< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
Again he went into a synagogue where there was a man with his hand withered.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
And they kept watching Jesus to see whether he would cure him on the Sabbath; so as to have some charge to bring against him.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
"Stand up," Jesus said to the man with the withered hand, "and come forward."
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
Then he asked them. "Is it lawful to do good on the Sabbath Day, or to do harm? to save a life, or to destroy it?"
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
They were silent. Then looking around upon them with anger, and deeply grieved by the hardening of their hearts, he said to the man, "Stretch out your hand!" He stretched it out, and the hand was at once completely restored.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
As soon as they came out, the Pharisees plotted against him with the Herodians, in order to destroy him.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
Then Jesus withdrew to the sea with his disciples; and a great crowd of people from Galilee followed.
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
From Judea, too, and Jerusalem, and Idumea, and from beyond Jordan, and from the district of Tyre and Sidon, they came to him a vast multitude, because they heard what he was doing.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
So he directed his disciples to keep a little boat in readiness for him, because of the crowd, to prevent their crushing him.
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
For he had healed so many that all the people who had ailments pressed upon him so as to touch him.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
And whenever the unclean spirits beheld him, they threw themselves down at his feet, screaming out, "You are the Son of God."
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
But over and over, he strictly forbade them to make him known.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
Then he went up the hillside and called to him those whom he chose, and they came to him.
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
Twelve of them whom he also called "Apostles," he appointed to be with him, and also that he might send them out to preach,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
and to have authority to cast out demons.
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
There was Simon, whom he surnamed Peter,
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
and James(them he surnamed Boanerges, that is, Sons of Thunder),
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and Jamesthe son of Alphaeus, and Thaddeus, and Simon the Zealot,
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
and Judas Iscariot who betrayed him.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
Then he went into a house, but again such a multitude assembled that they could not get their food.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
When his relatives heard of it, they came to take possession of him, for they said, "He is out of his mind."
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
The Scribes also who had come down from Jerusalem, said, "He is Beelzebub," and, "He casts out demons by the power of the Prince of the demons."
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
So when he had called them to him he spoke to them in parables. "How," said he, "can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
If a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand;
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
if a household be divided against itself, that household cannot stand;
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
and if Satan has revolted against himself, and is divided, he cannot stand. Nay, he meets his end!
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
"Indeed, no one can enter the strong man’s house and carry off his property without first binding the strong man; then he can plunder his house.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
In solemn truth I tell you that the sons of men shall be forgiven all their sins and all the blasphemies they may utter,
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
but he who blasphemes against the Holy Spirit is never forgiven. Nay, he is in the grasp of an eternal sin." (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
Because they kept saying, "He has an unclean spirit."
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
Then his mother and his brothers came up, and standing outside, they sent a messenger to him to call him.
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
Now a crowd was sitting round him and they told him, "See! your mother and your brothers and sisters are outside, wanting to see you."
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
"Who are my mother and my brothers?" he replied.
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
Then, with a glance at those who were in the circle sitting around him, he added.
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
"Here are my mother and my brothers! Whoever does the will of God, that one is my brother and sister and mother."

< Marko 3 >