< Luka 9 >

1 Akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa uwezo na mamlaka juu ya mapepo yote na kuponya magonjwa.
Then he called the Twelve together, and gave them power and authority over all demons, and to heal;
2 Akawatuma waende kuhubiri ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
and sent them out to preach the kingdom of God, and heal the sick.
3 Akawaambia, “Msichukue chochote kwa ajili ya safari yenu wala fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala pesa wala msichukue kanzu mbili.
And he said to them. "Take nothing for your journey, neither staff, nor bag, nor bread, nor money, and do not have two tunics.
4 Nyumba yoyote mtakayo iingia, kaeni humo mpaka mtakapo ondoka mahali hapo.
"Into whatever house you enter, there stay, and thence depart.
5 Na kwa wale wasio wapokea, mtakapo ondoka mji huo, jikung'uteni vumbi katika miguu yenu kwa ushuhuda juu yao”.
"If any one will not receive you, shake off the dust from your feet as you leave this town, as a testimony against them."
6 Wakaondoka na kwenda kupitia vijijini, wakitangaza habari njema na kuponya watu kila mahali.
So they went forth, and walked from village to village, preaching the gospel and healing everywhere.
7 Sasa Herode, mtawala, alisikia yote yaliyo kuwa yakitokea alitaabika sana, kwa sababuu ilisemekana na baadhi kwamba Yohana mbatizaji amefufuka kutoka wafu,
Now Herod, the Tetrarch, heard of all that was happening; and he was perplexed because of its being said by someone that Johnwas risen from the dead;
8 na baathi kwamba Elia amekwisha tokea, na kwa wengine kwamba mmoja wa manabii wa zamani amefufuka katika wafu tena.
and by some that Elijah had appeared; and by others that one of the ancient prophets was risen again.
9 Herode alisema, “nilimchinja Yohana, lakini huyu ni nani ninae sikia habari zake? Na Herode alitafuta njia ya kumwona Yesu.
So Herod said, "I beheaded John, but who is this of whom I am hearing such reports," And he kept seeking to see him.
10 Wakati waliporudi wale waliotumwa, wakamwamwambia kila kitu walicho fanya. Akawachukua pamoja naye, akaenda peke yake katika mji uitwao Bethsadia.
On their return the apostles told him what they had done. and he took them and withdrew in private to a town called Bethsaida.
11 Lakini makutano wakasikia kuhusu hili wakamfuata, na aliwakaribisha, na akaongea nao kuhusu ufalme wa Mungu, na aliwaponya wale waliohitaji uponyaji.
But when the crowd learned this they followed him. He received them kindly and spoke to them concerning the kingdom of God, and healed those who needed restored to good health.
12 Siku ikaanza kuisha, na wale kumi na wawili wakaenda kwake na kusema, “Watawanye makutano kwamba waende katika vijiji vya karibu na mijini wakatafute mapumziko na chakula, kwa sababu tupo eneo la nyikani.”
But now the day began to decline, and the twelve came to him and said. "Send away the crowd so that they may go into the villages and surrounding the country to lodge and buy provisions; for here we are on a solitary place."
13 Lakini akawaambia, “Nyie wapeni kitu cha kula.” Wakasema “Hatuna zaidi ya vipande vitano vya mikate na samaki wawili, isipokuwa tungeenda na kununua chakula kwa ajili ya kusanyiko hili la watu.”
"Do you yourselves give them food," he answered. "We have nothing," they replied "Except five loaves, and a couple fish, unless you mean for us to go and buy provisions for all the crowd."
14 Kulikua na wanaume wapatao elfu tano pale. Akawambia wanafunzi wake. “Wakalisheni chini katika makundi ya watu wapatao hamsini kwa kila kundi.
(For there were about five thousand men.) "Make them sit down in table-companies, of about fifty each," he said to his disciples.
15 Kwa hiyo wakafanya hivyo na watu wa wakaketi chini.
This they did, and made them all sit down.
