< Marko 10 >
1 Yesu aliondoka eneo hilo na akaenda katika mkoa wa Uyahudi na eneo la mbele ya Mto Yorodani, na makutano walimfuata tena. Aliwafundisha tena, kama ilivyokuwa kawaida yake kufanya.
On leaving that place, Jesus went into the district of Judea on the other side of the Jordan. Crowds gathered about him again; and again, as usual, he began teaching them.
2 Na Mafarisayo walikuja kumjaribu na wakamuuliza, “Ni halali kwa mwanamume kuachana na mke wake?”
Presently some Pharisees came up and, to test him, asked, “Has a husband the right to divorce his wife?”
3 Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuru nini?”
“What direction did Moses give you?” replied Jesus.
4 Wakasema, “Musa aliruhusu kuandika cheti cha kuachana na kisha kumfukuza mwanamke.”
“Moses,” they said, “permitted a man to draw up in writing a notice of separation and divorce his wife.”
5 “Ni kwa sababu ya mioyo yenu migumu ndiyo maana aliwaandikia sheria hii,” Yesu aliwaambia.
“It was owing to the hardness of your hearts,” said Jesus, “that Moses gave you this direction;
6 “Lakini kutoka mwanzo wa uumbaji, 'Mungu aliwaumba mwanamume na mwanamke.'
but, at the beginning of the Creation, ‘God made them male and female.’
7 Kwa sababu hii mwanamume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake,
‘For this reason a man will leave his father and mother,
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; Kwa kuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
and the man and his wife will become one;’ so that they are no longer two, but one.
9 Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
What God himself, then, has yoked together no one must separate.”
10 Walipokuwa ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza tena kuhusu hili.
When they were indoors, the disciples asked him again about this,
11 Akawaambia, “Yeyote amwachaye mke wake na kumwoa mwanamke mwingine, anafanya uzinzi dhidi yake.
and he said, “Anyone who divorces his wife and marries another woman is guilty of adultery against his wife;
12 Mwanamke naye akimwacha mme wake na kuolewa na mwanamme mwingine, anafanya uzinzi.”
and, if the woman divorces her husband and marries another man, she is guilty of adultery.”
13 Nao walimletea watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
Some of the people were bringing little children to Jesus, for him to touch them; but the disciples rebuked those who had brought them.
14 Lakini Yesu alipotambua hilo, hakufurahishwa nalo kabisa akawaambia, “Waruhusuni watoto wadogo waje kwangu, na msiwazuie, kwa sababu walio kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
When, however, Jesus saw this, he was indignant. “Let the little children come to me,” he said, “do not hinder them; for it is to the childlike that the kingdom of God belongs.
15 Ukweli nawaambia, yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hakika hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
I tell you, unless a person receives the kingdom of God like a child, they will not enter it at all.”
16 Kisha akawachukua watoto mikononi mwake na akawabariki akiwawekea mikono yake juu yao.
Then he embraced the children, and, placing his hands on them, gave them his blessing.
17 Na alipoanza safari yake mtu mmoja alimkimbilia na akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niweze kurithi uzima ya milele?” (aiōnios )
As Jesus was resuming his journey, a man came running up to him, and threw himself on his knees before him. “Good teacher,” he asked, “what must I do to gain eternal life?” (aiōnios )
18 Na Yesu akasema, “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa Mungu peke yake.
“Why do you call me good?” answered Jesus. “No one is good but God.
19 Unazijua amri: 'Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, mheshimu baba na mama yako'.”
You know the commandments – ‘Do not kill. Do not commit adultery. Do not steal. Do not say what is false about others. Do not cheat. Honor your father and your mother.’”
20 Mtu yule akasema, “Mwalimu, haya yote nimeyatii tangu nikiwa kijana.”
“Teacher,” he replied, “I have observed all these from my childhood.”
