< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu baada ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na waandishi walikuwa wakitafuta namna ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
After two days was the feast of the passover, and of unleavened bread: and the chief priests and the scribes sought how they might take him by craft, and put him to death.
2 Kwa kuwa walisema, “Sio wakati huu wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
But they said, Not on the feast day, lest there be an uproar of the people.
3 Wakati Yesu alipokuwa Bethania nyumbani kwa Simoni mkoma, na alipokuwa akielekea mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa na chupa ya marashi ya nardo safi yenye gharama kubwa sana, aliivunja chupa na kuimimina juu ya kichwa chake.
And being in Bethany in the house of Simon the leper, as he sat at meat, there came a woman having an alabaster box of ointment of spikenard very precious; and she broke the box, and poured it on his head.
4 Lakini kulikuwa na baadhi yao waliokasirika. Waliambiana wao kwa wao wakisema, “Ni nini sababu ya upotevu huu?
And there were some that had indignation within themselves, and said, Why was this waste of the ointment made?
5 Manukato haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari mia tatu, na wakapewa maskini.” Nao walimkemea.
For it might have been sold for more than three hundred pence, and have been given to the poor. And they murmured against her.
6 Lakini Yesu alisema, “Mwacheni peke yake. Kwa nini mnamsumbua? Amefanya jambo zuri kwangu.
And Jesus said, Let her alone; why trouble you her? she has worked a good work on me.
7 Siku zote maskini mnao, na wakati wowote mnapotamani mnaweza kufanya mazuri kwao, lakini hamtakuwa nami wakati wote.
For you have the poor with you always, and whenever you will you may do them good: but me you have not always.
8 Amefanya kile anachoweza: ameupaka mwili wangu mafuta kwa ajili ya maziko.
She has done what she could: she is come beforehand to anoint my body to the burying.
9 Kweli nawaambia, kila mahali injili inapohubiriwa katika ulimwengu wote, kile alichofanya mwanamke huyu kitazungumzwa kwa ukumbusho wake.
Truly I say to you, Wherever this gospel shall be preached throughout the whole world, this also that she has done shall be spoken of for a memorial of her.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale kumi na wawili, alikwenda kwa wakuu wa makuhani ili kwamba apate kumkabidhi kwao.
And Judas Iscariot, one of the twelve, went to the chief priests, to betray him to them.
11 Wakati wakuu wa Makuhani waliposikia hivyo, walifurahi na wakaahidi kumpa fedha. Alianza kutafuta nafasi ya kumkabidhi kwao.
And when they heard it, they were glad, and promised to give him money. And he sought how he might conveniently betray him.
12 Katika siku ya kwanza ya mkate usiotiwa chachu, wakati walipotoa mwanakondoo wa pasaka, wanafunzi wake walimwambia, “Unataka twende wapi tukaandae ili upate kula mlo wa Pasaka?”
And the first day of unleavened bread, when they killed the passover, his disciples said to him, Where will you that we go and prepare that you may eat the passover?
13 Aliwatuma wanafuzi wake wawili na kuwaambia, “Nendeni mjini, na mwanamume ambaye amebeba mtungi ataonana nanyi. Mfuateni.
And he sends forth two of his disciples, and says to them, Go you into the city, and there shall meet you a man bearing a pitcher of water: follow him.
14 Nyumba atakayoingia, mfuateni na mmwambie mwenye nyumba hiyo, 'Mwalimu asema, “Kiko wapi chumba cha wageni mahali nitakapokula Pasaka na wanafunzi wangu?”
And wherever he shall go in, say you to the manager of the house, The Master says, Where is the guest room, where I shall eat the passover with my disciples?
15 Atawaonesha chumba cha juu kikubwa chenye samani ambacho kiko tayari. Fanyeni maandalizi kwa ajili yetu pale.”
And he will show you a large upper room furnished and prepared: there make ready for us.
