< Marko 6 >
1 Na akaondoka hapo na kwenda mjini kwao, na wanafunzi wake wakamfuata.
Jesus left that place, and accompanied by his disciples, came into his own part of the country.
2 Sabato ilipofika, alianza kufundisha katika Sinagogi. Watu wengi walimsikia na wakashangazwa. Wakasema, “Amepata wapi mafundisho haya?” “Ni hekima gani hii aliyopewa?” “Anatendaje miujiza hii kwa mikono yake?”
When it came Sabbath he began to teach in the synagogue; many, as they listened, were deeply impressed. "Where did he get all this?" they asked; "What is the wisdom that is given to this man, and miracles such as these that happen at his hands?
3 “Je huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu na ndugu yao kina Yakobo, Yose, Yuda na Simioni? Je dada zake si wanaishi papa hapa pamoja nasi?” Na hawakufurahishwa na Yesu.
Is not this the carpenter, the son of Mary, and the brother of Jamesand Joses and Judas and Simon? And are not his sisters here with us?"
4 Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika mji wake na miongoni mwa ndugu zake na nyumbani mwake.”
So they disapproved of him. Then Jesus said to them, "A prophet is not without honor except in his native land and among his relatives and in his home."
5 Hakuweza kutenda miujiza hapo, ila aliwawekea mikono wagonjwa wachache akawaponya.
And he was unable to do any miracle there, except that he laid his hands on a few sick folk and healed them.
6 Alishangazwa sana kwa sababu ya kutokuamini kwao. Kisha alivitembelea vijiji vya jirani akifundisha.
And he wondered at their lack of faith. So he went among the neighboring villages, teaching.
7 Aliwaita wale wanafunzi kumi na wawili akaanza kuwatuma wawili wawili. Aliwapa mamlaka juu ya pepo wachafu,
Then summoning the Twelve to him, he began to send them out two by two, giving them authority over unclean spirits.
8 na kuwaamuru wasichukue chochote wanapokwenda isipokuwa fimbo tu. Wasichukue mkate, wala mkoba, wala fedha kibindoni;
He bade them take nothing but a staff for their journey; no bread, no wallet, no coins in their purse;
9 lakini wavae viatu, na siyo kanzu mbili.
they were to wear sandals, but not to put on two tunics.
10 Na akawaambia, “Nyumba yoyote mtakayoingia, kaeni hapo mpaka mtakapoondoka.
"Wherever you enter a house," he told them, "remain there until you leave the place;
11 Na mji wowote usipowapokea wala kuwasikiliza, ondokeni kwao, kung'uteni mavumbi ya miguu yenu, iwe ushuhuda kwao.”
and if any place does not receive you, or listen to you, as you go out of it shake off the dust under your feet, as a warning to them."
12 Nao wakaenda wakitangaza watu watubu na kuacha dhambi zao.
So they fared forth and summoned men to repentance.
13 Waliwafukuza pepo wengi, na waliwapaka mafuta wagonjwa na wakaponywa.
They cast out many demons, and anointed many sick people with oil and cured them.
14 Mfalme Herode aliposikia hayo, kwa kuwa jina la Yesu lilikuwa limejulikana sana. Baadhi walisema, “Yohana mbatizaji amefufuka na kwa sababu hiyo, hii nguvu ya miujiza inafanya kazi ndani yake.”
King Herod heard it, for the name of Jesus had become well known, People were saying, "Johnthe Baptist is risen from the dead, and on that account these powers are working in him."
15 Baadhi yao wakasema, “Huyu ni Eliya,” Bado wengine wakasema, “Huyu ni nabii, kama mmoja wa wale manabii wa zamani.”
"He is Elijah," said others. And still others were saying, "He is a prophet, like one of the old prophets."
16 Lakini Herode aliposikia haya akasema, “Yohana, niliyemkata kichwa amefufuliwa.”
But when Herod heard, he said, "That Johnwhom I beheaded has come back to life."
17 Maana Herode mwenyewe aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani kwa sababu ya Herodia (mke wa kaka yake Filipo) kwa sababu yeye alikuwa amemuoa.
Now this Herod had sent and arrested John, and bound him in prison, for the sake of Herodias, his brother Philip’s wife, whom he had married.
18 Kwa maana Yohana alimwambia Herode, “Si halali kumuoa mke wa kaka yako.”
For Johnhad often told Herod, "It is not right for you to live with your brother’s wife."
