< Luka 6 >

1 Sasa ilitokea kwenye Sabato kwamba Yesu alikuwa akipita katika ya shamba la nafaka na wanafunzi wake walikuwa wakichuma masuke, wakayasuguasugua kati ya mikono yao wakala nafaka.
Agora, no segundo sábado depois do primeiro, ele estava passando pelos campos de grãos. Seus discípulos arrancaram as cabeças dos grãos e comeram, esfregando-os em suas mãos.
2 Lakini baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Kwa nini mnafanya kitu ambacho si halali kisheria kukifanya siku ya sabato”?
Mas alguns dos fariseus lhes disseram: “Por que vocês fazem o que não é lícito fazer no dia de sábado?
3 Yesu, akawajibu, akisema, “Hamkuwahi kusoma kile Daudi alifanya alipokuwa na njaa, yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye?
Jesus, respondendo-lhes, disse: “Não leram o que Davi fez quando tinha fome, ele e os que estavam com ele,
4 Alikwenda katika nyumba ya Mungu, na akachukuwa mikate mitakatifu na kuila baadhi, na kuitoa baadhi kwa watu aliokuwa nao kuila, hatakama ilikuwa halali kwa makuhani kuila.”
como entrou na casa de Deus, tomou e comeu o pão do espetáculo, e deu também aos que estavam com ele, o que não é lícito comer a não ser só aos sacerdotes”?
5 Kisha akawaambia, “Mwana wa Adamu ni Bwana wa Sabato.”
Ele disse a eles: “O Filho do Homem é senhor do sábado”.
6 Ilitokea katika Sabato nyingine kwamba alikwenda ndani ya sinagogi na kuwafundisha watu huko. Palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kulia ulikuwa umepooza.
Aconteceu também em outro sábado que ele entrou na sinagoga e ensinou. Havia lá um homem, e sua mão direita estava murcha.
7 Waandishi na Mafarisayo walikuwa wanamwangalia kwa makini kuona kama angemponya mtu siku ya Sabato, ili waweze kupata sababu ya kumshtaki kwa kufanya kosa.
Os escribas e os fariseus o observavam, para ver se ele curaria no sábado, para que encontrassem uma acusação contra ele.
8 Lakini alijua nini walikuwa wanafikiri na akasema kwa mtu aliyekuwa amepooza mkono, “Amka, simama hapa katikati ya kila mmoja.” Hivyo huyo mtu akanyanyuka na kusimama pale.
Mas ele conhecia seus pensamentos; e disse ao homem que tinha a mão murcha: “Levante-se e fique no meio”. Ele se levantou e ficou de pé.
9 Yesu akasema kwao, “Nawauliza ninyi, ni halali siku ya Sabato kufanya mema au kufanya madhara, kuokoa maisha au kuyaharibu?” Kisha aliwaangalia wote na kumwambia yule mtu,
Então Jesus lhes disse: “Vou lhes perguntar uma coisa: é lícito no sábado fazer o bem, ou fazer o mal? Para salvar uma vida, ou para matar”?
10 “Nyoosha mkono wako.” Akafanya hivyo, na mkono wake ulikuwa umeponywa.
Ele olhou em volta para todos eles e disse ao homem: “Estende a mão”. Ele o fez, e sua mão foi restaurada tão bem quanto a outra.
11 Lakini walijawa na hasira, wakaongeleshana wao kwa wao kuhusu nini wanapaswa wafanye kwa Yesu.
Mas eles estavam cheios de raiva, e conversaram uns com os outros sobre o que poderiam fazer a Jesus.
12 Ilitokea siku hizo kwamba alikwenda mlimani kuomba. Aliendelea usiku mzima kumuomba Mungu.
Nestes dias, ele foi para a montanha para rezar, e continuou a noite inteira em oração a Deus.
13 Ilipokuwa asubuhi, aliwaita wanafunzi wake kwake, na akawachagua kumi na wawili kati yao, ambao pia aliwaita “mitume.”
Quando era dia, ele chamou seus discípulos, e dentre eles escolheu doze, a quem também nomeou apóstolos:
14 Majina ya wale mitume yalikuwa Simoni (ambaye pia alimwita Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartolomayo,
Simão, a quem também chamou Pedro; André, seu irmão; Tiago; João; Filipe; Bartolomeu;
15 Mathayo, Tomaso na Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni, ambaye aliitwa Zelote,
Mateus; Tomé; Tiago, filho de Alfeu; Simão, chamado de Zelota;
16 Yuda mwana Yakobo na Yuda Iskariote, ambaye alikuwa msaliti msaliti.
Judas, filho de Tiago; e Judas Iscariotes, que também se tornou um traidor.