16 Akachukua mikate mitano na samaki wawili na akatazama mbinguni, akavibariki, na kuvimega katika vipande, akawapa wanafunzi wake ili waviweke mbele ya makutano.
Then he took the five loaves and the two fish, and looking up in heaven, he blessed them, broke them in pieces, and began to giving to his disciples to apportion among the crowd.
17 Wote wakala na wakashiba, na vipande vya chakula vilivyo baki viliokotwa na kujaza vikapu kumi na viwili.
So they ate and were filled, all of them. And there was picked up that which remained over to them, of broken pieces, twelve basketfuls.
18 Nayo ikawa kwamba, alipokuwa akiomba peke yake, wanafunzi wake walikuwa pamoja naye, na akawauliza akisema, “watu husema mimi ni nani?”
Now it happened that while he was praying by himself, the disciples were with him, and he asked them a question. "Who do the crowd think I am?"
19 Wakijibu, wakasema, “Yohana mbatizaji, lakini wengine husema Eliya, na wengine husema mmoja wa manabii wa nyakati za zamani amefufuka tena.”
"Johnthe Baptist," they answered, "But others say Elijah, and others that one of the ancient prophets is risen again."
20 Akawambia, “Lakini ninyi mwasema mimi ni nani?” Akijibu Petro akasema, “Kristo kutoka kwa Mungu.”
Then he said to them, "But who do you say I am? Then Peter answered saying, "The Christ of God.’
21 Lakini kwa kuwaonya, Yesu akawaelekeza kutomwambia yeyote juu ya hili,
Then he strictly forbade them to tell this to any one;
22 akasema kwamba mwana wa Adamu lazma ateseke kwa mambo mengi na kukataliwa na wazee na Makuhani wakuu na waandishi, na atauawa, na siku ya tatu atafufuka.
and he said, "The Son of man must suffer much, and be restricted by the elders and high priests and scribes and be put to death, and on the third day be raised again."
23 Akawambia wote, “kama mtu yeyote akitaka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake kila siku, na anifuate.
And he said to all. "If any man wills to follow me, Let him renounce self and take up his cross daily and follow me.
24 Yeyote ajaribuye kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote apotezae maisha yake kwa faida yangu, atayaokoa.
"For whoever wills to save his life shall lose it; and whoever loses his life for my sake shall save it.
25 Je kitamfaidia nini mwanadamu, kama akiupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au akapata hasara ya nafsi yake?
"For what shall it profit a man if he shall gain the whole world and lose or forfeit himself?
26 Yeyote atakaye nionea aibu mimi na maneno yangu, kwake yeye mwana wa Adam atamuonea aibu atakapo kuwa katika utukufu wake, na utukufu wa Baba na malaika watakatifu.
"For whoever is ashamed of me and of my teachings, of him shall the Son of man be ashamed when he comes in his own and in his Father’s glory, and in that of the holy angels.
27 Lakini ninawaambia ukweli, kuna baadhi yenu wasimamao hapa, hawata onja umauti mpaka wauone ufalme wa Mungu.”
"But I tell you truly there are some of those standing here who will not taste death till they see the kingdom of God."
28 Ikatokea yapata siku nane baada ya Yesu kusema maneno haya kwamba akawachukua pamoja nae Petro, Yohana na, Yakobo, wakapanda mlimani kuomba.
About eight days after this it happened that Jesus took Peter, James, and John, and went up on the mountain to pray.
29 Na alipokuwa katika kuomba, muonekano wa uso wake ulibadilika, na mavazi yake yakawa meupe na ya kung'aa.
And as he was praying the appearances of his countenance became different, and his clothing became white and dazzling.
30 Na tazama, walikuwepo wanaume wawili wakiongea naye! Walikuwa Musa na Elia,
And suddenly there were two men talking with him, who were Moses and Elijah.
31 walionekana katika utukufu. Waliongea kuhusu kuondoka kwake, jambo ambalo alikaribia kulitimiza Yerusalem.
These appeared in glory and talked about his departure which he was about to accomplish at Jerusalem.
