< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
He came again into the synagogue, a man was there having a withered hand.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
And they were watching Him, if He will heal him on the Sabbath, that they might accuse Him.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
And He says to the man having a withered hand; Rise up in the midst.
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
And He says to them; Is it lawful to do good or to do evil on the Sabbath; to save life, or to kill? And they were silent.
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
And looking round on them with indignation, being grieved over the hardness of their hearts, He says to the man; Reach forth thy hand. And he reached it forth and it was restored.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
And the Pharisees, having gone out immediately along with the Herodians, took counsel against Him in order that they might kill Him.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
And Jesus departed with His disciples to the sea: and a great multitude followed Him from Galilee, and from Judea,
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
and from Jerusalem, and from Idumea, and from beyond the Jordan, and those about Tyre and Sidon, a great multitude, hearing so many things that He was doing, came to Him.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
And He said to His disciples, that a little boat should wait on Him in order that they may not tread on Him.
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
For He healed many; so that they were falling before Him so that they might touch Him, so many as had diseases.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
And unclean spirits, when they saw Him, fell down before Him, and were crying out, saying, Thou art the Son of God.
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
And He charged them much that they should not make Him known.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
And He goes up into the mountain, and calls whom He wished: and they went away to Him.
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
And He made twelve (apostles) that they may be with Him and that He may send them out to preach,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
and to have power to heal diseases, and to cast out the demons.
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
And He placed the name Peter on Simon;
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
and James the son of Zebedee, and John the brother of James; and on them He placed the names Boanerges, which is, Sons of thunder:
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
and Andrew and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the son of Alpheus, and Thaddeus, and Simon the Zealot, and Judas Iscariot,
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
who also betrayed Him.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
And He comes into a house; and the multitude come together again so they are not able to eat bread.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
And those along with Him hearing came out to arrest Him: for they continued to say, He is beside Himself.
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
And the scribes having come down from Jerusalem were saving, He has Beelzebul and He is casting out the demons through the prince of the demons.
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
And calling them to Him, He continued to speak to them in parables, How is Satan able to cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
And if a kingdom may be divided against itself, that kingdom is not able to stand,
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
and if a house may be divided against itself, that house will not be able to stand;
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
and if Satan stand up against himself, and is divided, he is not able to stand, but has an end.
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
No one is able, having entered into the house of a strong man, to spoil his goods, unless he may first bind the strong man, and then he will spoil his house.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
Truly I say unto you, that all sins shall be forgiven unto the sons of men, and blasphemies whatsoever they may blaspheme:
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
but whosoever may blaspheme against the Holy Ghost hath never forgiveness, but is subject of eternal condemnation. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
Because they were saying, He has an unclean spirit.
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
And His mother and His brothers come; and standing without, sent to Him, calling Him.
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
And the crowd was sitting round Him; and they say to Him, Behold thy mother and thy brothers without are seeking thee.
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
And He responding to them, says, Who is my mother and my brothers?
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
And looking round on His disciples sitting about Him in a circle, He says, Behold my mother and my brothers!
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
For whosoever may do the will of God, the same is my brother, and my sister, and my mother.

< Marko 3 >