< Marko 2 >

1 Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
Po nekaj dneh je ponovno vstopil v Kafarnáum, in razglasilo se je, da je v hiši.
2 Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
In nemudoma so bili zbrani mnogi, toliko, da tam ni bilo več prostora, da jih sprejme, ne, niti pred vrati ne; in oznanjal jim je besedo.
3 Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
In prišli so k njemu in prinesli nekoga, bolnega zaradi paralize, ki je bil prenašan od štirih.
4 Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
Ko pa zaradi gneče niso mogli priti bliže k njemu, so odkrili streho, kjer je bil. In ko so jo predrli, so spustili posteljo, na kateri je ležal bolni zaradi paralize.
5 Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
Ko je Jezus videl njihovo vero, je rekel bolnemu zaradi paralize: »Sin, tvoji grehi so ti odpuščeni.«
6 Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
Toda bili so nekateri izmed pisarjev, ki so tam sedeli ter v svojih srcih razmišljali:
7 “Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
»Zakaj ta človek govori takšna bogokletja? Kdo lahko odpušča grehe razen Boga samega?«
8 Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
In takoj, ko je Jezus v svojem duhu zaznal, da so v sebi tako modrovali, jim je rekel: »Zakaj v svojih srcih razmišljate te besede?
9 Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
Ali je bolnemu zaradi paralize lažje reči: ›Tvoji grehi so ti odpuščeni‹ ali reči: ›Vstani in vzemi svojo posteljo ter hôdi?‹
10 Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
Toda da boste lahko vedeli, da ima Sin človekov na zemlji oblast odpuščati grehe, (reče bolnemu zaradi paralize)
11 “Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
pravim ti: ›Vstani in vzemi svojo posteljo ter pojdi svojo pot v svojo hišo.‹«
12 Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
In ta je takoj vstal, vzel posteljo ter pred njimi vsemi odšel, tako da so bili vsi osupli in slavili Boga, rekoč: »Nikoli tega nismo videli na tak način.«
13 Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
In ponovno je odšel naprej ob morski obali, in vsa množica je krenila k njemu in jih je učil.
14 Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
In ko je hodil mimo, je zagledal Levija, Alfejevega sina, ki je sedel pri kraju plačevanja davkov ter mu rekel: »Sledi mi.« In ta je vstal ter mu sledil.
15 Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
In pripetilo se je, ko je Jezus v njegovi hiši sedel pri obedu, da je tudi mnogo davkarjev in grešnikov sedelo skupaj z Jezusom in njegovimi učenci, kajti bilo jih je mnogo in so mu sledili.
16 Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
In ko so ga pisarji in farizeji videli jesti z davkarji in grešniki, so njegovim učencem rekli: »Kako to, da jé in pije z davkarji in grešniki?«
17 Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
Ko je Jezus to slišal, jim reče: »Tisti, ki so zdravi, nimajo nobene potrebe po zdravniku, temveč tisti, ki so bolni; nisem prišel klicat pravičnih, temveč grešnike h kesanju.«
18 Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
Janezovi učenci in učenci farizejev so se postili; in prišli so ter mu rekli: »Zakaj se Janezovi učenci in učenci farizejev postijo, tvoji učenci pa se ne postijo?«
19 Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
Jezus jim je rekel: »Ali se lahko otroci svatovske sobe postijo, dokler je z njimi ženin? Kolikor dolgo imajo s seboj ženina, se ne morejo postiti.
20 Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
Toda prišli bodo dnevi, ko bo ženin vzet proč od njih in tedaj, v tistih dneh, se bodo postili.
21 Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
Tudi nihče ne prišije koščka novega oblačila na staro obleko; sicer bo nov košček, ki jo je zapolnil, odvzel iz stare in nastane hujša raztrganina.
22 Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
In novega vina nihče ne vliva v stare mehove, sicer novo vino mehove razžene, vino pa se izlije in mehovi bodo poškodovani; temveč mora biti novo vino vlito v nove mehove.«
23 Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
In pripetilo se je, da je na šabatni dan šel skozi žitna polja; in njegovi učenci so med hojo začeli smukati žitno klasje.
24 Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
Farizeji so mu rekli: »Glej, zakaj delajo na šabatni dan to, kar ni zakonito?«
25 Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
Rekel jim je: »Ali niste nikoli brali, kaj je storil David, ko je imel potrebo in je bil lačen on in tisti, ki so bili z njim?
26 Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
Kako je v dneh vélikega duhovnika Abjatárja odšel v Božjo hišo in jedel hlebe navzočnosti, kar ni zakonito jesti [nikomur] razen duhovnikom in je dal tudi tem, ki so bili z njim?«
27 Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
In rekel jim je: »Šabat je bila narejena zaradi človeka, ne pa človek zaradi šabate,
28 Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”
zato je Sin človekov Gospod tudi [čez] šabat.«

< Marko 2 >