< Luka 5 >

1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
One day, as Jesus was standing beside the Sea of Galilee, people crowded around him to hear the word of God.
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
Jesus noticed two boats lying on the shore, left there by fishermen who were washing their nets.
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
Jesus got into a boat, the one that belonged to Simon, and asked him to push it out into the water, just offshore. Then Jesus sat down in the boat and taught the people from there.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
After he'd finished speaking, he told Simon, “Go out into deeper water, and let down your nets for a catch.”
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
“Lord, we worked hard all night, and didn't catch anything. But if you say so, I'll let down the nets,” Simon replied.
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
Having done this, a large shoal of fish filled the nets full to breaking point.
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
They waved to their partners in the other boat, asking them to come over and help. The others came over and together they filled both of the boats with fish. The boats were so full that they began to sink.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
When Simon Peter saw what had happened, he dropped to his knees before Jesus. “Lord, please stay away from me, for I am a sinful man!” he exclaimed.
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
For he and everybody with him were completely amazed by the catch of fish that they had landed.
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
James and John, the sons of Zebedee, Simon's partners, felt the same way. “Don't be afraid,” Jesus told Simon. “From now on you'll be fishing for people!”
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
So they dragged the boats onto the shore, left everything, and followed Jesus.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
Once when Jesus was visiting one of the towns, he met a man there who had a very bad case of leprosy. The man fell with his face to the ground and begged Jesus, “Please Lord, if you're willing, you can make me clean.”
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
Jesus reached out and touched the man. “I am willing,” he said. “Be clean!” Immediately the leprosy disappeared.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
“Say nothing to anyone,” Jesus instructed him. “Go and show yourself to the priest and make the ceremonial offerings as required by the law of Moses as proof that you've been healed.”
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
Yet the news about Jesus spread more and more. Large crowds came to hear Jesus and to be healed from their diseases.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
But Jesus often used to retreat to quiet places and pray.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
One day when Jesus was teaching, the Pharisees and religious teachers who had come from all over Galilee, Judea, and Jerusalem were sitting there. The power of the Lord to heal was with him so he could heal.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
Some men arrived carrying a paralyzed man on a mat. They tried to take him in and lay him in front of Jesus.
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
But they couldn't find any way through the crowd, so they went up on the roof and made a hole in the roof tiles. Then they lowered the man down on the mat, right into the crowd in front of Jesus.
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
When Jesus saw the trust they had in him, he said to the man, “Your sins are forgiven.”
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
The religious teachers and the Pharisees began to argue with that. “Who is this who's speaking blasphemies?” they asked. “Who can forgive sins? Only God can do that!”
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
Jesus knew what they were arguing about, so he asked them, “Why are you thinking to question this?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
What is easier? To say your sins are forgiven, or to say get up and walk?
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
However, I will prove to you that the Son of man has the authority here on earth to forgive sins.” Then he said to the paralyzed man, “I tell you: Get up, pick up your mat, and go home.”
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
Immediately the man stood up in front of them. He picked up the mat he'd been lying on, and went home, praising God as he went.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
Everyone was completely astonished at what had happened, and in great awe they praised God, saying, “What we saw today was amazing!”
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
Later, as Jesus was leaving the town, he saw a tax collector called Levi sitting at his tax booth. “Follow me,” Jesus told him.
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
Levi stood up, left everything, and followed Jesus.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
Levi organized a large banquet at his home in Jesus' honor. Many tax collectors and others were in the crowd that sat down to eat with them. But the Pharisees and the religious teachers complained to Jesus' disciples, asking,
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
“Why do you eat and drink with tax collectors and sinners?”
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
“Healthy people don't need a doctor—but sick people do,” Jesus replied.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
“I didn't come to call those who are living right to repentance—I came to call sinners.”
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
“Well, John's disciples often fast and pray, and the Pharisees' disciples do so as well. But your disciples don't—they go on eating and drinking,” they told him.
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
“Should the groomsmen fast while the bridegroom is with them?” Jesus asked.
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
“No—but the time is coming when the bridegroom will be taken away from them. Then they can fast.”
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
Then he gave them an illustration: “You don't tear out a patch from new clothes to mend old clothes. Otherwise you'd ruin new clothes, and the patch from the new wouldn't match the old.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
You don't put new wine into old wineskins, because if you did the new wine would burst the wineskins. Then both wine and wineskins would be wasted.
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
You put new wine in new wineskins.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
And nobody after drinking old wine wants new wine, for they say, ‘the old tastes good.’”

< Luka 5 >