< Luka 1 >

1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
Forasmuch as many have taken in hand to draw up a narrative concerning those matters which have been fulfilled among us,
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
even as they delivered them unto us, which from the beginning were eyewitnesses and ministers of the word,
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write unto thee in order, most excellent Theophilus;
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
that thou mightest know the certainty concerning the things wherein thou wast instructed.
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
There was in the days of Herod, king of Judaea, a certain priest named Zacharias, of the course of Abijah: and he had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elisabeth.
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
And they were both righteous before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
And they had no child, because that Elisabeth was barren, and they both were [now] well stricken in years.
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
Now it came to pass, while he executed the priest’s office before God in the order of his course,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
according to the custom of the priest’s office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
And the whole multitude of the people were praying without at the hour of incense.
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
And there appeared unto him an angel of the Lord standing on the right side of the altar of incense.
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
And Zacharias was troubled when he saw [him], and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
But the angel said unto him, Fear not, Zacharias: because thy supplication is heard, and thy wife Elisabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John.
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
And thou shalt have joy and gladness; and many shall rejoice at his birth.
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
For he shall be great in the sight of the Lord, and he shall drink no wine nor strong drink; and he shall be filled with the Holy Ghost, even from his mother’s womb.
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
And many of the children of Israel shall he turn unto the Lord their God.
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
And he shall go before his face in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of the fathers to the children, and the disobedient [to walk] in the wisdom of the just; to make ready for the Lord a people prepared [for him].
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
And Zacharias said unto the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife well stricken in years.
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
And the angel answering said unto him, I am Gabriel, that stand in the presence of God; and I was sent to speak unto thee, and to bring thee these good tidings.
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
And behold, thou shalt be silent and not able to speak, until the day that these things shall come to pass, because thou believedst not my words, which shall be fulfilled in their season.
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
And the people were waiting for Zacharias, and they marveled while he tarried in the temple.
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
And when he came out, he could not speak unto them: and they perceived that he had seen a vision in the temple: and he continued making signs unto them, and remained dumb.
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
And it came to pass, when the days of his ministration were fulfilled, he departed unto his house.
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
And after these days Elisabeth his wife conceived; and she hid herself five months, saying,
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
Thus hath the Lord done unto me in the days wherein he looked upon [me], to take away my reproach among men.
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
Now in the sixth month the angel Gabriel was sent from God unto a city of Galilee, named Nazareth,
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin’s name was Mary.
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
And he came in unto her, and said, Hail, thou that art highly favoured, the Lord [is] with thee.
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
But she was greatly troubled at the saying, and cast in her mind what manner of salutation this might be.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
And the angel said unto her, Fear not, Mary: for thou hast found favour with God.
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
And behold, thou shalt conceive in thy womb, and bring forth a son, and shalt call his name JESUS.
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
He shall be great, and shall be called the Son of the Most High: and the Lord God shall give unto him the throne of his father David:
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
and he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
And Mary said unto the angel, How shall this be, seeing I know not a man?
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
And the angel answered and said unto her, The Holy Ghost shall come upon thee, and the power of the Most High shall overshadow thee: wherefore also that which is to be born shall be called holy, the Son of God.
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
And behold, Elisabeth thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age: and this is the sixth month with her that was called barren.
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
For no word from God shall be void of power.
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
And Mary said, Behold, the handmaid of the Lord; be it unto me according to thy word. And the angel departed from her.
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
And Mary arose in these days and went into the hill country with haste, into a city of Judah;
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
and entered into the house of Zacharias and saluted Elisabeth.
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
And it came to pass, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Ghost;
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
and she lifted up her voice with a loud cry, and said, Blessed [art] thou among women, and blessed [is] the fruit of thy womb.
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
And whence is this to me, that the mother of my Lord should come unto me?
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
For behold, when the voice of thy salutation came into mine ears, the babe leaped in my womb for joy.
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
And blessed [is] she that believed; for there shall be a fulfillment of the things which have been spoken to her from the Lord.
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
And Mary said, My soul doth magnify the Lord,
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
And my spirit hath rejoiced in God my Saviour.
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
For he hath looked upon the low estate of his handmaiden: For behold, from henceforth all generations shall call me blessed.
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
For he that is mighty hath done to me great things; And holy is his name.
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
And his mercy is unto generations and generations On them that fear him.
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
He hath shewed strength with his arm; He hath scattered the proud in the imagination of their heart.
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
He hath put down princes from [their] thrones, And hath exalted them of low degree.
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
The hungry he hath filled with good things; And the rich he hath sent empty away.
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
He hath holpen Israel his servant, That he might remember mercy
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
(As he spake unto our fathers) Toward Abraham and his seed for ever. (aiōn g165)
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
And Mary abode with her about three months, and returned unto her house.
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
Now Elisabeth’s time was fulfilled that she should be delivered; and she brought forth a son.
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
And her neighbours and her kinsfolk heard that the Lord had magnified his mercy towards her; and they rejoiced with her.
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
And it came to pass on the eighth day, that they came to circumcise the child; and they would have called him Zacharias, after the name of his father.
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
And his mother answered and said, Not so; but he shall be called John.
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
And they said unto her, There is none of thy kindred that is called by this name.
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
And they made signs to his father, what he would have him called.
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
And he asked for a writing tablet, and wrote, saying, His name is John. And they marveled all.
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
And his mouth was opened immediately, and his tongue [loosed], and he spake, blessing God.
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
And fear came on all that dwelt round about them: and all these sayings were noised abroad throughout all the hill country of Judaea.
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
And all that heard them laid them up in their heart, saying, What then shall this child be? For the hand of the Lord was with him.
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
And his father Zacharias was filled with the Holy Ghost, and prophesied, saying,
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
Blessed [be] the Lord, the God of Israel; For he hath visited and wrought redemption for his people,
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
And hath raised up a horn of salvation for us In the house of his servant David
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
(As he spake by the mouth of his holy prophets which have been since the world began), (aiōn g165)
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
Salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us;
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
To shew mercy towards our fathers, And to remember his holy covenant;
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
The oath which he sware unto Abraham our father,
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
To grant unto us that we being delivered out of the hand of our enemies Should serve him without fear,
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
In holiness and righteousness before him all our days.
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
Yea and thou, child, shalt be called the prophet of the Most High: For thou shalt go before the face of the Lord to make ready his ways;
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
To give knowledge of salvation unto his people In the remission of their sins,
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
Because of the tender mercy of our God, Whereby the dayspring from on high shall visit us,
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
To shine upon them that sit in darkness and the shadow of death; To guide our feet into the way of peace.
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
And the child grew, and waxed strong in spirit, and was in the deserts till the day of his shewing unto Israel.

< Luka 1 >