< Luka 5 >
1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
Aitulikile matungo iantu akizura nakumupilimilya U-Yesu nukumutegelya ulukani Langwi Itunda, nai wimikile panipelo aluzi la Genesareti.
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
Auine mabine abili Imikingwe kupelo aluzi Iaibua Samaki aiapumaa aiakoja inyabu yao.
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
U-Yesu akingila mibini, nai lang'wa Simoni na akalompa atwale ibini muluzi kuli inino nihi ninyumu. hangi akikie kumumanyisa kupuma mibini.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
Akaligitia, akamuila U-Simoni litwale ibini lako muluzi uisimie inyabu yako utule bua Insamaki.
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
Simoni akasusha nukulunga, tata kituma, aimilimo uliku wihi, Shakupatile anga kintu kihi hangi kulukani lako kuisimya inyabu.
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
Naitumile uu ikahoela Insamaki iduu na lyabu yao yika tula tinike.
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
Ikaitanga Iabuani ao kibini Ingiza hangi aze kua ailya. Ikaza akizulia imabini ihi ikatula kilieka mukati muluzi.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
Hangi Simoni Petro nauine uu, akatugama na malu pang'wa Yesu akalunga;''Hega kitalane, kunsoko une ni muntu wamilandu tata.
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
Kunsoko akapata ikuilwa ihi naine kunsamaki naiatendile.
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
Ulu iti aliakuile uYakobo na Yohana ng'wana wang'wa Zebedayo aipulug'wi nu Simoni. Nu Yesu akamuila uSimoni kandya itungili apana kogopa kumbele ukutula bua iantu.
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
Naiamaletile imabini ao mihi ni nyumu, kaleka kintu kihi ikamutyata nuanso.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
Niipumie naukali mukisali muntu naukete ibili kuko, matungo namuine U-Yesu augwie akakumana pihi nukulompa, akalunga,''tata ang'wi uloiwe umponie.''
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
Sunga U-Yesu akahumbula umukona nukumuamba, akalunga ndoilwa ukomie itungo lilo imbili iakahega.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
Akamuile alekekumuila anga muntu wihi, akamula longala wionyeshe nu utemi upumie isongiliyo.
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
Kulula ikani yakwe ikasambaila kui, numilundo wa antu ukaza palung'wi nukumutigelya numanyisa nukuguna imalwae ao.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
Ingi hapu hapuu akikie wingene akazilompa.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
Aituile luhiku lungwi nema hiku ayo naukumanyisa, aiokoli Mafarisayo niamanyisa anonya nkai akikie hapo aizile kupuma muisali ningiza numukisali kang, wa Galilaya nanu Yudea, hangi nukupuma mukisali kang'wa Yerusalemu. Ingulu yang'wa tata akali palung'wi nung'wenso kuguna.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
antu akehu aiazile, ainkenkile mundili umuntu nuigandi naikai ikaduma inzila akumingilya mukati amulalishe pihi kuntongela ang'wa Yesu.
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
Shaikapata inzila akumingilya mukati kunsoko umilundo, ukanankila migulya milialo lanyumba ikamusunta muntu nuanso pihi kukiila mibolomya migulya mundili akwe mukati wa antu kuntongela lukulu pang'wa Yesu.
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
Akazigoza uhuili wakwe, Yesu akalunga muhumba miane, imilandu ako wasamehelwa.
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
Anumwa nkani ni mafalisayo ikandya kukolya nulanso, akalunga uyu nyenyu nukuligitya kuubii? Nyenyu nuhumile kusamehela imilandu ingi Itunda du nuing'wine?
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
Ingi u Yesu ainualinga ntuni naiakukisiga, akasukilya, nukuaila, kuniki nimukikolya mukolo yanyu?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
Nikiuli nikipepele kulugilya, Imilandu ako alekwa ang'wi kulunga uka ugende?
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
Ingi mulinge gwa ung'wana wang'wa Adamu ukite uhumu muukumbigulu kusamehela imilandu, kuila uewe uka uhole indili ako ulongole kitalako.
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
Imatungo yayo yayo akauko meleao nukuhola indili akwe naulaie. Hangi akasuka kitalakwe nukumukulya Itunda.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
Ingi kila ung'wi ao akakuilwa nukumukulya Itunda. Ikizuilwa nuao, ikalunga, kuine ikani shanga nzaile liyi.
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
Ingi inkani nianso kupumila, u Yesu akahega kung'wanso akamuona umuhoela mpia naiwitang'wa Lawi wikie mukisali kakuhoela mpia. Akamuiila, ntwate.
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
Ingi u Lawi akahumbuka nukumuntwata, akaleka kila kintu kunyuma.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
Ingi u Lawi akanunelya munyumbakwe isikukuu ninkulu kunsoko ang'wa Yesu. Aiakoli iahoela mpia indu kung'wanso ni antu indu naiikie pameza akizilya palung'wi nienso.
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
Hangi mafalisayo aiakuanung'u nikila iamanyisigwa akizilunga, kuniki nimukulya nukung'wa niahoela mpia palung'wi ni antu niangiza niakite milandu?
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
U Yesu akasusha, iantu niakite upanga nuuza shaatakile itabibu, ingi ao nialwaeli niaamutakile ung'wi.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
Shainzile kuitanga iantu makite itai ahume kugunwa, ingi ainziitanga nia milandu ahume kugunwa.
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
Ikamuila, iamanyisigwa ang'wa Yohana a hapouifunga nukulompa, ni amanyisigwa ang'wa mafalisayonienso itenda uu, Ai amanyisigwa ako iliza nukung'wa.
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
U Yesu akaaila, ihumile muntu wihi kituma naiendile muwinga kumunyawinga, matungo numunyawinga, kilukoli palung'wi nienso?
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
Ingi imahiku aziziza imatungo umunyamwinga nuzi hegigwa kitalao, lulo luhiku lakufunga.
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
Ingi u Yesu akaligitya kitalao kwakilingasilyo. Hutile nukutamula inino ung'wenda kupuma mivazi nipya nukutumila kunonelya ivazi nilakali. Anga watende uu, ukutamula ung'wenda.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
Hangi kutile anga muntu nuika idivai nimpya muuriba nunkulukulu, inga angitume uu, idivai nimpya aizitamula. Ikiseme ni divai aizihunuka iriba aiyizigazika.
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
Ingi idivai nimpya iikwe muiliba nimpya.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
Kutile umuntu hangi nukung'wa idivai na kali, shukulowa nimpya kunsoko ukulunga na kali nza.