< Marko 7 >

1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
And there gathered about him Pharisees and Scribes, who had come from Jerusalem.
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
And they saw some of his disciples eating bread, with their hands unwashed; and they censured it.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
For all the Jews and the Pharisees, unless they carefully wash their hands do not eat; because they hold fast the tradition of the Elders.
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
And coming from the market-place, except they baptize, they do not eat. And there are many other things which they have received to observe, such as the baptisms of cups, and of pots, and of brazen vessels, and of couches.
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
And the Scribes and Pharisees asked him: Why walk not thy disciples according to the tradition of the Elders, but eat bread with their hands unwashed?
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
And he said to them: Well did Isaiah the prophet prophecy concerning you, ye hypocrites; as it is written: This people honoreth me with its lips, but their heart is very far from me.
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
And in vain do they give me reverence, while teaching as doctrines the precepts of men.
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
For ye have forsaken the commandment of God, and hold fast the tradition of men, the baptisms of cups, and of pots, and many things like these.
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
He said also to them: Full well do ye spurn the precept of God, that ye may establish your tradition!
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
For Moses said: Honor thy father and thy mother; and whoever shall revile his father or his mother, shall surely die.
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
But ye say: If a man say to his father or to his mother, Be it my oblation, whatever thou mayest gain from me:
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
then ye suffer him not to do any thing for his father or his mother.
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
And ye reject the word of God, on account of the tradition which ye hand down. And many things like these, ye do.
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
And Jesus called all the multitude, and said to them: Hear, all ye; and understand.
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
There is nothing without a man which, by entering him, can pollute him. But that which cometh out of him, that it is that polluteth a man.
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
Whoever hath ears to hear, let him hear.
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
And when Jesus had entered the house, apart from the multitude, his disciples asked him about this similitude.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
And he said to them: Are ye likewise so undiscerning? Do ye not know, that whatever from without entereth into a man, cannot defile him?
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
For it doth not enter into his heart, but into his belly, and is thrown into the digestive process, which carries off all that is eaten.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
But that which proceedeth from a man, that defileth a man.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
For from within, from the heart of men, proceed evil thoughts, adultery, whoredom,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
theft, murder, avarice, malice, deceit, lasciviousness, an evil eye, reviling, haughtiness, folly.
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
All these evil things come from within, and defile a man.
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
Thence Jesus arose, and went to the border of Tyre and Sidon. And he entered a house, and wished no man to know him; but he could not be concealed.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
For immediately a woman, whose daughter had an unclean spirit, heard of him; and she came, and fell before his feet,
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
(the woman was a Gentile from Phenicia of Syria), and besought him, that he would expel the demon from her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
Jesus said to her: Permit the children first to be satisfied; for it is not becoming, to take the children's bread and cast it to dogs.
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
And she replied, and said to him: Yes, my Lord: and yet the dogs under the table eat the children's crumbs.
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
Jesus said to her: Go thou; because of this speech, the demon hath departed from thy daughter.
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
And she went to her house, and found her daughter lying on a bed, and the demon gone from her.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
Again Jesus departed from the border of Tyre and Sidon, and came to the sea of Galilee, to the border of Decapolis.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
And they brought to him a deaf and stammering man, and besought him to lay his hand on him.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
And he led him aside from the multitude, and put his fingers into his ears, and spit, and touched his tongue,
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
and looked towards heaven, and sighed, and said to him: Be opened.
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
And immediately his ears were opened, and the bond of his tongue was loosed, and he spake plainly.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
And he charged them to tell no man of it: and the more he charged them, the more they proclaimed it.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
And they admired exceedingly, and said: He doeth every thing excellently: he maketh the deaf to hear, and the speechless to talk.

< Marko 7 >