21 Yesu alimwangalia na kumpenda. Akawambia, “Unapungukiwa kitu kimoja. Unapaswa kuuza vyote ulivyo navyo na uwape masikini, na utakuwa na hazina mbinguni. Ndipo uje unifuate.”
Jesus looked at the man, and his heart went out to him, and he said, “There is still one thing wanting in you; go and sell all that you have, and give to the poor, and you will have wealth in heaven; then come and follow me.”
22 Lakini alikata tamaa kwa sababu ya maelezo haya; aliondoka akiwa mwenye huzuni, kwa kuwa alikuwa na mali nyingi.
But the man’s face clouded at these words, and he went away distressed, for he had great possessions.
23 Yesu akatazama pande zote na kuwaambia wanafunzi wake, “Ni jinsi gani ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu!
Then Jesus looked around, and said to his disciples, “How hard it will be for people of wealth to enter the kingdom of God!”
24 Wanafunzi walishangazwa kwa maneno haya. Lakini Yesu akawaambia tena, “Watoto, ni jinsi gani ilivyo vigumu kuingia katika ufalme wa Mungu!
The disciples were amazed at his words. But Jesus said again, “My children, how hard a thing it is to enter the kingdom of God!
25 Ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano, kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to get through a needle’s eye, than for a rich person to enter the kingdom of God.”
26 Walishangazwa sana na wakasemezana, “Hivyo nani ataokoka”
“Then who can be saved?” they exclaimed in the greatest astonishment.
27 Yesu akawaangalia na kusema, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini sio kwa Mungu. Kwa kuwa katika Mungu yote yanawezekana.”
Jesus looked at them, and answered, “With people it is impossible, but not with God; for everything is possible with God.”
28 “Petro akaanza kuzungumza naye, “Angalia tumeacha vyote na tumekufuata.”
“But we,” began Peter, “we left everything and have followed you.”
29 Yesu akasema, “Ukweli nawaambia ninyi, hakuna aliyeacha nyumba, au kaka, au dada, au mama, au baba, au watoto, au ardhi, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
“I tell you,” said Jesus, “there is no one who has left house, or brothers, or sisters, or mother, or father, or children, or land, for my sake and for the good news,
30 ambaye hatapokea mara mia zaidi ya sasa hapa duniani: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, na ardhi, kwa mateso, na ulimwengu ujao, uzima wa milele. (aiōn , aiōnios )
who will not receive a hundred times as much, even now in the present – houses, and brothers, and sisters, and mothers, and children, and land, though not without persecutions – and in the age that is coming, eternal life. (aiōn , aiōnios )
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many who are first now will then be last, and the last will be first.”
32 Walipokuwa njiani, kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa amewatangulia mbele yao. Wanafunzi walishangaa, na wale waliokuwa wanafuata nyuma waliogopa. Ndipo Yesu akawatoa pembeni tena wale kumi na wawili na akaanza kuwaambia ambacho kitamtokea hivi karibuni:
They were on the road going up to Jerusalem, with Jesus walking in front of them. The disciples were filled with awe, while those who were following behind were overwhelmed with fear. Gathering the Twelve around him once more, Jesus began to tell them what was about to happen to him.
33 “Tazama, tunakwenda mpaka Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atafikishwa kwa makuhani wakuu na waandishi. Watamhukumu afe na watamtoa kwa watu wa Mataifa.
“Listen!” he said. “We are going up to Jerusalem; and there the Son of Man will be betrayed to the chief priests and the teachers of the Law, and they will condemn him to death, and they will give him up to the Gentiles,
34 Watamdhihaki, watamtemea mate, watampiga fimbo, na watamwua. Lakini baada ya siku tatu atafufuka.”
who will mock him, spit on him, and scourge him, and put him to death; and after three days he will rise again.”
35 Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walikuja kwake na kusema, “Mwalimu, tunakuhitaji utufanyie chochote tukuombacho.”
James and John, the two sons of Zebedee, went to Jesus, and said, “Teacher, we want you to do for us whatever we ask.”
