< Marko 2 >
1 Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
[Jesus and his disciples] returned to Capernaum [town]. A few days later, because it was {people} heard that Jesus was in [his] house,
2 Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
many people gathered there. As a result, [after the people filled the house], there was no longer space to stand [in the house or outside] around the doorway. Jesus preached [God’s] message to them.
3 Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
Some people came to the house bringing to Jesus a man who was paralyzed. He was carried by four men {Four men carried [him]} [on a sleeping pad].
4 Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
They were not able to bring the man to Jesus because there was a crowd there. So they [went up the steps to the flat roof and] removed [some of] the tiles [above] where Jesus was. Then, after they made a [big] hole in the roof, they lowered [by ropes] the sleeping pad on which the paralyzed man lay. They lowered [it through the hole, down in front of Jesus].
5 Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
After Jesus perceived that the men believed [that he could heal this man], he said to the paralyzed man, “My friend, [I] forgive your sins!”
6 Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
There were some men who taught [the Jewish] laws sitting there. They started thinking like this:
7 “Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
“(Who does this man think he is, talking like that/This man shouldn’t talk like that!) [RHQ]? (He is insulting God!/Does he think he is God?) [RHQ] (No person can forgive sins!/Who can forgive sins?) [RHQ] Only God can forgive sins!”
8 Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
Jesus sensed that they were deliberating like that within themselves. So he said to them, “(You should not question within yourselves [whether I have the right to forgive this man’s sins]!/Why do you question [whether I have the right to forgive this man’s sins]?) [RHQ]
9 Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
It is [not risky] [RHQ] for someone to tell the man who is paralyzed, ‘Your sins are forgiven {[I] forgive your sins},’ [because no one can prove that it has happened]. But no one would say to him, ‘Get up, pick up your stretcher, and then walk away’, [unless he really had the power to heal him, because people can easily see whether it happens or not].
10 Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
So I [will do something] in order that you may know that [God] has authorized me, the one who came from heaven, to forgive sins on earth [as well as to heal people].” Then he said to the paralyzed man,
11 “Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
“To you I say, ‘Get up! Pick up your sleeping pad! And then go home!’”
12 Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
The man stood up immediately! He picked up the sleeping pad, and then he went away, while all the people [there] were watching. They were all amazed, and they praised God and said, “We have never before seen anything like [what happened] just now!”
13 Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
Jesus left [Capernaum town again and walked with his disciples] alongside [Galilee] lake. A large crowd came to him. Then he taught them.
14 Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
As he walked on further, he saw a man named Levi, whose other name was Matthew, and whose father’s name was Alpheus. He was sitting in his office where he collected taxes [for the Roman government]. Jesus said to him, “Come with me [and become my disciple]!” So he got up and went with Jesus.
15 Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
[Later], Jesus was eating a meal in Levi’s house. Many men who collected taxes and [other] people who were [considered to be] sinning regularly were eating with Jesus and his disciples. [This was not surprising], for there were many people like this who were going [everywhere] with Jesus.
16 Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
The [men who taught the Jewish] laws [who were there] and who were members of the Pharisee [sect] saw that Jesus was eating with men who collected taxes and [others who were considered] {[whom they considered]} [to be] sinners. So they said to his disciples, “(It is disgusting that he eats with [such disgusting] men as those who collect taxes, and with [other] sinners!/Why is it that he eats with [such disgusting] men as those who collect taxes, and with [other] sinners?)” [RHQ]
17 Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
After Jesus heard [what they were saying], he said to the men who taught the [Jewish] laws, “People who [consider that they] are well do not seek a doctor. On the contrary, it is those who are sick [who seek a doctor] [MET]!” [This he said to indicate that it was those who knew that they had sinned who were coming to him in order that he might help them spiritually]. And he said, “I did not come to invite people [who think that] [IRO] they are righteous [to come to me and turn from their sinful behavior]. On the contrary, I came [from heaven to invite] people who [know that they] are sinners, [in order that they might turn from their sins and come to me].”
18 Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
The disciples of John [the Baptizer] and some men who belonged to the Pharisee [sect] used to abstain from food [to show that they wanted to please God]. One day, some people came [to Jesus] and asked him [critically], “The disciples of John and the Pharisees (fast/abstain from food) [from time to time], but your disciples do not. [We think they should abstain from food also. What do you say about that] [RHQ]?”
19 Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
[Jesus wanted them to understand that it was not appropriate for his disciples to show sorrow by abstaining from food while he was still with them]. So he said to them, “When a man is marrying a woman, his friends will certainly not abstain from food while he is still with them, will they [RHQ]? No. During the time that he is with them, they will not abstain from food [because they are happy together].
20 Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
But some day, he will be taken away {his [enemies] will take him away} from them. Then, in those days, they will abstain from food, [because they will be sad].”
21 Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
[Jesus wanted to show that those who desire to live in accordance with his new message should not try to continue to obey the old religious traditions like fasting. So he also said to them], “People do not sew a patch of unshrunken cloth on an old garment [in order to mend a hole]. If they did that, [when they washed the garment, the patch would shrink] and the new [piece of cloth] would tear off more of the old cloth. As a result, the hole would become bigger!
22 Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
[Similarly], people do not put newly [squeezed] grape juice into old skin bags [to store it]. If they did that, that juice will burst the skin bags [because they would not stretch when the wine ferments and expands]. As a result both the wine and the skin bags would be ruined! On the contrary, people must put new wine into new skin bags!” [MET]
23 Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
On one (Sabbath/Jewish day of rest) Jesus was walking through some grain fields with his disciples. As they were walking along [through the grain fields], the disciples were plucking some of the heads of grain. [They rubbed them in their hands to remove the chaff, and were eating the grain. The laws of Moses permitted people to do that if they were hungry].
24 Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
[Some of] the Pharisees [saw them doing what they considered to be work. So they] said to him, “Look! (They should not be doing on our (Sabbath day/day of rest) [work] that our laws forbid!/Why are they doing on our (Sabbath day/day of rest) [work] that our laws forbid?) [RHQ]”
25 Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
[Jesus wanted to show them that the record in the Scriptures indicated that God permitted people to disobey certain religious laws when they needed food]. So he said to them, “[It is written in the Scriptures] what [our revered ancestor, King] David, did when he needed food, and both he and the men with him were hungry. You have read about that, but ([you do not think about what it implies./why do you not think about what it implies]?) [RHQ]
26 Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
During the time Abiathar was high priest, David entered the big tent [where people worshipped] God [and asked for some bread. The high priest gave him some] of the loaves of bread. That bread was the bread he had presented to God. It was permitted in one of Moses’ laws that only the priests could eat that bread! But David ate some of it. Then he also gave some of it to the men who were with him. [But God did not consider that was wrong!]”
27 Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
Jesus said to them further, “[God] established (the day of rest/the Sabbath day) [to help] people! He did not create people to [obey rules about] (the Sabbath/the day of rest)!
28 Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”
And [think about this]: I am the one who came from heaven. So I have the authority [to determine what is right for my disciples to do] (on the Sabbath/on the Jewish rest day)!”