< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
And he entered again into the synagogue, and there was a man there who had a withered hand.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
And they watched him whether he would heal on the sabbath days; that they might accuse him.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
And he said to the man who had the withered hand: Stand up in the midst.
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
And he saith to them: Is it lawful to do good on the sabbath days, or to do evil? to save life, or to destroy? But they held their peace.
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
And looking round about on them with anger, being grieved for the blindness of their hearts, he saith to the man: Stretch forth thy hand. And he stretched it forth: and his hand was restored unto him.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
And the Pharisees going out, immediately made a consultation with the Herodians against him, how they might destroy him.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
But Jesus retired with his disciples to the sea; and a great multitude followed him from Galilee and Judea,
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
And from Jerusalem, and from Idumea, and from beyond the Jordan. And they about Tyre and Sidon, a great multitude, hearing the things which he did, came to him.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
And he spoke to his disciples that a small ship should wait on him because of the multitude, lest they should throng him.
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
For he healed many, so that they pressed upon him for to touch him, as many as had evils.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
And the unclean spirits, when they saw him, fell down before him: and they cried, saying:
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
Thou art the Son of God. And he strictly charged them that they should not make him known.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
And going up into a mountain, he called unto him whom he would himself: and they came to him.
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
And he made that twelve should be with him, and that he might send them to preach.
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
And he gave them power to heal sicknesses, and to cast out devils.
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
And to Simon he gave the name Peter:
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
And James the son of Zebedee, and John the brother of James; and he named them Boanerges, which is, The sons of thunder:
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
And Andrew and Philip, and Bartholomew and Matthew, and Thomas and James of Alpheus, and Thaddeus, and Simon the Cananean:
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
And Judas Iscariot, who also betrayed him.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
And they come to a house, and the multitude cometh together again, so that they could not so much as eat bread.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
And when his friends had heard of it, they went out to lay hold on him. For they said: He is become mad.
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
And the scribes who were come down from Jerusalem, said: He hath Beelzebub, and by the prince of devils he casteth out devils.
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
And after he had called them together, he said to them in parables: How can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
And if a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand.
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
And if a house be divided against itself, that house cannot stand.
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
And if Satan be risen up against himself, he is divided, and cannot stand, but hath an end.
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
No man can enter into the house of a strong man and rob him of his goods, unless he first bind the strong man, and then shall he plunder his house.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
Amen I say to you, that all sins shall be forgiven unto the sons of men, and the blasphemies wherewith they shall blaspheme:
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
But he that shall blaspheme against the Holy Ghost, shall never have forgiveness, but shall be guilty of an everlasting sin. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
Because they said: He hath an unclean spirit.
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
And his mother and his brethren came; and standing without, sent unto him, calling him.
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
And the multitude sat about him; and they say to him: Behold thy mother and thy brethren without seek for thee.
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
And answering them, he said: Who is my mother and my brethren?
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
And looking round about on them who sat about him, he saith: Behold my mother and my brethren.
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
For whosoever shall do the will of God, he is my brother, and my sister, and mother.

< Marko 3 >