< Marko 2 >
1 Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
A few days later Jesus went to Capernaum again, and the people heard that he was at home.
2 Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
Immediately many were gathered together, so that there was no longer any room, not even at the door, and he was speaking the word to them.
3 Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
Then some people came to him, bringing a paralytic carried by four men.
4 Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
Since they were not able to come near Jesus because of the crowd, they uncovered the roof where he was. After digging through it, they let down the mat on which the paralytic was lying.
5 Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
When Jesus saw their faith, he said to the paralytic, “Son, yoʋr sins are forgiven yoʋ.”
6 Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
Now some of the scribes were sitting there and questioning in their hearts:
7 “Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
“Why does this man speak such blasphemies? Who can forgive sins but God alone?”
8 Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
Immediately Jesus knew in his spirit that they were discussing these questions among themselves, so he said to them, “Why are you questioning these things in your hearts?
9 Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
Which is easier, to say to the paralytic, ‘Yoʋr sins are forgiven,’ or to say, ‘Rise, take up yoʋr mat, and walk’?
10 Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
But so that you may know that the Son of Man has authority on earth to forgive sins”—he said to the paralytic—
11 “Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
“I say to yoʋ, rise, pick up yoʋr mat, and go to yoʋr house.”
12 Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
So the man immediately rose, picked up his mat, and went out in front of them all, so that they were all amazed and began glorifying God, saying, “We have never seen anything like this!”
13 Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
Once again Jesus went out by the sea. The entire crowd came to him, and he taught them.
14 Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
As he was walking along, he saw Levi the son of Alphaeus sitting at the tax booth. Jesus said to him, “Follow me,” so Levi rose and followed him.
15 Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
Later, as Jesus was reclining at the table in Levi's house, many tax collectors and sinners reclined with him and his disciples, for there were many who followed him.
16 Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
When the scribes and the Pharisees saw Jesus eating with tax collectors and sinners, they said to his disciples, “Why is he eating and drinking with tax collectors and sinners?”
17 Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
When Jesus heard this, he said to them, “It is not the healthy who need a physician, but the sick. I did not come to call the righteous, but sinners to repentance.”
18 Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
Now the disciples of John and the disciples of the Pharisees were fasting. So some people came and said to Jesus, “Why is it that the disciples of John and the disciples of the Pharisees fast, but yoʋr disciples do not fast?”
19 Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
Jesus said to them, “Can the bridegroom's attendants fast while the bridegroom is with them? As long as they have the bridegroom with them they cannot fast.
20 Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
But the days are coming when the bridegroom will be taken away from them, and then they will fast in those days.
21 Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
“No one sews a piece of unshrunk cloth on an old garment. For the garment's new patch would pull away from the old cloth, and a worse tear would be made.
22 Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
And no one puts new wine into old wineskins. For the new wine would burst the wineskins; the wine would be spilled, and the wineskins would be ruined. But new wine must be put into new wineskins.”
23 Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
On the Sabbath Jesus was going through the grainfields, and his disciples began to make their way, plucking heads of grain.
24 Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
So the Pharisees said to him, “Behold, why are they doing what is not lawful to do on the Sabbath?”
25 Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
He said to them, “Have you never read what David did when he had need and was hungry, he and those who were with him,
26 Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
how he entered the house of God, in the time of Abiathar the high priest, and ate the bread of the Presence, which is not lawful for anyone to eat except for the priests, and how he also gave it to those who were with him?”
27 Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
Then he said to them, “The Sabbath was made for man, not man for the Sabbath.
28 Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”
So the Son of Man is Lord even of the Sabbath.”