< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
He entered again into the synagogue, and there was a man there whose hand was withered.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
They watched him, whether he would heal him on the Sabbath day, that they might accuse him.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
He said to the man whose hand was withered, “Stand up.”
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
He said to them, “Is it lawful on the Sabbath day to do good or to do harm? To save a life or to kill?” But they were silent.
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
When he had looked around at them with anger, being grieved at the hardening of their hearts, he said to the man, “Stretch out your hand.” He stretched it out, and his hand was restored as healthy as the other.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
The Pharisees went out, and immediately conspired with the Herodians against him, how they might destroy him.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
Yeshua withdrew to the sea with his disciples; and a great multitude followed him from Galilee, from Judea,
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
from Jerusalem, from Idumaea, beyond the Jordan, and those from around Tyre and Sidon. A great multitude, hearing what great things he did, came to him.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
He spoke to his disciples that a little boat should stay near him because of the crowd, so that they wouldn’t press on him.
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
For he had healed many, so that as many as had diseases pressed on him that they might touch him.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
The unclean spirits, whenever they saw him, fell down before him and cried, “You are the Son of God!”
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
He sternly warned them that they should not make him known.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
He went up into the mountain and called to himself those whom he wanted, and they went to him.
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
He appointed twelve, that they might be with him, and that he might send them out to proclaim
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
and to have authority to heal sicknesses and to cast out demons:
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
Simon (to whom he gave the name Peter);
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
Jacob the son of Zebedee; and Yochanan, the brother of Jacob, (whom he called Benei-Regesh, which means, Sons of Thunder);
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
Andrew; Philip; Bartholomew; Matthew; Thomas; Jacob, the son of Halfai; Taddai; Simon the Zealot;
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
and Judah Iscariot, who also betrayed him. Then he came into a house.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
The multitude came together again, so that they could not so much as eat bread.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
When his friends heard it, they went out to seize him; for they said, “He is insane.”
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
The scribes who came down from Jerusalem said, “He has Beelzebul,” and, “By the prince of the demons he casts out the demons.”
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
He summoned them and said to them in parables, “How can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
If a kingdom is divided against itself, that kingdom cannot stand.
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
If a house is divided against itself, that house cannot stand.
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
If Satan has risen up against himself, and is divided, he can’t stand, but has an end.
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
But no one can enter into the house of the strong man to plunder unless he first binds the strong man; then he will plunder his house.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
“Most certainly I tell you, all sins of the descendants of man will be forgiven, including their blasphemies with which they may blaspheme;
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
but whoever may blaspheme against the Holy Spirit never has forgiveness, but is subject to eternal condemnation.” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
—because they said, “He has an unclean spirit.”
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
His mother and his brothers came, and standing outside, they sent to him, calling him.
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
A multitude was sitting around him, and they told him, “Behold, your mother, your brothers, and your sisters are outside looking for you.”
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
He answered them, “Who are my mother and my brothers?”
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
Looking around at those who sat around him, he said, “Behold, my mother and my brothers!
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
For whoever does the will of God is my brother, my sister, and mother.”

< Marko 3 >