19 Lakini Herodia alianza kumchukia na alikuwa akitaka kumuua, lakini hakuweza,
So Herodias hated him, and wished to put him to death;
20 maana Herode alimwogopa Yohana; alijua kwamba ni mwenye haki mtu mtakatifu, na alimwacha salama. Na alipoendelea kumsikiliza alihuzunika sana, lakini alifurahi kumsikiliza.
but she could not, for Herod was afraid of Johnbecause he knew that he was a just and holy man. So he kept him safe. When he listened to Johnhe was much exercised, yet he found pleasure in listening to him.
21 Hata ilipofika wakati mwafaka ikiwa imekaribia siku ya kuzaliwa Herode akawaandalia moafisa wake karamu, na makamanda, na viongozi wa Galilaya.
Then came a convenient day, when Herod on his birthday held a feast for his lords and generals and the leading men of Galilee,
22 Ndipo binti wa Herodia akaingia na kucheza mbele yao, akamfurahisha Herode na wageni walioketi wakati wa chakula cha jioni. Ndipo mfalme akamwambia binti, “Niombe chochote unachotaka nami nitakupa.”
at which the daughter of Herodias herself came in and danced. She charmed Herod and his guests. "Ask me whatever you want," said the king to the young girl, "and I will give it to you."
23 Akamwapia na kusema, chochote utakachoniomba, nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.”
He even swore to her that whatever she asked, he would give it to her, up to half his kingdom.
24 Akatoka nje akamuuliza mama yake, “Niombe nini?” Akasema, “Kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
So she came out and said to her mother, "What shall I ask for?" "The head of Johnthe Baptist," she replied.
25 Na mara moja akaingia kwa mfalme akaanza kusema, “Nataka unipatie ndani ya sahani, kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
So she at once hurried in to the king and made her request, "I want you," she said, "to give me, without delay, the head of Johnthe Baptist on a charger."
26 Mfalme alisikitishwa sana, lakini kwa sababu ya kiapo chake na kwa ajili ya wageni, hakuweza kumkatalia ombi lake.
Then the king was exceedingly sorry; yet on account of his oaths and his guests he was unwilling to disappoint her.
27 Hivyo, mfalme akatuma askari kati ya walinzi wake na kuwaagiza kwenda kumletea kichwa cha Yohana. Mlinzi alikwenda kumkata kichwa akiwa kifungoni.
So he sent at once a soldier of the guard with orders to bring his head.
28 Akakileta kichwa chake kwenye sahani na kumpatia binti, na binti akampa mama yake.
And he went and beheaded Johnin prison, brought his head on a platter, and gave it to the young girl, and she gave it to her mother.
29 Na wanafunzi wake waliposikia hayo, walikwenda kuuchukua mwili wake wakaenda kuuzika kaburini.
When John’s disciples heard of this, they came, and took his body, and laid it in a tomb.
30 Na mitume, walikusanyika pamoja mbele ya Yesu, wakamweleza yote waliyofanya na waliyoyafundisha.
When the apostles had come back to Jesus, they told him all the things they had done, and all they had taught.
31 Naye akawaambia, “Njooni wenyewe mahali pa faragha na tupumzike kwa muda.” Watu wengi walikuwa wanakuja na kuondoka, hata hawakupata nafasi ya kula.
Then he said to them, "Come apart, yourselves, to a quiet spot, and rest a while." For there were many coming and going, and they could not get time even to eat.
32 Hivyo wakapanda mashua wakaenda mahali pa faragha peke yao.
So they sailed away privately to a solitary place.
33 Lakini waliwaona wakiondoka na wengi wakawatambua, kwa pamoja walikimbia kwa miguu kutoka miji yote, nao wakafika kabla yao.
However, many saw them going, and recognized them, and ran together by land from all the neighboring towns, and arrived there first.
34 Walipofika pwani, aliona umati mkubwa na akawahurumia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji. Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.
So when Jesus landed he saw a vast multitude, and he was moved with compassion for them, because they were like sheep without a shepherd, and he began to teach them many things.
35 Muda ulipoendelea sana, wanafunzi wakamjia wakamwambia,”Hapa ni mahali pa faragha na muda umeendelea.
Then when the day was now far spent, his disciples came to him and said. "This place is desert, and the day is now far spent.
