< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
[One day some] Pharisees and some men who teach the [Jewish] laws gathered around Jesus. They had come from Jerusalem [to investigate him].
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
The Pharisees and all of the [other] Jews [strictly] observe the traditions that their ancestors [taught. For example, they refuse to] eat until they first wash their hands [with a special ritual], especially after they [return] from [buying things in] the marketplace. [They think that God will be angry with them if they do not do that, because some person or thing unacceptable to God might have touched] ([them/the things they bought]). There are many other such [traditions] that they accept and try to obey. Specifically, they wash [in a special way] their cups, pots, kettles, containers, and beds [in order that using these things will not make God reject them].
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
That day, those Pharisees and men who taught the [Jewish] laws saw that some of his disciples were eating food with hands that they had not washed [using the special ritual]. So they questioned Jesus, saying, “[Your] disciples disobey the traditions of our ancestors! (You should not [let them] eat food if they have not washed their hands [using our special ritual]!/Why do you [let them] eat food if they have not washed their hands [using our special ritual]?) [RHQ]”
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
Jesus said to them, “Isaiah [rebuked your ancestors], and his words describe very well you people who only pretend to be good! He wrote these words [that God said]: These people speak [as if they] honor me, but they [SYN] really do not think about honoring me at all.
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
It is useless for them to worship me, because they teach only what people have commanded [as if I myself had commanded them].
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
You, [like your ancestors], refuse [to do] what God has commanded. Instead, you follow only the traditions that (others/your ancestors) have [taught].”
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
Jesus also said to them, “[You think] [IRO] that you are clever in refusing to do what God commanded just so that you can obey your own traditions!
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
[For example, our ancestor] Moses [wrote God’s] command, ‘Honor your fathers and your mothers’. He also wrote, ‘[The authorities must] execute a person who speaks evil about his father or mother.’
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
But you [teach people that it is all right that people no longer must help their parents. You teach people that it is all right if people] give their things to God [instead of giving them to their parents]. You allow them to say to their parents, ‘What I was going to give to you [to provide for you, I have now promised to] give to God. So I [cannot any longer help you]!’ As a result, you are [actually telling people] that they no longer have to help their parents!
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
And, by doing that, you disregard what God commanded! You teach your own traditions to others [and tell them strongly that they should obey them] And you do many other things like that.”
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
Then Jesus again summoned the crowd [to come closer. Then] he said to them [figuratively], “All of you people listen to me! [Try to] understand [DOU] [what I am about to tell you].
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
Nothing that people eat causes [God to] consider them to be unacceptable. On the contrary, it is that which comes from people’s (inner beings/hearts) that causes God to reject them.”
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
After Jesus had left the crowd and then entered a house with the disciples, they asked him about the parable [that he had just spoken].
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
He replied, “([I am disappointed that] you also do not understand [what it means]!/Why can you not understand [what it means]?) [RHQ] (You ought to understand that nothing that [enters us from] outside can cause [God to] consider us unacceptable to him./Can you not understand that nothing that [enters us from] outside of us can cause [God to] consider us unacceptable to him?) [RHQ]
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
Instead of entering [and ruining] our minds/souls, it goes into our stomachs, and afterwards the refuse passes out [of our bodies].” By saying this, Jesus was declaring that people [can eat] any food without causing [God] to reject them.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
He also said, “It is the [thoughts and actions] that come from within people that cause [God] to consider them unacceptable to him.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
Specifically, it is people’s innermost being [that causes them to] think things that are evil; they act immorally, they steal [things], they commit murder.
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
They [commit] adultery, they are greedy, they [act] maliciously, they deceive [people]. They [act] indecently, they envy [people], they speak evil about others, they are proud, and they [act] foolishly.
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
People think [these thoughts] and then they do these evil actions, and that is what causes [God to] consider them unacceptable to him.”
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
After Jesus [and his disciples] left [Galilee district], they went to the region around Tyre. While he stayed at a certain house, he desired that no one know [it], but people soon found out [that he was there].
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
A certain woman, whose daughter had an evil spirit [within her], heard about Jesus. At once she came to him and prostrated herself at his feet.
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
This woman [was not a Jew. Her ancestors came] from Greece [country], but she was born in [the region around] Phoenicia [town] in Syria district. She pleaded with Jesus that he expel the evil spirit from her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
But he [wanted to see how strongly she believed in him. So, suggesting that he should help the Jews first and not the non-Jews whom some Jews called dogs] [MET], [he] spoke to her saying, “First let the children eat all they want, because it is not good for someone to take the food [the mother has prepared] for the children and then throw it to the [little] dogs.”
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
But [to show that she believed that non-Jews could also receive help from God] [MET], she replied to him, “Sir, [what you say is] correct, but even the [little] dogs, which lie under the table, eat the crumbs that the children [drop].”
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
[Jesus] said to her, “Because of what you have said, [you have shown me that you believe in what I can do for you]. So I will help you. Now you may go [home, because I have caused] the evil spirit to leave your daughter.”
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
The woman returned to her house and saw that her child was lying [quietly] on the bed and that the evil spirit had left.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
Jesus [and his disciples] left the region around Tyre [city] and went [north] through Sidon [city], then [toward the east] through the district of the Ten Towns, and then [south] to [the towns near] Lake Galilee.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
[There], people brought to him a man who was deaf and who could hardly talk. They begged [Jesus] to lay his hands on him [in order to heal him].
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
[So Jesus] took him away from the crowd [in order that the two of them could be] alone. Then he put [one of] his fingers into [each of] the man’s ears. After he spat [on his fingers], he touched the man’s tongue [with his fingers].
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
Then he looked up toward heaven, he sighed [because he was concerned for the man], and then [in his own language] he said to the man’s [ears], “Ephphatha”, which means, “Be opened {Open up}!”.
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
At once the man could hear plainly [MTY]. He also began to speak clearly because [what was causing him to be unable to speak] was healed {Jesus healed [what was causing him to be unable to speak]}.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
Jesus told ([the people/his friends]) not to tell anyone [what he had done]. But, although he ordered them [and others] repeatedly [not to tell anyone about it], they kept talking about it very much.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
[People who heard about it] were utterly amazed and were saying [enthusiastically], “Everything he has done is wonderful! [Besides doing other amazing things], he enables deaf people to hear! And he enables those who cannot speak to speak!”