< Marko 5 >
1 Walikuja mpaka upande mwingine wa bahari, katika mkoa wa Gerasi
And they came to the other side of the sea into the country of the Gadarenes.
2 Na ghafla wakati Yesu alipokuwa akitoka nje ya mtumbwi, mtu mwenye roho chafu alikuja kwake kutoka makaburini.
And when he came out of the boat, straightaway there met him out of the sepulchers a man with an unclean spirit who had his habitation among the sepulchers.
3 Mtu huyu aliishi makaburini. Hakuna aliyeweza kumzuia zaidi, hakuna hata kwa minyororo.
And no man was able to bind him, not even with chains.
4 Alikuwa amefungwa nyakati nyingi kwa pingu na minyororo. Aliikata minyororo na pingu zake zilivunjwa. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
Because he was often bound with shackles and chains, and the chains were pulled apart by him, and the shackles broken in pieces. And no man had strength to subdue him.
5 Usiku na mchana akiwa makaburini na milimani, alilia na kujikata yeye mwenyewe kwa mawe makali.
And always, night and day, in the mountains and in the sepulchers, he was crying out, and cutting himself with stones.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alikimbilia kwake na kuinama mbele yake.
And when he saw Jesus from a distance, he ran and worshiped him.
7 Alilia kwa sauti kuu, “Wataka nikufanyie nini, Yesu, Mwana wa Mungu aliye Juu sana? Ninakusihi kwa Mungu mwenyewe, usinitese.”
And having cried out in a great voice, he said, What is with me and with thee, Jesus, thou Son of the Most High God? I adjure thee by God, do not torment me.
8 Kwa kuwa alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe roho mchafu.”
For he said to him, Come out from the man, thou unclean spirit.
9 Naye alimwuliza, “Jina lako ni nani?” Naye alimjibu, “Jina langu ni Legion, kwa kuwa tuko wengi.”
And he demanded him, What is thy name? And he answered, saying, My name is Legion, because we are many.
10 Alimsihi tena na tena asiwapeleke nje ya mkoa.
And he besought him much that he would not send them outside of the territory.
11 Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likilishwa juu ya kilima,
Now there was near the mountain a great herd of swine feeding.
12 nao walimsihi, wakisema, “Tutume kwa nguruwe; tuingie ndani yao.”
And all the demons besought him, saying, Send us into the swine, so that we may enter into them.
13 Hivyo aliwaruhusu; roho wachafu waliwatoka na kuingia ndani ya nguruwe, nao walikimbilia chini ya kilima mpaka baharini, na karibia nguruwe elfu mbili walizama baharini.
And straightaway, Jesus allowed them. And the unclean spirits having come out, entered into the swine. And the herd stampeded down the slope into the sea, and were drowned in the sea. And there were about two thousand.
14 Na wale waliokuwa wakiwalisha nguruwe walikimbia na kutoa taarifa ya kilichotokea katika mji na katika nchi. Ndipo watu wengi walitoka kwenda kuona kilichotokea.
And those who fed the swine fled, and reported in the city and in the fields. And they came to see what it was that happened.
15 Ndipo walikuja kwa Yesu na walimwona mtu aliyepagawa na pepo—aliyekuwa na Jeshi—amekaa chini, amevikwa, na akiwa katika akili yake timamu, nao waliogopa.
And they come to Jesus, and see the man who was demon-possessed, sitting, and clothed, and in his right mind (the man who had the legion), and they were afraid.
16 Wale waliokuwa wameona kilichotokea kwa mtu aliyekuwa amepagawa na pepo waliwaambia kilichotokea kwake na pia kuhusu nguruwe.
And those who saw it related to them how it happened to the man who was demon-possessed, and about the swine.
17 Nao walianza kumsihi aondoke katika mkoa wao.
And they began to beg him to depart from their borders.
18 Na alipokuwa akiingia ndani ya mtumbwi, mtu aliyekuwa amepagawa na mapepo alimsihi kwamba aende pamoja naye.
And as he entered into the boat, the man who had been demon-possessed besought him that he might be with him.
19 Lakini hakumruhusu, lakini alimwambia, “Nenda nyumbani kwako na kwa watu wako, na uwaambie alikufanyia Bwana, na rehema aliyokupa.”
But Jesus did not allow him, but says to him, Go to thy house to thy men, and report to them how much the Lord has done for thee, and was merciful to thee.
20 Hivyo alienda na alianza kutangaza mambo makuu ambayo Yesu amefanya kwake katika Dekapoli, na kila mmoja alistaajabu.
And he departed, and began to proclaim in Decapolis how much Jesus did for him. And all men marveled.
21 Na wakati Yesu alipovuka tena upande mwingine, ndani ya mtumbwi, umati mkubwa ulikusanyika kumzunguka, alipokuwa kando ya bahari.
And when Jesus crossed over again in the boat to the other side, a great multitude gathered to him, and he was near the sea.
