< Marko 5 >
1 Walikuja mpaka upande mwingine wa bahari, katika mkoa wa Gerasi
So they arrived at the opposite shore of the Lake, in the country of the Gerasenes.
2 Na ghafla wakati Yesu alipokuwa akitoka nje ya mtumbwi, mtu mwenye roho chafu alikuja kwake kutoka makaburini.
At once, on His landing, there came from the tombs to meet Him a man possessed by a foul spirit.
3 Mtu huyu aliishi makaburini. Hakuna aliyeweza kumzuia zaidi, hakuna hata kwa minyororo.
This man lived among the tombs, nor could any one now secure him even with a chain;
4 Alikuwa amefungwa nyakati nyingi kwa pingu na minyororo. Aliikata minyororo na pingu zake zilivunjwa. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
for many a time he had been left securely bound in fetters and chains, but afterwards the chains lay torn link from link, and the fetters in fragments, and there was no one strong enough to master him.
5 Usiku na mchana akiwa makaburini na milimani, alilia na kujikata yeye mwenyewe kwa mawe makali.
And constantly, day and night, he remained among the tombs or on the hills, shrieking, and mangling himself with sharp stones.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alikimbilia kwake na kuinama mbele yake.
And when he saw Jesus in the distance, he ran and threw himself at His feet,
7 Alilia kwa sauti kuu, “Wataka nikufanyie nini, Yesu, Mwana wa Mungu aliye Juu sana? Ninakusihi kwa Mungu mwenyewe, usinitese.”
crying out in a loud voice, "What hast Thou to do with me, Jesus, Son of God Most High? In God's name I implore Thee not to torment me."
8 Kwa kuwa alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe roho mchafu.”
For He had said to him, "Foul spirit, come out of the man."
9 Naye alimwuliza, “Jina lako ni nani?” Naye alimjibu, “Jina langu ni Legion, kwa kuwa tuko wengi.”
Jesus also questioned him. "What is your name?" He said. "Legion," he replied, "for there are a host of us."
10 Alimsihi tena na tena asiwapeleke nje ya mkoa.
And he earnestly entreated Him not to send them away out of the country.
11 Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likilishwa juu ya kilima,
Feeding there, on the mountain slope, was a great herd of swine.
12 nao walimsihi, wakisema, “Tutume kwa nguruwe; tuingie ndani yao.”
So they besought Jesus. "Send us to the swine," they said, "so that we may enter into them."
13 Hivyo aliwaruhusu; roho wachafu waliwatoka na kuingia ndani ya nguruwe, nao walikimbilia chini ya kilima mpaka baharini, na karibia nguruwe elfu mbili walizama baharini.
He gave them leave; and the foul spirits came out and entered into the swine, and the herd--about 2,000 in number--rushed headlong down the cliff into the Lake and were drowned in the Lake.
14 Na wale waliokuwa wakiwalisha nguruwe walikimbia na kutoa taarifa ya kilichotokea katika mji na katika nchi. Ndipo watu wengi walitoka kwenda kuona kilichotokea.
The swineherds fled, and spread the news in town and country. So the people came to see what it was that had happened;
15 Ndipo walikuja kwa Yesu na walimwona mtu aliyepagawa na pepo—aliyekuwa na Jeshi—amekaa chini, amevikwa, na akiwa katika akili yake timamu, nao waliogopa.
and when they came to Jesus, they beheld the demoniac quietly seated, clothed and of sane mind--the man who had had the legion; and they were awe-stricken.
16 Wale waliokuwa wameona kilichotokea kwa mtu aliyekuwa amepagawa na pepo waliwaambia kilichotokea kwake na pia kuhusu nguruwe.
And those who had seen it told them the particulars of what had happened to the demoniac, and all about the swine.
17 Nao walianza kumsihi aondoke katika mkoa wao.
Then they began entreating Him to depart from their district.
18 Na alipokuwa akiingia ndani ya mtumbwi, mtu aliyekuwa amepagawa na mapepo alimsihi kwamba aende pamoja naye.
As He was embarking, the man who had been possessed asked permission to accompany Him.
19 Lakini hakumruhusu, lakini alimwambia, “Nenda nyumbani kwako na kwa watu wako, na uwaambie alikufanyia Bwana, na rehema aliyokupa.”
But He would not allow it. "Go home to your family," He said, "and report to them all that the Lord has done for you, and the mercy He has shown you."
20 Hivyo alienda na alianza kutangaza mambo makuu ambayo Yesu amefanya kwake katika Dekapoli, na kila mmoja alistaajabu.
So the man departed, and related publicly everywhere in the Ten Towns all that Jesus had done for him; and all were astonished.
21 Na wakati Yesu alipovuka tena upande mwingine, ndani ya mtumbwi, umati mkubwa ulikusanyika kumzunguka, alipokuwa kando ya bahari.