36 Aliwaambia, “Mnataka niwatendee nini?”
“What do you want me to do for you?” he asked.
37 Wakasema, “Turuhusu tukae nawe katika utukufu wako, mmoja katika mkono wako wa kuume na mwingine mkono wako wa kushoto.”
“Grant us this,” they answered, “to sit, one on your right, and the other on your left, when you come in glory.”
38 Lakini Yesu aliwajibu, “Hamjui mnachoomba. Mnaweza kukinywea kikombe ambacho nitakiywea au kustahimili ubatizo ambao nitabatizwa?”
“You do not know what you are asking,” Jesus said to them. “Can you drink the cup that I am to drink? Or receive the baptism that I am to receive?”
39 Wakamwambia, “Tunaweza” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokinywea, mtakinywea. Na ubatizo ambao kwao nimebatizwa, mtaustahimili.
“Yes,” they answered, “we can.” “You will indeed drink the cup that I am to drink,” Jesus said, “and receive the baptism that I am to receive,
40 Lakini atakayekaa mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto sio mimi wa kutoa, lakini ni kwa wale ambao kwao imekwisha andaliwa.”
but as to a seat at my right or at my left – that is not mine to give, but it is for those for whom it has been prepared.”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
On hearing of this, the ten others were at first very indignant about James and John.
42 Yesu akawaita kwake na kusema, “Mnajua kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala, na watu wao mashuhuri huwaonyesha mamlaka juu yao.”
But Jesus called the ten to him, and said, “Those who are regarded as ruling among the Gentiles lord it over them, as you know, and their great men oppress them.
43 Lakini haipaswi kuwa hivi kati yenu. Yeyote atakaye kuwa mkubwa kati yenu lazima awatumikie,
But among you it is not so. No, whoever wants to become great among you must be your servant,
44 na yeyote atakaye kuwa wa kwanza kati yenu ni lazima awe mtumwa wa wote.
and whoever wants to take the first place among you must be the servant of all;
45 Kwa kuwa Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa bali kutumika, na kuyatoa maisha yake kuwa fidia kwa wengi.”
for even the Son of Man came, not be served, but to serve, and to give his life as a ransom for many.”
46 Wakaja Yeriko. Alipokuwa akiondoka Yeriko na wanafunzi wake na kundi kubwa, mwana wa Timayo, Batimayo, kipofu mwombaji, alikaa kando ya barabara.
They came to Jericho. When Jesus was going out of the town with his disciples and a large crowd, Bartimaeus, the son of Timaeus, a blind beggar, was sitting by the roadside.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu Mnazareti, alianza kupiga kelele na kusema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Hearing that it was Jesus the Nazarene, he began to call out, “Jesus, Son of David, take pity on me.”
48 Wengi walimkemea yule kipofu, wakimwambia anyamaze. Lakini alilia kwa sauti zaidi, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Many of the people kept telling him to be quiet; but the man continued to call out all the louder, “Son of David, take pity on me.”
49 Yesu alisimama na kuamuru aitwe. Walimwita yule kipofu, wakisema, “Kuwa shujaa! Inuka! Yesu anakuita.”
Then Jesus stopped. “Call him,” he said. So they called the blind man. “Have courage!” they exclaimed. “Get up; he is calling you.”
50 Akalitupa pembeni koti lake, akakimbia zaidi, na kuja kwa Yesu.
The man threw off his cloak, sprang up, and came to Jesus.
51 Yesu akamjibu na kusema, “Unataka nikufanyie nini?” Yule mwanaume kipofu akamjibu, “Mwalimu, ninataka kuona.”
“What do you want me to do for you?” said Jesus, addressing him. “Rabboni,” the blind man answered, “I want to recover my sight.”
52 Yesu akamwambia, “Nenda. Imani yako imekuponya.” Hapo hapo macho yake yakaona; na akamfuata Yesu barabarani.
“You may go,” Jesus said, “Your faith has delivered you.” Immediately he recovered his sight, and began to follow Jesus along the road.