17 Kisha Yesu alitelemka pamoja nao toka mlimani na kusimama mahali tambarare. Idadi kubwa ya wanafunzi wake walikuwa huko, pamoja na idadi kubwa ya watu kutoka Uyahudi na Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
Ele desceu com eles e ficou em um lugar plano, com uma multidão de seus discípulos e um grande número de pessoas de toda a Judéia e Jerusalém e da costa marítima de Tiro e Sidon, que vieram para ouvi-lo e para serem curados de suas doenças,
18 Walikuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Watu waliokuwa wakisumbuliwa na pepo wachafu waliponywa pia.
assim como aqueles que estavam perturbados por espíritos impuros; e eles estavam sendo curados.
19 Kila mmoja kwenye hilo kusanyiko alijaribu kumgusa kwa sababu nguvu za uponyaji zilikuwa zikitokea ndani yake, na aliwaponya wote.
Toda a multidão procurava tocá-lo, pois o poder saía dele e curava a todos eles.
20 Kisha akawaangalia wanafunzi wake, na kusema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa maana ufalme wa Mungu ni wenu.
Ele levantou os olhos para seus discípulos, e disse: “Abençoados sejam vocês que são pobres”, pois o Reino de Deus é seu.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa maana mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mliao sasa, kwa maana mtacheka.
Abençoados sejam vocês que têm fome agora, para você será preenchido. Abençoados sejam vocês que choram agora, pois você vai rir.
22 Mmebarikiwa ninyi ambao watu watakapowachukia na kuwatenga na kuwashutumu ninyi kwamba ni waovu, kwa ajili ya Mwana Adamu.
Abençoado sejas quando os homens te odeiam, e quando te excluem e zombam de ti, e deitam fora teu nome como maligno, pelo bem do Filho do Homem.
23 Furahini katika siku hiyo na kurukaruka kwa furaha, kwa sababu hakika mtakuwa na thawabu kubwa mbinguni, kwa maana baba zao waliwatendea vivyohivyo manabii.
Alegre-se naquele dia e pule de alegria, pois eis que sua recompensa é grande no céu, pois seus pais fizeram a mesma coisa com os profetas.
24 Lakini ole wenu mlio matajiri! Kwa maana mmekwisha pata faraja yenu.
“Mas ai de vocês que são ricos! Pois você recebeu o seu consolo.
25 Ole wenu mlio shiba sasa! Kwa maana mtaona njaa baadaye. Ole wenu mnaocheka sasa! Kwa maana mtaomboleza na kulia baadaye.
Ai de vocês, que agora estão cheios, pois você estará com fome. Ai de vocês que riem agora, pois você vai lamentar e chorar.
26 Ole wenu, mtakaposifiwa na watu wote! Kwa maana baba zao waliwatendea manabii wa uongo vivyohivyo.
Woe, quando os homens falam bem de você, pois seus pais fizeram a mesma coisa com os falsos profetas.
27 Lakini nasema kwenu ninyi mnaonisikiliza, wapendeni adui zenu na kufanya mema kwa wanao wachukieni.
“Mas eu lhes digo a vocês que ouvem: amem seus inimigos, façam o bem àqueles que os odeiam,
28 Wabarikini wale wanao walaani ninyi na waombeeni wale wanaowaonea.
abençoem aqueles que os amaldiçoam e rezem por aqueles que os maltratam.
29 Kwake yeye akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili. Kama mtu akikunyang'anya joho lako usimzuilie na kanzu.
Àquele que te bater na bochecha, oferece-lhe também o outro; e àquele que te tirar o manto, não te esconda também o casaco.
30 Mpe kila akuombaye. Kama mtu akikunyang'anya kitu ambacho ni mali yako, usimuombe akurudishie.
Ofereça a todos que lhe pedirem, e não peça a quem lhe tirar seus bens que os devolva novamente.
31 Kama mpendavyo watu wawatendee, nanyi watendeeni vivyo hivyo.
“Como você gostaria que as pessoas fizessem com você, faça exatamente isso com elas”.
32 Kama mkiwapenda watu wawapendao ninyi tu, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwamaana hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao.
“Se você ama aqueles que o amam, que crédito é esse para você? Pois até os pecadores amam aqueles que os amam.
33 Kama mkiwatendea mema wale wanaowatendea ninyi mema, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwa maana hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo.
“Se você faz o bem àqueles que lhe fazem o bem, que crédito é esse para você? Pois até mesmo os pecadores fazem o mesmo.
34 Kama mkikopesha vitu kwa watu ambao mnategemea watawarudishia, hiyo ni thawabu gani kwenu? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, na hutegemea kupokea kiasi hicho hicho tena.
Se você empresta àqueles de quem você espera receber, que crédito é esse para você? Mesmo os pecadores emprestam aos pecadores, para receber de volta o mesmo valor.
