< Marko 11 >

1 Wakati huo walipokuja Yerusalemu, walipokaribia Besthfage na Bethania, katika Mlima wa Mizeituni, Yesu aliwatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake
Et comme ils approchaient de Jérusalem, étant près de Bethphagé, et de Béthanie, vers le mont des oliviers, il envoya deux de ses Disciples,
2 na aliwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachokabiliana nasi. Mara mtakapoingia humo, mtamkuta mwanapunda ambaye hajapandwa. Mfungueni na mmlete kwangu.
Et il leur dit: allez-vous-en à cette bourgade qui est vis-à-vis de vous; et en y entrant, vous trouverez un ânon attaché, sur lequel jamais homme ne s'assit; détachez-le, et l'amenez.
3 Na kama yeyote akiwaambia, 'Kwa nini mnafanya hivi'?, mnapaswa kusema, 'Bwana anamhitaji na mara atamrudisha hapa'.”
Et si quelqu'un vous dit: pourquoi faites-vous cela? dites que le Seigneur en a besoin; et d'abord il l'enverra ici.
4 Walikwenda na kumkuta mwanapunda amefungwa nje mlangoni kwenye mtaa ulio wazi, nao walimfungua.
Ils partirent donc, et trouvèrent l'ânon qui était attaché dehors, auprès de la porte, entre deux chemins, et ils le détachèrent.
5 Na baadhi ya watu walikuwa wamesimama pale na waliwaambia, “Mnafanya nini, kumfungua mwanapunda huyo?”
Et quelques-uns de ceux qui étaient là, leur dirent: pourquoi détachez-vous cet ânon?
6 Waliwaambia kama Yesu alivyowaambia, na watu wakawaacha waende.
Et ils leur répondirent comme Jésus avait commandé; et on les laissa faire.
7 Wanafunzi wawili walimleta mwanapunda kwa Yesu na walitandika mavazi yao juu yake ili Yesu aweze kumpanda.
Ils amenèrent donc l'ânon à Jésus, et mirent leurs vêtements sur l'ânon, et il s'assit dessus.
8 Watu wengi wakatandika mavazi yao barabarani, na wengine wakatandika matawi waliyoyakata kutoka mashambani.
Et plusieurs étendaient leurs vêtements par le chemin, et d'autres coupaient des rameaux des arbres, et les répandaient par le chemin.
9 Wale waliokwenda mbele yake na wale waliomfuata walipiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa anayekuja kwa jina la Bwana.
Et ceux qui allaient devant, et ceux qui suivaient, criaient, disant: Hosanna! Béni soit celui qui vient au Nom du Seigneur!
10 Ubarikiwe ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi! Hosana kwa aliye juu”
Béni soit le règne de David notre père, [le règne] qui vient au Nom du Seigneur; Hosanna dans les lieux très-hauts!
11 Ndipo Yesu aliingia Yerusalemu na alikwenda hekaluni na alitazama kila kitu. Sasa, wakati ulikuwa umeenda, alikwenda Bethania pamoja nao kumi na wawili.
Jésus entra ainsi dans Jérusalem, et au Temple, et après avoir regardé de tous côtés, comme il était déjà tard, il sortit pour aller à Béthanie avec les douze.
12 Siku iliyofuata, wakati walipokuwa wakirudi kutoka Bethania, alikuwa na njaa.
Et le lendemain en revenant de Béthanie, il eut faim.
13 Na akaona mti wa mtini uliokuwa na majani kwa mbali, alikwenda kutazama kama angeweza kupata chochote juu yake. Na wakati alipokwenda kwa huo, hakupata chochote isipokuwa majani, kwa kuwa haikuwa majira ya mtini.
Et voyant de loin un figuier qui avait des feuilles, il alla voir s'il y trouverait quelque chose, mais y étant venu, il n'y trouva rien que des feuilles; car ce n'était pas la saison des figues.
14 Aliuambia, “Hakuna yeyote atakayekula tunda kutoka kwako tena”. Na wanafunzi wake wakasikia. (aiōn g165)
Et Jésus prenant la parole dit au figuier: que jamais personne ne mange de fruit de toi. Et ses Disciples l'entendirent. (aiōn g165)
15 Walikuja Yerusalemu, naye aliingia hekaluni na kuanza kuwatoa nje wauzaji na wanunuzi ndani ya hekalu. Alizipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
Ils vinrent donc à Jérusalem, et quand Jésus fut entré au Temple, il se mit à chasser dehors ceux qui vendaient, et ceux qui achetaient dans le Temple, et il renversa les tables des changeurs, et les sièges de ceux qui vendaient des pigeons.
16 Hakumruhusu yeyote kubeba chochote hekaluni kilichoweza kuuzwa.
Et il ne permettait point que personne portât aucun vaisseau par le Temple.
17 Aliwafundisha na akasema, “Je haikuandikwa, 'nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote'? Lakini mmeifanya pango la wanyang'anyi”.