16 Wanafunzi waliondoka wakaenda mjini; walikuta kila kitu kama alivyokuwa amewaambia, na wakaandaa mlo wa Pasaka.
And his disciples went forth, and came into the city, and found as he had said to them: and they made ready the passover.
17 Wakati ilipokuwa jioni, alikuja na wale Kumi na wawili.
And in the evening he comes with the twelve.
18 Na walipokuwa wakiikaribia meza na kula, Yesu alisema, “Kweli nawaambia, mmoja kati yenu anayekula pamoja nami atanisaliti.”
And as they sat and did eat, Jesus said, Truly I say to you, One of you which eats with me shall betray me.
19 Wote walisikitika, na mmoja baada ya mwingine walimwambia, “Hakika siyo mimi?”
And they began to be sorrowful, and to say to him one by one, Is it I? and another said, Is it I?
20 Yesu alijibu na kuwaambia, “Ni mmoja wa Kumi na wawili kati yenu, mmoja ambaye sasa anachovya tonge katika bakuli pamoja nami.
And he answered and said to them, It is one of the twelve, that dips with me in the dish.
21 Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakwenda kama vile maandiko yasemavyo juu yake. Lakini ole wake mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu atasalitiwa! Ingekuwa vizuri zaidi kwake kama mtu yule asingezaliwa.”
The Son of man indeed goes, as it is written of him: but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! good were it for that man if he had never been born.
22 Na walipokuwa wakila, Yesu alichukua mkate, akaubariki, na kuumega. Aliwapa akisema, “Chukueni. Huu ni mwili wangu.”
And as they did eat, Jesus took bread, and blessed, and broke it, and gave to them, and said, Take, eat: this is my body.
23 Alichukua kikombe, akashukuru, na akawapatia, na wote wakakinywea.
And he took the cup, and when he had given thanks, he gave it to them: and they all drank of it.
24 Aliwaambia, “Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi.
And he said to them, This is my blood of the new testament, which is shed for many.
25 Kweli nawaambia, sitakunywa tena katika zao hili la mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa mpya katika ufalme wa Mungu.”
Truly I say to you, I will drink no more of the fruit of the vine, until that day that I drink it new in the kingdom of God.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, walikwenda nje katika Mlima wa Mizeituni.
And when they had sung an hymn, they went out into the mount of Olives.
27 Yesu aliwaaambia, “Ninyi nyote mtajitenga mbali kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, 'Nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika.'
And Jesus says to them, All you shall be offended because of me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep shall be scattered.
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia mbele yenu Galilaya.”
But after that I am risen, I will go before you into Galilee.
29 Petro alimwambia, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
But Peter said to him, Although all shall be offended, yet will not I.
30 Yesu alimwambia, “Kweli nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utakuwa umenikana mara tatu.”
And Jesus says to him, Truly I say to you, That this day, even in this night, before the cock crow twice, you shall deny me thrice.
31 Lakini Petro alisema, “Hata itanilazimu kufa pamoja nawe, sitakukana.” Wote walitoa ahadi ile ile.
But he spoke the more vehemently, If I should die with you, I will not deny you in any wise. Likewise also said they all.
32 Walikuja kwenye eneo lililoitwa Gethsemane, na Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nasali.”
And they came to a place which was named Gethsemane: and he says to his disciples, Sit you here, while I shall pray.
33 Aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana pamoja naye, akaanza kuhuzunika na kutaabika sana.
And he takes with him Peter and James and John, and began to be sore amazed, and to be very heavy;
34 Aliwaambia, “Nafsi yangu ina huzuni sana, hata kufa. Bakini hapa na mkeshe.”
And says to them, My soul is exceeding sorrowful to death: tarry you here, and watch.
35 Yesu alienda mbele kidogo, akaanguka chini, akaomba, kama ingewezekana, kwamba saa hii ingemwepuka.
And he went forward a little, and fell on the ground, and prayed that, if it were possible, the hour might pass from him.
36 Alisema, “Aba, Baba, Mambo yote kwako yanawezekana. Niondolee kikombe hiki. Lakini siyo kwa mapenzi yangu, bali mapenzi yako.”
