< Marko 6 >

1 Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
Jeesus lahkus ja läks koos oma jüngritega koju Naatsaretti.
2 Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
Hingamispäeval hakkas ta sünagoogis õpetama ja paljud kuulajaist olid üllatunud. „Kust ta need mõtted saab?“küsisid nad. „Mis tarkus on talle antud? Kust ta saab väe imesid teha?
3 “Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
Kas ta pole mitte see puusepp, Maarja poeg, Jaakobuse, Joosepi, Juuda ja Siimona vend? Kas tema õed ei ela meie juures?“Nad haavusid ja hülgasid ta.
4 Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
„Prohvetist peetakse lugu kõikjal, välja arvatud tema enda kodulinnas, oma sugulaste ja pereliikmete hulgas, “ütles Jeesus neile.
5 Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
Seepärast ei saanud Jeesus teha seal mingeid imetegusid, ta ainult tervendas mõned haiged.
6 Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
Ta oli nende usupuuduse tõttu hämmastunud. Jeesus rändas mööda külasid ja õpetas ringi käies.
7 Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
Ta kutsus kokku kaksteist jüngrit ja hakkas neid kahekaupa välja saatma, andes neile meelevalla kurjade vaimude üle.
8 na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
Ta ütles, et nad ei võtaks peale jalutuskepi midagi kaasa − ei leiba, kotti ega raha vöötaskus.
9 lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
Nad võisid kanda sandaale, kuid ei tohtinud lisasärki kaasa võtta.
10 Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
„Kui teid kutsutakse majja, siis jääge sinna kuni lahkumiseni, “ütles ta neile.
11 Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
„Kui teid vastu ei võeta ega kuulata, siis puistake lahkudes oma jalgadelt tolm maha märgiks, et olete nad nende enda hooleks jätnud.“
12 Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
Nii nad siis käisid ringi ja käskisid inimestel meelt parandada.
13 Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
Nad ajasid välja palju kurje vaime ning tegid õliga võides terveks palju haigeid.
14 Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
Ka kuningas Heroodes kuulis Jeesusest, kuna ta oli tuntuks saanud. Mõned ütlesid: „See on surnuist ülestõusnud Ristija Johannes. Sellepärast tal on nii imelised võimed.“
15 Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
Teised ütlesid: „See on Eelija.“Veel mõned ütlesid: „Ta on prohvet, nagu üks mineviku prohvetitest.“
16 Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
Aga kui Heroodes sellest kuulis, ütles ta: „See on Johannes, kellel ma pea maha võtsin! Ta on surnuist üles tõusnud!“
17 Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
Sest Heroodes oli andnud korralduse Johannes vahistada ja vangi panna oma venna Filippuse naise Heroodiase pärast, kellega Heroodes oli abiellunud.
18 Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
Johannes oli Heroodesele öelnud: „Oma venna naisega abiellumine on seaduse vastu.“
19 Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
Seepärast pidas Heroodias Johannese vastu vimma ja tahtis teda tappa, kuid tal ei olnud võimalik seda korraldada,
20 maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
sest Heroodes teadis, et Johannes on püha mees, kes tegi seda, mis on õige. Heroodes kaitses Johannest ja kuigi Johannese sõnad häirisid teda väga, oli ta ikkagi hea meelega kuulanud, mis Johannesel öelda oli.
21 Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
Heroodiase võimalus tuli Heroodese sünnipäeval. Heroodes korraldas suure peo ülikutele, sõjapealikutele ja Galilea tähtsatele juhtidele.
22 Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
Heroodiase tütar tuli sisse ja tantsis neile. Tema esinemine rõõmustas Heroodest ja teisi, kes temaga peol olid, nii väga, et ta ütles neiule:
23 Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
„Palu mult ükskõik mida ja ma annan selle sulle.“Ta kinnitas oma lubadust vandega: „Ma annan sulle kas või pool oma kuningriigist.“
24 Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
Neiu läks välja ja küsis oma ema käest: „Mida ma peaksin paluma?“„Ristija Johannese pead, “vastas ema.
25 Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
Tüdruk kiirustas sisse tagasi ja ütles kuningale: „Ma tahan, et sa annaksid mulle kohe Ristija Johannese pea kandikul.“
26 Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
Kuningas oli vapustatud, aga kuna ta oli oma külaliste ees vande andnud, ei tahtnud ta palvest keelduda.
27 Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
Seega saatis ta kohe timuka Johannese pead tooma. Pärast seda, kui timukas oli vanglas Johannesel pea maha võtnud,
28 Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
tõi ta pea kandikul kohale ja andis selle tüdrukule ning tüdruk andis selle emale.
