< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
And there are gathered together unto him the Pharisees, and certain of the scribes, which had come from Jerusalem,
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
and had seen that some of his disciples ate their bread with defiled, that is, unwashen, hands.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
For the Pharisees, and all the Jews, except they wash their hands diligently, eat not, holding the tradition of the elders:
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
and [when they come] from the marketplace, except they wash themselves, they eat not: and many other things there be, which they have received to hold, washings of cups, and pots, and brasen vessels.
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
And the Pharisees and the scribes ask him, Why walk not thy disciples according to the tradition of the elders, but eat their bread with defiled hands?
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
And he said unto them, Well did Isaiah prophesy of you hypocrites, as it is written, This people honoureth me with their lips, But their heart is far from me.
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
But in vain do they worship me, Teaching [as their] doctrines the precepts of men.
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
Ye leave the commandment of God, and hold fast the tradition of men.
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
And he said unto them, Full well do ye reject the commandment of God, that ye may keep your tradition.
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
For Moses said, Honour thy father and thy mother; and, He that speaketh evil of father or mother, let him die the death:
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
but ye say, If a man shall say to his father or his mother, That wherewith thou mightest have been profited by me is Corban, that is to say, Given [to God];
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
ye no longer suffer him to do aught for his father or his mother;
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
making void the word of God by your tradition, which ye have delivered: and many such like things ye do.
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
And he called to him the multitude again, and said unto them, Hear me all of you, and understand:
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
there is nothing from without the man, that going into him can defile him: but the things which proceed out of the man are those that defile the man.
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
And when he was entered into the house from the multitude, his disciples asked of him the parable.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
And he saith unto them, Are ye so without understanding also? Perceive ye not, that whatsoever from without goeth into the man, [it] cannot defile him;
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
because it goeth not into his heart, but into his belly, and goeth out into the draught? [This he said], making all meats clean.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
And he said, That which proceedeth out of the man, that defileth the man.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
For from within, out of the heart of men, evil thoughts proceed, fornications, thefts, murders, adulteries,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
covetings, wickednesses, deceit, lasciviousness, an evil eye, railing, pride, foolishness:
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
all these evil things proceed from within, and defile the man.
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
And from thence he arose, and went away into the borders of Tyre and Sidon. And he entered into a house, and would have no man know it: and he could not be hid.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
But straightway a woman, whose little daughter had an unclean spirit, having heard of him, came and fell down at his feet.
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
Now the woman was a Greek, a Syrophoenician by race. And she besought him that he would cast forth the devil out of her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
And he said unto her, Let the children first be filled: for it is not meet to take the children’s bread and cast it to the dogs.
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
But she answered and saith unto him, Yea, Lord: even the dogs under the table eat of the children’s crumbs.
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
And he said unto her, For this saying go thy way; the devil is gone out of thy daughter.
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
And she went away unto her house, and found the child laid upon the bed, and the devil gone out.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
And again he went out from the borders of Tyre, and came through Sidon unto the sea of Galilee, through the midst of the borders of Decapolis.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
And they bring unto him one that was deaf, and had an impediment in his speech; and they beseech him to lay his hand upon him.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
And he took him aside from the multitude privately, and put his fingers into his ears, and he spat, and touched his tongue;
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
and looking up to heaven, he sighed, and saith unto him, Ephphatha, that is, Be opened.
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
And his ears were opened, and the bond of his tongue was loosed, and he spake plain.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
And he charged them that they should tell no man: but the more he charged them, so much the more a great deal they published it.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
And they were beyond measure astonished, saying, He hath done all things well: he maketh even the deaf to hear, and the dumb to speak.