Et il les enseignait, en leur disant: n'est-il pas écrit? ma Maison sera appelée une Maison de prière par toutes les nations; mais vous en avez fait une caverne de voleurs.
18 Makuhani wakuu na waandishi walisikia alivyokuwa amesema, nao walitafuta njia ya kumwua. Hata hivyo walimwogopa kwa sababu umati ulishangazwa na mafundisho yake.
Ce que les Scribes et les principaux Sacrificateurs ayant entendu, ils cherchaient comment ils feraient pour le perdre; car ils le craignaient, à cause que tout le peuple avait de l'admiration pour sa doctrine.
19 Na kila wakati jioni ilipofika, waliondoka mjini.
Et le soir étant venu il sortit de la ville.
20 Walipokuwa wakitembea asubuhi, waliuona mti wa mtini umekauka mpaka kwenye mizizi yake.
Et le matin comme ils passaient auprès du figuier, ils virent qu'il était devenu sec jusqu'à la racine.
21 Petro alikumbuka na kusema, “Rabi! Tazama, mti wa mtini ulioulaani umekauka”.
Et Pierre s'étant souvenu [de ce qui s'était passé], dit à Jésus: Maître, voici, le figuier que tu as maudit, est tout sec.
22 Yesu aliwajibu, “Muwe na imani katika Mungu.
Et Jésus répondant, leur dit: croyez en Dieu.
23 Amini nawaambia kwamba kila auambiaye mlima huu, 'Ondoka, na ukajitupe mwenyewe baharini, 'na kama hana mashaka moyoni mwake lakini anaamini kwamba alichokisema kitatokea, hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya.
Car en vérité je vous dis, que quiconque dira à cette montagne: quitte ta place, et te jette dans la mer, et qui ne chancellera point en son cœur, mais croira que ce qu'il dit se fera, tout ce qu'il aura dit lui sera fait.
24 Kwa hiyo ninawaambia: kila kitu muombacho na kuuliza kwa ajili yake, aminini kwamba mmepokea, navyo vitakuwa vyenu.
C'est pourquoi je vous dis: tout ce que vous demanderez en priant, croyez que vous le recevrez, et il vous sera fait.
25 Wakati mnaposimama na kuomba, mnapaswa kusamehe chochote mlichonacho dhidi ya yeyote, ili kwamba Baba yenu aliye mbinguni awasamehe pia ninyi makosa yenu.
Mais quand vous vous présenterez pour faire votre prière, si vous avez quelque chose contre quelqu'un, pardonnez-lui, afin que votre Père qui est aux cieux vous pardonne aussi vos fautes.
26 (Zingatia: Mstari huu, “Lakini msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatasamehe dhambi zenu” haumo kwenye nakala za kale).
Mais si vous ne pardonnez point, votre Père qui est aux cieux ne vous pardonnera point aussi vos fautes.
27 Walikuja Yerusalemu tena. Na Yesu alipokuwa akitembea hekaluni, makuhani wakuu, waandishi na wazee walikuja kwake.
Ils retournèrent encore à Jérusalem, et comme il marchait dans le Temple, les principaux Sacrificateurs, et les Scribes, et les Anciens vinrent à lui,
28 Walimwambia, “Kwa mamlaka gani unafanya mambo haya?” Na ni nani aliyekupa mamlaka kuyafanya haya?”
Et lui dirent: par quelle autorité fais-tu ces choses, et qui est celui qui t'a donné cette autorité, pour faire les choses que tu fais?
29 Yesu aliwaambia, “Nitawauliza swali moja. Niambieni na mimi nitawaambia kwa mamlaka gani ninayafanya mambo haya.
Et Jésus répondant leur dit: je vous interrogerai aussi d'une chose, et répondez-moi; puis je vous dirai par quelle autorité je fais ces choses.
30 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au ulitoka kwa wanadamu? Nijibuni.”
Le Baptême de Jean était-il du ciel, ou des hommes? répondez-moi.
31 Walijadiliana miongoni mwao na kushindana na kusema, “Kama tukisema, 'Kutoka mbinguni,' atasema, 'Kwa nini basi hamkumwamini?'
Et ils raisonnaient entre eux, disant: si nous disons, du ciel: il nous dira: pourquoi donc ne l'avez-vous point cru?
32 Lakini kama tukisema, 'Kutoka kwa wanadamu,'...” Waliwaogopa watu, kwa kuwa wote walishikilia kwamba Yohana alikuwa Nabii.
Et si nous disons: des hommes, nous avons à craindre le peuple; car tous croyaient que Jean avait été un vrai Prophète.
33 Ndipo walimjibu Yesu na kusema, “Hatujui. Ndipo Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nayafanya mambo haya.
Alors pour réponse ils dirent à Jésus: nous ne savons. Et Jésus répondant leur dit: Je ne vous dirai point aussi par quelle autorité je fais ces choses.

< Marko 11 >