32 Sasa Petro na wale waliokua pamoja naye walikuwa katika usingizi mzito. Lakini walipokuamka, waliuona utukufu wake na wanaume wawili waliokuwa wamesimama pamoja nae.
Now Peter and those who were with him were heavy with sleep; but when they were fully awake they saw his glory, and the two men were standing beside him.
33 Ikatokea kwamba, walipokuwa wakiondoka kwa Yesu, Petro akamwambia, “Bwana, ni vizuri kwetu kukaa hapa na inatupasa tutengeneze makazi ya watu watatu. Tutengeneze moja kwa ajili yako, moja kwa ajili ya Musa, na moja kwa ajili ya Eliya.” Hakuelewa alichokuwa akiongelea.
And when they were preparing to depart from him Peter said to Jesus. "Master, it is good for us to be here; and let us make three tents, one for you, one for Moses, and one for Elijah" - not knowing what he was saying.
34 Alipokuwa akisema hayo, likaja wingu na likawafunika; na waliogopa walipoona wamezunguwa na wamezungukwa na wingu.
And while he was saying this, there came a cloud and began to overshadow them; and they were awestruck as they entered into the cloud.
35 Sauti ikatoka kwenye wingu ikasema, “Huyu ni Mwanangu mteule. Msikilizeni yeye.”
And a voice came out of the cloud, saying. "This is my Son, my chosen one; listen to him."
36 Sauti iliponyamaza, Yesu alikuwa peke yake. walikaa kimya, na katika siku hizo hawakumwambia yeyote lolote miongoni mwa waliyoyaona.
When the voice ceased Jesus was found alone. And they held their peace, and told no one at that time about what they had seen.
37 Siku iliyofuata, baada ya kutoka mlimani, kusanyiko kubwa la watu lilikutana naye.
It happened the next day, when they were come down from the mountain, that a large crowd came to meet him;
38 Tazama, mwanaume kutoka kwenye kusanyiko alilia kwa sauti, akisema, “Mwalimu ninakuomba umtazame mwanangu, kwa kuwa ni mwanangu wa pekee.
and a man called out of the crowd saying. "Teacher, I beg you to look upon my son; for he is my only boy,
39 Unaona roho chafu humshika, na mara hupiga kelele, na pia humfanya achanganyikiwe na kutokwa povu kinywani. Nayo humtoka kwa shida, ikimsababshia maumivu makali.
"and behold a spirit seizes hold of him, and rudely he shouts out, It convulses him till he foams; indeed it will hardly leave off bruising him sorely.
40 Naliwasihi wanafunzi wako kuikea itoke. lakini hawakuweza.”
"I begged your disciples to cast it out, but they could not."
41 Yesu akajibu akasema, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka, mpaka lini nitkaa nanyi na kuchukuliana nanyi? Mlete mwanao hapa.”
"O faithless and perverse generation," said Jesus, "how long shall I be with you and bear with you? Bring your son to me."
42 Kijana aliokuwa anakuja, roho cha ikamuangusha chini na kumtikisa kwa fujo. Lakini Yesu aliikemea ile roho chafu, alimponya mvulana, na kamkabidhi kwa baba yake.
But while he was yet coming the demon dashed him down, and cruelly convulsed him. Then Jesus rebuked the unclean spirit, and cured the boy, and gave him back to his father.
43 Wote walishangazwa na ukuu wa Mungu. Lakini walipokuwa wakistaajabu wote kwa mambo yote aliyo yaliyotedeka, akasema kwa wanafunzi wake,
And they were all awestruck at the mighty power of God. But while everyone was marveling at what he was doing, he said to his disciples.
44 “Maneno yawakae masikioni mwenu, kwa kuwa Mwana wa Adamu atatolewa mikononi mwa wanadamu.”
"Let these words sink into your ears; for the son of man is about to be betrayed into the hands of men."
45 Lakni hawakuelewa maana ya maneno hayo, na yalifichwa machoni pao, ili wasije wakalielewa. Waliogopa kumuuliza kuhusu neno hilo.