29 Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
Kui Johannese jüngrid juhtunust kuulsid, tulid nad ja viisid tema keha hauakambrisse.
30 Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
Apostlid tulid tagasi ja kogunesid Jeesuse ümber. Nad rääkisid talle kõigest, mida nad olid teinud ja õpetanud.
31 Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
„Tulge minuga, oleme omapead. Lähme vaiksesse kohta ja puhkame veidi, “ütles Jeesus neile, sest tulijaid ja minejaid oli nii palju, et neil ei olnud isegi aega süüa.
32 Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
Nii läksid nad paadiga vaiksesse kohta, et omapead olla.
33 Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
Aga rahvas nägi neid lahkumas ja tundis nad ära. Seega jooksis rahvas kõigist ümbruskonna linnadesse ette ja jõudis enne neid kohale.
34 Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
Kui Jeesus paadist välja tuli ja suurt rahvahulka nägi, tundis ta neile kaasa, sest nad olid nagu karjaseta lambad. Nii hakkas ta neile paljudest asjadest õpetama.
35 Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
Päev kaldus õhtusse ning jüngrid tulid Jeesuse juurde ja ütlesid talle: „Me oleme küladest kaugel ja aeg on juba hiline.
36 Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
Sa peaks rahvale ütlema, et nad läheksid ja ostaksid küladest ja maakoha elanikelt endale midagi süüa.“
37 Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
Ent Jeesus vastas: „Andke teie neile midagi süüa.“„Mida? Kõigile neile inimestele leiva ostmiseks oleks meil vaja rohkem kui kuue kuu palka, “vastasid jüngrid.
38 Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
„Kui palju leiba teil siis on?“küsis Jeesus. „Minge ja vaadake.“Nad läksid ja uurisid ning ütlesid talle: „Viis leiba ja paar kala.“
39 Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
Jeesus käskis kõigil rühmade kaupa rohelisele murule maha istuda.
40 Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
Nad istusid sajastes ja viiekümnestes rühmades.
41 Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
Seejärel võttis Jeesus viis leiba ja kaks kala. Taeva poole vaadates õnnistas ta toitu ja murdis leiva tükkideks. Siis andis ta leiva jüngritele, et nad annaksid rahvale, ning jagas neile kõigile ka kala.
42 Walikula wote hadi wakatosheka.
Kõik sõid, kuni kõht sai täis.
43 Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
Siis kogusid nad leiva ja kala jäägid kokku − kaksteist korvitäit.
44 Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
Toidust sai söönuks viis tuhat meest ja nende perekonnad.
45 Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
Kohe pärast seda käskis Jeesus jüngritel minna tagasi paati. Nad pidid suunduma järve teisel kaldal asuvasse Betsaidasse, Jeesus saatis sel ajal rahva laiali.
46 Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
Kui ta oli inimestega hüvasti jätnud, läks ta üles mägedesse palvetama.
47 Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
Hiljem samal õhtul oli paat keset järve, sel ajal kui Jeesus oli veel üksinda maal.
48 Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
Ta nägi, kuidas lained paati hüpitasid, kui nad tugevalt aerutasid, sest tuul puhus vastu. Varahommikustel tundidel tuli Jeesus nende juurde vett pidi kõndides. Ta oleks võinud neist mööda minna,
49 Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
aga kui nad nägid teda vett pidi kõndimas, pidasid nad teda lummutiseks. Nad karjusid,
50 kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
sest nad kõik nägid teda ja olid väga kohkunud. Jeesus ütles neile kohe: „Ärge kartke, see olen mina! Ärge kohkuge!“
51 Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
Ta läks nende juurde ja ronis paati ning tuul vaibus. Nad olid täiesti rabatud,
52 Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
sest nad ei olnud oma kangekaelse, põikpäise hoiaku tõttu toidu jagamise ime tähendust mõistnud.
53 Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
Pärast mere ületamist jõudsid nad Genneesaretti ja panid paadi ankrusse.
54 Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
Kui nad välja ronisid, tundsid inimesed otsekohe Jeesuse ära.
55 Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
Nad jooksid kogu piirkonda laiali, et tuua kõik haiged mattidel sinna, kus nad olid kuulnud Jeesuse olevat.
56 Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.
Kuhu iganes Jeesus läks − küladesse, linnadesse või maapiirkonda −, toodi haiged turuplatsidele ja paluti, et Jeesus laseks haigetel kas või oma rõivaserva puudutada. Kõik, kes teda puudutasid, said terveks.

< Marko 6 >