< Malaki 4 >

1 Tazama, siku inakuja, inaka kama tanuru, ambayo wote wenye kiburi na waharifu watakuwa mabua. siku inakuja itawachoma,” asema Bwana wa Majeshi, “siku hiyo itaondoa mzizi au shina.
For, behold, the day cometh, which shall burn as an oven; Then shall all the proud, And all that do wickedness, be stubble; And the day that cometh shall burn them up, Saith Jehovah of hosts; It shall leave them neither root nor branch.
2 Lakini kwenu mnaoliogopa jina langu, jua la haki litawaangazia na uponyaji katika mbawa zake. Mtarukaruka kama ndama zizini.
But for you that fear my name Shall the sun of salvation arise With healing under his wings. And ye shall go forth and leap for joy, Like calves of the stall.
3 Na waovu wote mtawakanyaga chini, watakuwa majivu chini ya nyazo za miguu yenu siku hiyo nitatenda,”asema Bwana wa Majeshi.
And ye shall tread down the wicked; For they shall be as dust under the soles of your feet In the day which I appoint, saith Jehovah of hosts.
4 Kumbukeni kutii sheria za mtumishi wangu Musa, mmri na sheria nilizomwamuru huko Horebu, kwa Israel wote.
Remember ye the law of Moses, my servant, Which I commanded him in Horeb for all Israel, My statutes and precepts!
5 Tazama, nitamtuma Eliya nabii mbele ya siku kuu na yenye kutisha ya kuja kwa Bwana.
Behold, I will send you Elijah, the prophet, Before the day of Jehovah come, The great and terrible day.
6 Atarudisha moyo wa baba kwa watoto, na mioyo ya watoto kwa baba zao; ili kwamba nisije nikaiangamiza nchi kwa uharibifu wote.”
He shall turn the heart of the fathers to the children, And the heart of the children to their fathers, That I may not come And smite the land with a curse.

< Malaki 4 >