36 Uwaage waende miji ya jirani na vijiji ili wakajinunulie chakula.”
Send the people away so that they may go to the farms and villages about here, and buy themselves something to eat."
37 Lakini akawajibu akisema, “Wapeni ninyi chakula.” Wakamwambia, “Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa wale?”
In answer he said to them, "You yourselves are to give them food." "Are we to go and buy fifty dollars worth of bread," they said, "and give them food?"
38 Akawambia,” Mna mikate mingapi? Nendeni mkaangalie.” walipopata wakamwambia, “Mikate mitano na samaki wawili.”
"How many loaves have you?" he answered. "Go and see." When they had found out, they said, "Five, and two fishes."
39 Akawaamuru watu waketi katika makundi juu ya majani mabichi.
Then he directed them to make all sit down by companies on the green grass.
40 Wakawaketisha katika makundi; makundi ya mamia kwa hamsini.
And they sat down like beds in a garden, by hundreds and by fifties.
41 Kisha akachukua mikate mitano na samaki wawili, na kutazama mbinguni, akaibariki kisha akawapa wanafunzi waweke mbele ya umati. Na kisha aligawa samaki wawili kwa watu wote.
Then he took the five loaves and the two fishes, and looking up to heaven he blessed, broke the loaves in pieces, and kept giving to the disciples to distribute.
42 Walikula wote hadi wakatosheka.
The two fish also he divided to them all.
43 Walikusanya vipande vya mikate iliyobaki, Vikajaa vikapu kumi na viwili, na pia vipande vya samaki.
All ate and had enough; and they carried away broken fragments of bread and of fish, enough to fill twelve baskets.
44 Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate.
Those who ate the bread were five thousand adult men.
45 Mara akawaambia wapande kwenye mashua waende sehemu nyingine, hadi Bethsaida, wakati Yeye akiwaaga makutano.
Then he at once compelled the disciples to embark in the boat and go before him to Bethsaida on the other side, while he sent the people away.
46 Walipokuwa wamekwisha kuondoka, akaenda mlimani kuomba.
After he had taken leave of them, he went away into the mountain to pray.
47 Kulipokuwa jioni, na mashua yao wakati huo ikiwa katikati ya bahari, naye alikuwa peke yake nchi kavu.
And when evening came, the boat was half-way across the sea, while he was on shore alone;
48 Na aliwaona wakitaabika kupiga makasia kwa sababu upepo uliwazuia. Ilipokaribia asubuhi akawaendea, akitembea juu ya maji, na alitaka kuwapita.
but when he saw them distressed in rowing (for the wind was against them), about the fourth watch of the night he went to them, walking upon the sea,
49 Lakini walipomwona anatembea juu ya maji, wakaingiwa na wasiwasi wakidhani ni mzimu hata wakapiga kelele.
they thought it was an apparition and shrieked aloud, for they all saw him and were terrified.
50 kwa sababu walimwona wakajawa na hofu. Mara akasema nao akawaambia, “Muwe wajasiri! ni mimi! Msiwe na hofu.”
But he at once spoke with them, saying. "Courage! It is I. Do not be afraid!"
51 Akaingia ndani ya mashua, na upepo ukaacha kuvuma, nao wakamshangaa kabisa.
Then he got into the boat beside them, and the wind ceased, and they were utterly astounded,
52 Hivyo hawakuwa wameelewa maana ya ile mikate. Maana akili zao zilikuwa na uelewa mdogo.
for they had not understood about the loaves; on the contrary their heart was hardened.
53 Nao walipovuka ng'ambo, walifika nchi ya Genesareti mashua ikatia nanga.
When they had crossed over they landed at Gennesaret and moored to the shore.
54 Walipotoka nje ya mashua, mara wakamtambua.
As soon as they got out of the boat, the people at once recognized him,
55 Wakakimbia kutangaza katika mkoa mzima na wakaanza kuwaleta wagonjwa kwa machela, kila waliposikia anakuja.
and began running over that whole country, and carrying the sick about on their beds, wherever they heard he was.
56 Popote alipoingia katika vijiji, au mjini, au katika nchi, waliwaweka wagonjwa mahali pa soko, na wakamsihi awaruhusu kugusa pindo la vazi lake. Na wote waliomgusa waliponywa.
And whenever he entered into villages or cities or the fields they would lay the sick in the market-places and beseech him to let them touch even the tassel of his cloak, and all who touched him were made well.