But they did not understand this saying; it was hidden from them so that they perceived it not, and they were sore afraid to ask him about his saying.
46 Kisha mgogoro ulianza ulizuka miongoni mwao i juu ya nani angekuwa mkuu.
Now there arose a dispute among them as to which one of them was the greatest.
47 Lakini Yesu alipotambua walichokuwa wakihojiana mioyoni mwao, alimchukua mtoto mdogo, na kumuweka upande wake,
And Jesus who knew the dispute that was in their hearts, took a young child, and placed him by his side;
48 na akasema, “kama mtu yeyote akimpokea mtoto mdogo kama huyu kwa jina langu, anipokea mimi pia, na yeyote akinipokea mimi, ampokea pia aliyenituma, kwa kuwa aliye mdogo kati yenu wote ndiye alie mkuu”
then he said to them. "Whoever shall receive this little child in my name receives me; and whoever shall receive me receives him that sent me. For it is the lowliest among you all who is great."
49 Yohana akajibu akasema, “Bwana, tulimuona mtu akifukuza pepo kwa jina lako na tukamzuia, kwa sababu haambatani na sisi.”
"Master," said John, "we saw a man who was casting out demons in your name, and we forbade him, because he was not following us."
50 Lakini Yesu akamwambia, “Msimzuie, kwa kuwa asiye kinyume na ninyi ni wa kwenu”
But Jesus said, "Forbid him not, for he who is not against you is for you."
51 Ikatokea kwamba, kulinga na siku zilivyokua zikikaribia zsiku zake za kwenda mbinguni, kwa uimara alielekeza uso wake Yerusalemu.
When now when the time drew near for him to be received up, he stedfastly set his face to go to Jerusalem,
52 Akatuma wajumbe mbele yake, nao wakaenda na kuingia katika kijiji cha Wasamaria ili wamtayarishie mahali.
and sent messengers before him. These went and entered into a Samaritan village to make ready for him.
53 Lakini watu huko hawakumpokea, kwasababu alikua ameelekeza uso wake Yerusalemu.
But they did not receive him because his face was set to go to Jerusalem.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipo liona hili, wakasema, “Bwana unahitaji tuamuru moto ushuke chini kutoka mbinguni uwateketeze?”
And when his disciples, Jamesand John, saw this they said, "Lord, are you willing for us to bid fire come down from heaven and destroy them?" As Elijah did.
55 Lakini aliwageukia akawakemea.
But he turned and rebuked them and said,
56 Kisha walikwenda kijiji kingine.
"You know not what kind of spirit you share, for the Son of man came not to destroy men’s lives, but to save them." And they went to another village.
57 Walipokuwa wakienda katika njia yao, mtu mmoja akamwambia, “Nitakufuata popote uendapo.”
As they were going on their way, a man came to him and said, "I will follow wherever you go."
58 Yesu akamwambia, “Mbweha wanamashimo, ndege wa angani wana viota, lakini mwana wa Adamu hana pakulaza kichwa chake.”
"The foxes have their holes," Jesus answered, "and the wild birds have their nest, but the Son of man has not where to lay his head."
59 Ndipo akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Lakini yeye akasema, “Bwana, niruhusu kwanza niende nikamzika baba yangu,”
To another he said, "Follow me!" But he replied, "Permit me first to go and bury my father."
60 Lakini yeye akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, lakini wewe nenda ukautangaze ufalme wa Mungu kila mahali.”
"Leave the dead to bury their own dead," said Jesus to him, "go you and announce, far and wide the kingdom of God."
61 Pia mtu mwingine akasema. “Nitakufuata, Bwana, lakini niruhusu kwanza nikawaage walio katika nyumba yangu.”
And another man also said to him. "I will follow you, Lord; but first permit me to bid farewell to those who are in my house."
62 Laki Yesu akamwambia hakuna mtu, atiaye mkono wake kulima na kuangalia nyuma atakayefaa kwa ufalme wa Mungu.”
But Jesus answered him, "No man who puts his hand to the plow and then looks back, is fit for the kingdom of God."

< Luka 9 >