He replied; "as it is written, "'This People honour Me with their lips, while their hearts are far away from Me:
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
But idle is their devotion while they lay down precepts which are mere human rules.'
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
"You neglect God's Commandment: you hold fast to men's traditions."
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
"Praiseworthy indeed!" He added, "to set at nought God's Commandment in order to observe your own traditions!
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
For Moses said, 'Honour thy father and thy mother' and again, 'He who curses father or mother, let him die the death.'
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
But you say, 'If a man says to his father or mother, It is a Korban (that is, a thing devoted to God), whatever it is, which otherwise you would have received from me--'
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
And so you no longer allow him to do anything for his father or mother,
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
thus nullifying God's precept by your tradition which you have handed down. And many things of that kind you do."
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
Then Jesus called the people to Him again. "Listen to me, all of you," He said, "and understand.
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
There is nothing outside a man which entering him can make him unclean; but it is the things which come out of a man that make him unclean."
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
After He had left the crowd and gone indoors, His disciples began to ask Him about this figure of speech.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
"Have you also so little understanding?" He replied; "do you not understand that anything whatever that enters a man from outside cannot make him unclean,
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
because it does not go into his heart, but into his stomach, and passes away ejected from him?" By these words Jesus pronounced all kinds of food clean.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
"What comes out of a man," He added, "that it is which makes him unclean.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
For from within, out of men's hearts, their evil purposes proceed--fornication, theft, murder, adultery,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
covetousness, wickedness, deceit, licentiousness, envy, reviling, pride, reckless folly:
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
all these wicked things come out from within and make a man unclean."
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
Then He rose and left that place and went into the neighbourhood of Tyre and Sidon. Here He entered a house and wished no one to know it, but He could not escape observation.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
Forthwith a woman whose little daughter was possessed by a foul spirit heard of Him, and came and flung herself at His feet.
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
She was a Gentile woman, a Syro-phoenician by nation: and again and again she begged Him to expel the demon from her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
"Let the children first eat all they want," He said; "it is not right to take the children's bread and throw it to the dogs."
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
"True, Sir," she replied, "and yet the dogs under the table eat the children's scraps."
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
"For those words of yours, go home," He replied; "the demon has gone out of your daughter."
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
So she went home, and found the child lying on the bed, and the demon gone.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
Returning from the neighbourhood of Tyre, He came by way of Sidon to the Lake of Galilee, passing through the district of the Ten Towns.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
Here they brought to Him a deaf man that stammered, on whom they begged Him to lay His hands.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
So Jesus taking him aside, apart from the crowd, put His fingers into his ears, and spat, and moistened his tongue;
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
and looking up to Heaven He sighed, and said to him, "Ephphatha!" (that is, "Open!")
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
And the man's ears were opened, and his tongue became untied, and he began to speak perfectly.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
Then Jesus charged them to tell no one; but the more He charged them, all the more did they spread the news far and wide.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
The amazement was extreme. "He succeeds in everything he attempts," they exclaimed; "he even makes deaf men hear and dumb men speak!"

< Marko 7 >