And he said, Abba, Father, all things are possible to you; take away this cup from me: nevertheless not what I will, but what you will.
37 Alirudi na kuwakuta wamelala, na akamwambia Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?
And he comes, and finds them sleeping, and says to Peter, Simon, sleep you? could not you watch one hour?
38 Kesheni na muombe kwamba msije mkaingia katika majaribu. Hakika roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Watch you and pray, lest you enter into temptation. The spirit truly is ready, but the flesh is weak.
39 Alienda tena na kuomba, na alitumia maneno yaleyale.
And again he went away, and prayed, and spoke the same words.
40 Alikuja tena akawakuta wamelala, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito na hawakujua nini cha kumwambia.
And when he returned, he found them asleep again, (for their eyes were heavy, ) neither knew they what to answer him.
41 Alikuja mara ya tatu na kuwaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Yatosha! Saa imefika. Tazama! Mwana wa Adamu atasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
And he comes the third time, and says to them, Sleep on now, and take your rest: it is enough, the hour is come; behold, the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
42 Amkeni, twendeni. Tazama, yule anayenisaliti yuko karibu.”
Rise up, let us go; see, he that betrays me is at hand.
43 Mara tu alipokuwa bado anaongea, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, alifika, na kundi kubwa kutoka kwa wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wenye mapanga na marungu.
And immediately, while he yet spoke, comes Judas, one of the twelve, and with him a great multitude with swords and staves, from the chief priests and the scribes and the elders.
44 Wakati huo msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema, Yule nitakayembusu, ndiye. Mkamateni na kumpeleka chini ya ulinzi.”
And he that betrayed him had given them a token, saying, Whomsoever I shall kiss, that same is he; take him, and lead him away safely.
45 Wakati Yuda alipofika, moja kwa moja alienda kwa Yesu na kusema, “Mwalimu!” Na akambusu.
And as soon as he was come, he goes straightway to him, and says, Master, master; and kissed him.
46 Kisha wakumtia chini ya ulinzi na kumkamata.
And they laid their hands on him, and took him.
47 Lakini mmoja kati yao aliyesimama karibu naye alichomoa upanga wake akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata sikio.
And one of them that stood by drew a sword, and smote a servant of the high priest, and cut off his ear.
48 Yesu aliwaambia, “Mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama mnyang'anyi?
And Jesus answered and said to them, Are you come out, as against a thief, with swords and with staves to take me?
49 Wakati kila siku nilikuwa nanyi na nikifundisha hekaluni, hamkunikamata. Lakini hili limefanyika ili maandiko yatimie.
I was daily with you in the temple teaching, and you took me not: but the scriptures must be fulfilled.
50 Na wale wote waliokuwa na Yesu walimwacha na kukimbia.
And they all forsook him, and fled.
51 Kijana mmoja alimfuata, aliyekuwa amevaa shuka tu aliyokuwa amejifunika kumzunguka; walimkamata lakini
And there followed him a certain young man, having a linen cloth cast about his naked body; and the young men laid hold on him:
52 aliwaponyoka akaiacha shuka pale akakimbia uchi.
And he left the linen cloth, and fled from them naked.
53 Walimwongoza Yesu kwa kuhani mkuu. Pale walikusanyika pamoja naye makuhani wakuu wote, wazee, na waandishi.
And they led Jesus away to the high priest: and with him were assembled all the chief priests and the elders and the scribes.
54 Petro naye alimfuata Yesu kwa mbali, kuelekea kwenye ua wa kuhani mkuu. Aliketi pamoja na walinzi, waliokuwa karibu na moto wakiota ili kupata joto.
And Peter followed him afar off, even into the palace of the high priest: and he sat with the servants, and warmed himself at the fire.
55 Wakati huo makuhani wakuu wote na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumwua. Lakini hawakuupata.
And the chief priests and all the council sought for witness against Jesus to put him to death; and found none.