35 Lakini wapendeni adui zenu na watendeeni mema. Wakopesheni na msihofu kuhusu kurudishiwa, na thawabu yenu itakuwa kubwa. Mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwasababu yeye mwenyewe ni mwema kwa watu wasio na shukurani na waovu.
Mas ame seus inimigos, e faça o bem, e empreste, não esperando nada de volta; e sua recompensa será grande, e vocês serão filhos do Altíssimo; pois ele é bondoso para com os ingratos e maus.
36 Iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
“Portanto, seja misericordioso, mesmo quando seu Pai também é misericordioso.
37 Msihukumu, nanyi hamta hukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Sameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
Não julgue, e você não será julgado. Não condenar, e você não será condenado. Liberte-se, e você será libertado.
38 Wapeni wengine, nanyi mtapewa. Kiasi cha ukarimu - kilichoshindiliwa, kusukwasukwa na kumwagika - kitamwagika magotini penu. Kwa sababu kwa kipimo chochote mnachotumia kupimia, kipimo hicho hicho kitatumika kuwapimia ninyi.”
“Dê, e será dado a você: boa medida, pressionado, sacudido juntos, e atropelado, será dado a você”. Pois com a mesma medida que você mede, ela será medida de volta para você”.
39 Kisha akawaambia mfano pia. “Je mtu aliye kipofu aweza kumwongoza mtu mwingine kipofu? Kama alifanya hivyo, basi wote wangalitumbukia shimoni, je wasingetumbukia?
Ele lhes contou uma parábola. “O cego pode guiar o cego? Não cairão os dois em um buraco?
40 Mwanafunzi hawi mkubwa kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu akiisha kufundishwa kwa ukamilifu atakuwa kama mwalimu wake.
Um discípulo não está acima de seu professor, mas todos quando ele estiver totalmente treinado serão como seu professor.
41 Na kwa nini basi wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti lililo ndani ya jicho lako huliangalii?
Por que você vê o grão de palha que está no olho de seu irmão, mas não considera a viga que está em seu próprio olho?
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, 'Ndugu, naomba nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,' nawe huangalii boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Kwanza itoe boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utaona vizuri kutoa kibanzi katika jicho la ndugu yako.
Ou como você pode dizer a seu irmão: 'Irmão, deixe-me remover o grão de palha que está em seu olho', quando você mesmo não vê a trave que está em seu próprio olho? Seu hipócrita! Primeiro remova a trave de seu próprio olho, e então você pode ver claramente para remover o grão de palha que está no olho de seu irmão.
43 Kwa sababu hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
“Pois não há árvore boa que produza frutos podres, nem novamente uma árvore podre que produza bons frutos”.
44 Kwa sababu kila mti hutambulika kwa matunda yake. Kwa sababu watu hawachumi tini kutoka kwenye miba, wala hawachumi zabibu kutoka kwenye michongoma.
Pois cada árvore é conhecida por seus próprios frutos. Pois as pessoas não apanham figos de espinhos, nem apanham uvas de um arbusto de silvado.
45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu. Kwa sababu kinywa chake husema yale yaujazayo moyo wake.
O homem bom do bom tesouro de seu coração tira o que é bom, e o homem mau do tesouro mau de seu coração tira o que é mau, pois da abundância do coração, sua boca fala.
46 Kwanini mnaniita, 'Bwana, Bwana', na bado hamyatendi yale nisemayo?
“Por que você me chama de 'Senhor, Senhor', e não faz as coisas que eu digo?
47 Kila mtu ajaye kwangu na kuyasikia maneno yangu na kuyatendea kazi, nitawaonyesha jinsi alivyo.
Todos que vêm até mim, e ouvem minhas palavras e as fazem, eu lhes mostrarei como ele é.
48 Anafanana na mtu ajengae nyumba yake, ambaye huchimba chini sana, na kujenga msingi wa nyumba juu ya mwamba imara. Mafuriko yalipokuja, maporomoko ya maji yaliipiga nyumba, lakini hayakuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
Ele é como um homem que constrói uma casa, que cavou e foi fundo e lançou uma fundação sobre a rocha. Quando surgiu uma enchente, o riacho quebrou-se contra aquela casa, e não conseguiu sacudi-la, porque foi fundada sobre a rocha.
49 Lakini yeyote asikiaye neno langu na hakulitii; mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ulipoishukia kwa nguvu, nyumba ile ilitopata maangamizi makubwa.
Mas quem ouve e não ouve, é como um homem que construiu uma casa na terra sem um alicerce, contra a qual o riacho quebrou, e imediatamente caiu; e a ruína daquela casa foi grande”.

< Luka 6 >