< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya waandishi ambao walikuwa wametokea Yerusalemu walikusanyika kumzunguka yeye.
And the Pharisees and certain ones of the scribes, having come from Jerusalem, gather to Him.
2 Na waliona kuwa baadhi ya wanafunzi wake walikula mkate kwa mikono najisi; ambayo haikuoshwa.
And seeing certain ones of His disciples eating bread with defiled, that is, unwashed hands.
3 (kwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali mpaka wameosha mikono yao vizuri; wanashikilia utamaduni wa wazee. Wakati
For the Pharisees and all the Jews, unless they diligently wash their hands, do not eat, holding the tradition of the elders.
4 Mafarisayo wanaporudi kutoka mahali pa soko, hawali mpaka wameoga kwanza. Na kuna sheria zingine ambazo wanazifuata kabisa, ikiwa ni pamoja na kuosha vikombe, masufuria, vyombo vya shaba, na hata viti vinavyotumika wakati wa chakula.)
And from the forum, unless they may baptize themselves, they do not eat: and many other things which they have received to hold, the baptism of cups, and pots, and brazen vessels, and couches.
5 Mafarisayo na waandishi walimuuliza Yesu, “Kwa nini wanafunzi wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mkate pasipo kunawa mikono?”
Then the Pharisees and scribes asked Him, Wherefore do not thy disciples walk according to the tradition of the elders: but they eat bread with unwashed hands?
6 Lakini yeye aliwaambia, “Isaya alitabiri vizuri kuhusu ninyi wanafiki, aliandika, 'Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali na mimi.
And responding He said to them, Beautifully did Isaiah prophesy concerning you hypocrites, as has been written, This people honor me with lips, but their heart is far from me.
7 Wananifanyia ibaada zisizo na maana, wakifundisha sheria za wanadamu kama mapokeo yao.'
In vain do they worship me, teaching for doctrines the commandments of men.
8 Mmeiacha sheria ya Mungu na kushikilia kwa wepesi tamaduni za wanadamu.”
For having left the commandment of God, you are holding the tradition of men.
9 Na akasema kwao, “Mmeikataa amri ya Mungu kwa urahisi ili kwamba mtunze tamaduni zenu!
And He said to them, Truly, you make void the commandment of God, that you may hold your own tradition.
10 Kwa kuwa Musa alisema, 'mheshimu baba yako na mama yako,' na 'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa.'
For Moses said, Honor thy father and thy mother; and let the one speaking evil of father and mother die the death.
11 Lakini mnasema, 'kama mtu akisema kwa baba yake au mama, “Msaada wowote ambao mngepokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu,”' (hiyo ni kusema kwamba, 'imetolewa kwa Mungu')
But you say, If a man may say to father or mother, Corban, that is a gift, whatsoever you may be profited by me;
12 hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake.
and you no longer permit him to do anything for his father or mother;
13 Mnaifanya amri ya Mungu kuwa bure kwa kuleta tamaduni zenu. Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya.”
making void the word of God by your tradition, which you have given: and you do many such similar things.
14 Aliwaita makutano tena na kuwaambia, “Mnisikilize mimi, ninyi nyote, na mnielewe.
And calling the crowd to Him again, He said to them, Hear all ye, and understand.
15 Hakuna chochote kutoka nje ya mtu ambacho chaweza kumchafua mtu kiingiapo kwake. Bali ni kile kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho.
There is nothing without a man coming into him, which is competent to defile him: but those things coming out from him, these are the things which defile the man.
16 (Zingatia: mstari huu, “kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia, na asikie” haumo kwenye nakala za kale).
If any one has ears to hear, let him hear.
17 Yesu alipowaacha makutano na kuingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kuhusu mfano huo.
And when He came from the multitude into the house, His disciples asked Him the parable.
18 Yesu akasema, “Na ninyi pia bado hamjaelewa? Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua,
And He says to them, Are you still without understanding? Do you not know that everything external entering into a man is not able to defile him?
19 kwa sababu hakiwezi kwenda kwenye moyo wake, lakini kinaingia katika tumbo lake na kisha kinapita kwenda chooni.” Kwa maelezo haya Yesu alivifanya vyakula vyote kuwa safi.
Because it does not go into his heart, but into his stomach, and is cast out into the excrement, purifying all edibles.