56 Kwa kuwa watu wengi walileta ushuhuda wa uongo dhidi yake, lakini hata ushahidi wao haukufanana.
For many bore false witness against him, but their witness agreed not together.
57 Baadhi walisimama na kuleta ushahidi wa uongo dhidi yake; wakisema,
And there arose certain, and bore false witness against him, saying,
58 “Tulimsikia akisema, 'Nitaliharibu hekalu hili lililotengenezwa kwa mikono, na ndani siku tatu nitajenga lingine lisilotengenezwa kwa mikono.'”
We heard him say, I will destroy this temple that is made with hands, and within three days I will build another made without hands.
59 Lakini hata ushahidi wao haukufanana.
But neither so did their witness agree together.
60 Kuhani mkuu alisimama katikati yao na akamwuliza Yesu, “Je, huna jibu? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
And the high priest stood up in the middle, and asked Jesus, saying, Answer you nothing? what is it which these witness against you?
61 Lakini alikaa kimya na hakujibu chochote. Mara Kuhani mkuu alimwuliza tena, “Je wewe ni Kristo, mwana wa Mbarikiwa?”
But he held his peace, and answered nothing. Again the high priest asked him, and said to him, Are you the Christ, the Son of the Blessed?
62 Yesu alisema, “Mimi ndiye. Na utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wa nguvu akija na mawingu ya mbinguni.”
And Jesus said, I am: and you shall see the Son of man sitting on the right hand of power, and coming in the clouds of heaven.
63 Kuhani mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Je, bado tunahitaji mashahidi?
Then the high priest rent his clothes, and says, What need we any further witnesses?
64 Mmesikia kufuru. Uamuzi wenu ni upi?” Na wote walimhukumu kama mmoja aliyestahili kifo.
You have heard the blasphemy: what think you? And they all condemned him to be guilty of death.
65 Baadhi wakaanza kumtemea mate na kumfunika uso na kumpiga na kumwambia, “Tabiri!” Maafisa walimchukua na kumpiga.
And some began to spit on him, and to cover his face, and to buffet him, and to say to him, Prophesy: and the servants did strike him with the palms of their hands.
66 Na Petro alipokuwa bado yuko chini uani, mtumishi mmoja wa wasichana wa kuhani mkuu alikuja kwake.
And as Peter was beneath in the palace, there comes one of the maids of the high priest:
67 Alimwona Petro alipokuwa amesimama akiota moto, na alimtazama kwa kumkaribia. Kisha alisema, “Nawe pia ulikuwa na Mnazareti, Yesu”.
And when she saw Peter warming himself, she looked on him, and said, And you also were with Jesus of Nazareth.
68 Lakini alikataa, akisema, “Sijui wala sielewi kuhusu kile unachosema!” Kisha alitoka akaenda nje uani. (Zingatia; Mstari huu, “Na jogoo akawika” haumo kwenye nakala za kale).
But he denied, saying, I know not, neither understand I what you say. And he went out into the porch; and the cock crew.
69 Lakini mtumishi wa kike pale, alimwona na alianza kuwaambia tena wale ambao walikuwa wamesimama pale, “Mtu huyu ni mmoja wao!”
And a maid saw him again, and began to say to them that stood by, This is one of them.
70 Lakini alikana tena. Baadaye kidogo wale waliokuwa wamesimama pale walikuwa wakimwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya.”
And he denied it again. And a little after, they that stood by said again to Peter, Surely you are one of them: for you are a Galilaean, and your speech agrees thereto.
71 Lakini alianza kujiweka mwenyewe chini ya laana na kuapa, “Simjui mtu huyu mnayemsema.”
But he began to curse and to swear, saying, I know not this man of whom you speak.
72 Kisha jogoo aliwika mara ya pili. Kisha Petro alikumbuka maneno ambayo Yesu aliyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Na alianguka chini na kulia.
And the second time the cock crew. And Peter called to mind the word that Jesus said to him, Before the cock crow twice, you shall deny me thrice. And when he thought thereon, he wept.

< Marko 14 >