22 Na mmoja wa kiongozi wa sinagogi, aliyeitwa Yairo, alikuja, na alipomwona, alianguka miguuni pake.
And behold, one of the synagogue rulers comes, Jairus by name. And having seen him, he falls at his feet,
23 Akamsihi zaidi na zaidi, akisema, “Binti yangu mdogo anakaribia kufa. Ninakusihi, njoo na uweke mikono yako juu yake ili kwamba aweze kupata afya na kuishi.”
and besought him much, saying, My little daughter has a terminal condition, so that having come, thou may lay thy hands on her, that she may be saved and will live.
24 Hivyo alikwenda pamoja naye, na umati mkubwa ulimfuata nao walimzonga karibu wakimzunguka.
And he went with him, and a great multitude followed him, and they thronged him.
25 Kulikuwa na mwanamke ambaye damu yake ilikuwa imetoka kwa miaka kumi na miwili.
And a certain woman, being with an issue of blood twelve years,
26 Aliteseka vya kutosha chini ya matabibu wengi na alitumia kila kitu alichokuwa nacho. Hata hivyo hakusaidika kwa chochote, lakini badala yake alizidi kuwa na hali mbaya.
and having suffered many things by many physicians, and having spent all of her things, and was helped nothing, but who became worse instead,
27 Alisikia habari kuhusu Yesu. Hivyo alikuja nyuma yake wakati alipokuwa akitembea ndani ya umati, naye aliligusa vazi lake.
when she heard about Jesus, having come in the crowd from behind, she touched his garment.
28 Kwa kuwa alisema, “Kama nikiyagusa mavazi yake tu, nitakuwa mzima.”
For she said, If I but touch his garments, I will be healed.
29 Alipomgusa, kutokwa damu kulikoma, na alijisikia katika mwili wake kwamba aliponywa kutoka kwenye mateso yake.
And straightaway the flow of her blood was dried up, and she knew in the body that she was healed of her scourge.
30 Na ghafla Yesu aligundua ndani yake mwenyewe kwamba nguvu zimemtoka. Na aligeuka huku na huku katika umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyeligusa vazi langu?”
And straightaway, Jesus, when he recognized in himself that power went forth from him, having turned around in the crowd, he said, Who touched my garments?
31 Wanafunzi wake walimwambia, “Unaona umati huu umekusonga ukikuzunguka, nawe wasema, 'Ni nani aliyenigusa?'”
And his disciples said to him, Thou see the multitude crowding thee, and thou say, Who touched me?
32 Lakini Yesu alitazama huku na huku kuona ambaye aliyekuwa amefanya hili.
And he looked around to see the woman who did this thing.
33 Mwanamke, akijua kilichotokea kwake, aliogopa na kutetemeka. Alikuja na alianguka chini mbele yake na kumwambia ukweli wote.
But the woman fearing and trembling, knowing what has happened to her, came and fell down before him, and told him all the truth.
34 Alisema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa amani na uponywe kutoka kwenye ugonjwa wako.”
And he said to her, Daughter, thy faith has healed thee. Go in peace, and be healthy from thy scourge.
35 Alipokuwa akizungumza, baadhi ya watu walikuja kutoka kwa kiongozi wa Sinagogi, wakisema, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua mwalimu?”
While he still spoke, they come from the synagogue ruler saying, Thy daughter died, why still trouble the teacher?
36 Lakini Yesu aliposikia ambacho walikisema, alimwambia kiongozi wa Sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
But straightaway, Jesus, having heard the word spoken, says to the ruler of the synagogue, Fear not, only believe.
37 Hakumruhusu yeyote kuongozana naye, isipokuwa Petro, Yakobo, na Yohana, ndugu yake Yakobo.
And he allowed no man to accompany him except Peter, and James, and John the brother of James.
38 Walikuja nyumbani kwa kiongozi wa Sinagogi naye aliona vurugu, kulia kwingi na kuomboleza.
And he comes to the house of the synagogue ruler, and sees a commotion, much weeping and wailing.
39 Alipoingia nyumbani, aliwaambia, “Kwa nini mmesikitika na kwa nini mnalia? Mtoto hajafa bali amelala.”
And when he entered in, he says to them, Why do ye make a commotion, and weep? The child did not die, but sleeps.
40 Walimcheka, lakini yeye, aliwatoa wote nje, alimchukua baba wa mtoto na mama na wale waliokuwa pamoja naye, na aliingia ndani alimokuwa mtoto.
And they ridiculed him. But he, having put them all out, takes the father of the child and the mother and those with him, and enters in where the child was lying.
41 Aliuchukua mkono wa mtoto na alimwambia, “Talitha koum,” ambayo ni kusema, “Binti mdogo, nakuambia, amka.”
And having taken the child's hand, he says to her, Talitha cumi. Which is, being interpreted, Little girl, I say to thee, awake.
42 Ghafla mtoto aliamka na kutembea (kwa kuwa alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Na ghafla walishikwa na mshangao mkubwa.
And straightaway the little girl rose up and walked, for she was twelve years old. And they were amazed with a great amazement.
43 Aliwaamuru kwa nguvu kwamba hakuna yeyote anapaswa kujua kuhusu hili. Na aliwaambia wampatie yule binti chakula.
And he commanded them much that no man should know this. And he said to give her to eat.