20 Alisema, “Ni kile ambacho kinamtoka mtu ndicho kimchafuacho.
And He said, Everything proceeding out from the man, that defiles the man.
21 Kwa kuwa hutoka ndani ya mtu, nje ya moyo, hutoka mawazo maovu, zinaa, wizi, mauaji,
For within, out of the heart of men, proceed evil reasonings, adulteries, fornications, murders,
22 uasherati, tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, kujamiiana, wivu, kashfa, majivuno, ujinga.
thefts, covetousness, wickedness, deceit, impurity, an evil eye, blasphemy, pride, folly.
23 Maovu haya yote yanatoka ndani, ndiyo yale yamchafuayo mtu.”
All these evils proceed out from within, and defile the man.
24 Aliamka kutoka pale na kuondoka kwenda katika mkoa wa Tiro na Sidoni. Aliingia ndani na hakutaka mtu yeyote ajue kuwa alikuwa hapo, lakini haikuwezekana kumficha.
And rising up, He departed thence into the regions of Tyre and Sidon. And having entered into a house, and He wished no one to know it: and He was not able to be hidden.
25 Lakini ghafla mwanamke, ambaye mtoto wake mdogo alikuwa na roho mchafu, alisikia habari zake, akaja, na akaanguka miguuni pake.
For a woman hearing concerning Him, whose daughter had an unclean spirit, having come worshiped at His feet.
26 Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki. Alimsihi yeye amfukuze pepo kutoka kwa binti yake.
For the woman was a Greek, a Syrophenician by race; and asked Him that He may cast the demon out of her daughter.
27 Yesu akamwambia mwanamke, “Waache watoto walishwe kwanza, kwa kuwa sio sawa kuuchukua mkate wa watoto na kuwatupia mbwa.”
And He said to her, Permit the children first to be fed: for It is not good to take the children's bread and cast it to little dogs.
28 Lakini mwanamke akamjibu na kusema, “Ndiyo Bwana, hata mbwa chini ya meza hula mabaki ya chakula cha watoto.”
And she responded and says to Him, Yea, Lord: for even the little dogs eat the crumbs of the children under the table.
29 Akamwambia, “Kwa kuwa umesema hivi, uko huru kwenda. Pepo ameshamtoka binti yako.”
And He said to her, On account of this word go; the demon has already gone out from thy daughter.
30 Mwanamke alirudi nyumbani kwake na akamkuta binti yake amelala kitandani, na pepo alikuwa amemtoka.
And having come into her house, she found the demon gone out, and the daughter lying on the bed.
31 Yesu alitoka tena nje ya mkoa wa Tiro na kupitia Sidoni kuelekea Bahari ya Galilaya mpaka kanda ya Dikapolisi.
And having again come out from Tyre and Sidon, He came to the Sea of Galilee, amid the coasts of Decapolis.
32 Na wakamletea mtu aliyekuwa kiziwi na alikuwa hawezi kuzungumza vizuri, walimsihi Yesu aweke mikono juu yake.
And they bring Him a deaf man, speaking with difficulty; and intreat Him that He may lay His hand on him.
33 Alimtoa nje ya kusanyiko kwa siri, na akaweka vidole vyake kwenye masikio yake, na baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake.
And taking him from the crowd privately, He put His fingers in his ears, and having spat, He touched his tongue;
34 Alitazama juu mbinguni, akahema na kumwambia, “Efata,” hiyo ni kusema “funguka!”
and looking up to heaven, he groaned, and says to him, Ephphatha, which is, Be thou opened.
35 Na muda ule ule masikio yakafunguka, na kilichokuwa kimezuia ulimi kiliharibiwa na akaweza kuongea vizuri.
And immediately his ears were opened, and the bond of his tongue loosed, and he continued to speak distinctly.
36 Na aliwaamuru wasimwambie mtu yeyote. Lakini kadri alivyowaamuru, ndivyo walivyotangaza habari hizo kwa wingi.
And He charged them that they should tell no one: and the more He charged them, the more abundantly they proclaimed it.
37 Hakika walishangazwa, na kusema, “Amefanya kila kitu vizuri. Hata amewafanya viziwi kusikia na mabubu kuongea.”
And were astonished exceedingly, saying, He has done all things well: He makes the deaf to hear, and the dumb to speak.