When Jesus had re-crossed in the boat to the other side, a vast multitude came crowding to Him; and He was on the shore of the Lake,
22 Na mmoja wa kiongozi wa sinagogi, aliyeitwa Yairo, alikuja, na alipomwona, alianguka miguuni pake.
when there came one of the Wardens of the Synagogue--he was called Jair--who, on beholding Him, threw himself at His feet,
23 Akamsihi zaidi na zaidi, akisema, “Binti yangu mdogo anakaribia kufa. Ninakusihi, njoo na uweke mikono yako juu yake ili kwamba aweze kupata afya na kuishi.”
and besought Him with many entreaties. "My little daughter," he said, "is at the point of death: I pray you come and lay your hands upon her, that she may recover and live."
24 Hivyo alikwenda pamoja naye, na umati mkubwa ulimfuata nao walimzonga karibu wakimzunguka.
And Jesus went with him. And a dense crowd followed Him, and thronged Him on all sides.
25 Kulikuwa na mwanamke ambaye damu yake ilikuwa imetoka kwa miaka kumi na miwili.
Now a woman who for twelve years had suffered from haemorrhage,
26 Aliteseka vya kutosha chini ya matabibu wengi na alitumia kila kitu alichokuwa nacho. Hata hivyo hakusaidika kwa chochote, lakini badala yake alizidi kuwa na hali mbaya.
and had undergone many different treatments under a number of doctors and had spent all she had without receiving benefit but on the contrary growing worse,
27 Alisikia habari kuhusu Yesu. Hivyo alikuja nyuma yake wakati alipokuwa akitembea ndani ya umati, naye aliligusa vazi lake.
heard of Jesus. And she came in the crowd behind Him and touched His cloak;
28 Kwa kuwa alisema, “Kama nikiyagusa mavazi yake tu, nitakuwa mzima.”
for she said, "If I but touch His clothes, I shall be cured."
29 Alipomgusa, kutokwa damu kulikoma, na alijisikia katika mwili wake kwamba aliponywa kutoka kwenye mateso yake.
In a moment the flow of her blood ceased, and she felt in herself that her complaint was cured.
30 Na ghafla Yesu aligundua ndani yake mwenyewe kwamba nguvu zimemtoka. Na aligeuka huku na huku katika umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyeligusa vazi langu?”
Immediately Jesus, well knowing that healing power had gone from within Him, turned round in the crowd and asked, "Who touched my clothes?"
31 Wanafunzi wake walimwambia, “Unaona umati huu umekusonga ukikuzunguka, nawe wasema, 'Ni nani aliyenigusa?'”
"You see the multitude pressing you on all sides," His disciples exclaimed, "and yet you ask, 'Who touched me?'"
32 Lakini Yesu alitazama huku na huku kuona ambaye aliyekuwa amefanya hili.
But He continued looking about to see the person who had done this,
33 Mwanamke, akijua kilichotokea kwake, aliogopa na kutetemeka. Alikuja na alianguka chini mbele yake na kumwambia ukweli wote.
until the woman, frightened and trembling, knowing what had happened to her, came and threw herself at His feet, and told Him all the truth.
34 Alisema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa amani na uponywe kutoka kwenye ugonjwa wako.”
"Daughter," He said, "your faith has cured you: go in peace, and be free from your complaint."
35 Alipokuwa akizungumza, baadhi ya watu walikuja kutoka kwa kiongozi wa Sinagogi, wakisema, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua mwalimu?”
While He is yet speaking, men come from the house to the Warden, and say, "Your daughter is dead: why trouble the Rabbi further?"
36 Lakini Yesu aliposikia ambacho walikisema, alimwambia kiongozi wa Sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
But Jesus, overhearing the words, said to the Warden, "Do not be afraid; only have faith."
37 Hakumruhusu yeyote kuongozana naye, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yohana, ndugu yake Yakobo.
And He allowed no one to accompany Him except Peter and the brothers James and John.
38 Walikuja nyumbani kwa kiongozi wa Sinagogi naye aliona vurugu, kulia kwingi na kuomboleza.
So they come to the Warden's house. Here He gazes on a scene of uproar, with people weeping aloud and wailing.
39 Alipoingia nyumbani, aliwaambia, “Kwa nini mmesikitika na kwa nini mnalia? Mtoto hajafa bali amelala.”
He goes in. "Why all this outcry and loud weeping?" He asks; "the child is asleep, not dead."
40 Walimcheka, lakini yeye, aliwatoa wote nje, alimchukua baba wa mtoto na mama na wale waliokuwa pamoja naye, na aliingia ndani alimokuwa mtoto.
To this their reply is a scornful laugh. He, however, puts them all out, takes the child's father and mother and those He has brought with Him, and enters the room where the child lies.
41 Aliuchukua mkono wa mtoto na alimwambia, “Talitha koum,” ambayo ni kusema, “Binti mdogo, nakuambia, amka.”
Then, taking her by the hand, He says to her, "Talitha, koum;" that is to say, "Little girl, I command you to wake!"
42 Ghafla mtoto aliamka na kutembea (kwa kuwa alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Na ghafla walishikwa na mshangao mkubwa.
Instantly the little girl rises to her feet and begins to walk (for she was twelve years old). They were at once beside themselves with utter astonishment;
43 Aliwaamuru kwa nguvu kwamba hakuna yeyote anapaswa kujua kuhusu hili. Na aliwaambia wampatie yule binti chakula.
but He gave strict injunctions that the matter should not be made known, and directed them to give her something to eat.