< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
One day the Pharisees came to him in a body with some Scribes who had come from Jerusalem.
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
They had noticed that some of his disciples were eating with "common," that is to say, unwashed hands.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
For the Pharisees and all of the Jews do not eat until they have ceremoniously washed their hands in obedience to the tradition of the elders;
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
and when they come from the market-place they do not eat without bathing first. and they have many other customs which they have received and observe, such as the washing of cups and jugs and copper pans.
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
So the Pharisees and Scribes asked him. "Why do your disciples not follow the traditions of the elders? Why do they eat with ‘common’ unwashed hands?"
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
"Well did Isaiah prophesy of you, hypocrites," he answered. "As it is written, "This people honor me with their lips, While their hearts are far from me;
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
But in vain do they worship me, For their teaching is only human precepts.
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
"You neglect the commandment of God, and hold fast the traditions of men."
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
"It is praiseworthy, is it," he exclaimed, "to reject the command of God that you may keep your tradition!
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
For although Moses said, Honor your father and mother, and Let him who curses father or mother suffer death,
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
you say that if a man tells his father or mother, ‘This money which otherwise you would have received from me, is Korban’ (that is, a thing devoted to God),
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
you exempt him from doing any service for his father or mother.
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
Thus by your tradition which you have handed down you set at naught the word of God; and you do many other things like that."
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
Then again he called the crowd to him and said.
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
"Listen to me, all of you, and understand; there is nothing outside a man which by entering in can defile him; but it is what comes from him that defiled him."
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
After he had left the crowd and gone indoors his disciples began asking him about the parable.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
"Are even you without understanding?" he said. "Do you not perceive that nothing whatever from without can defile a man by entering him,
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
because it does not go into his heart, but into his belly, and passes away, ejected from him?" By these words he pronounced all foods clean.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
"What comes out of a man," he continued, "is what defiles him.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
From within, from the heart of man, proceed evil purposes -
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
fornication, theft, murder, adultery, greed, malice, deceit, wantonness, envy, slander, arrogance, reckless folly -
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
all these wicked things issue from within and defile a man."
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
After he rose and left that place, he went away into the region of Tyre and Sidon. Here he went into a house and wished no one to know it but he could not be hid.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
Forthwith a woman whose little daughter was possessed by an unclean spirit, heard of him, and came and fell at his feet
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
(the woman was a Greek, a Syro-phoenician by race), and again and again she begged him to cast the demon out of her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
"Let the children be filled first," he said to her. "It is unseemly to take the children’s bread and throw it to the dogs."
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
"True, Master," she answered, "but the dogs under the table do pick up the children’s crumbs."
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
"For that saying of yours, go home," he replied; "the demon has departed from your daughter."
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
So she went home, and found the child lying in her bed and the demon departed.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
Again he left the region of Tyre, and passed through Sidon to the Sea of Galilee, crossing the District of the Ten Towns.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
And they brought to him a deaf man who stammered, and begged him to lay his hands upon him.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
So Jesus took him aside from the crowd, by himself, and put his finger in the man’s ears, and moistened his tongue with saliva;
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
then looking up to heaven with a sigh, he said to him, "Ephphatha!" (that is, "Be opened.")
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
And his ears were opened and the bond of his tongue was loosened, and he spoke plainly.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
Then Jesus charged them not to tell any one, but the more he charged them, the more they published it;
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
and people were amazed beyond measure saying. "How successfully he does things! Even the deaf he makes to hear, and the dumb to speak."