< Luka 4 >

1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
Jésus, plein de l’Esprit-Saint, revint du Jourdain; et il était conduit par l’Esprit dans le désert
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
Pendant quarante jours, et il était tenté par le diable. Durant ces jours il ne mangea rien, et après qu’ils furent passés, il eut faim.
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
Or le diable lui dit: Si vous êtes le Fils de Dieu, dites à cette pierre qu’elle devienne du pain.
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
Jésus lui répondit: Il est écrit: L’homme ne vit pas seulement de pain, mais de toute parole de Dieu.
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
Alors le diable le conduisit sur une haute montagne, et il lui montra en un instant tous les royaumes de la terre;
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
Puis il lui dit: Je vous donnerai toute cette puissance et toute la gloire de ces royaumes: car ils m’ont été livrés, et je les donne à qui je veux.
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
Si donc vous m’adorez, ils seront tous à vous.
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
Et Jésus répondant, lui dit: Il est écrit: Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu ne serviras que lui seul.
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
il le conduisit ensuite à Jérusalem, le posa sur le haut du temple et lui dit: Si vous êtes le Fils de Dieu, jetez-vous d’ici en bas.
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
Car il est écrit qu’il a ordonné à ses anges de vous garder;
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
Et qu’ils vous porteront en leurs mains, de peur que vous ne heurtiez votre pied contre la pierre.
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Jésus répondant, lui dit: il a été dit: Tu ne tenteras point le Seigneur ton Dieu.
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
Or toute tentation achevée, le diable se retira de lui pour un temps.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
Et Jésus retourna en Galilée, par la vertu de l’Esprit, et sa renommée se répandit dans tout le pays.
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
Et il enseignait dans leurs synagogues, et il était exalté par tous.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
Il vint à Nazareth, où il avait été élevé, et il entra, suivant sa coutume, le jour du sabbat, dans la synagogue, et il se leva pour lire.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
On lui donna le livre du prophète Isaïe; et l’ayant déroulé, il trouva l’endroit où il était écrit:
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
L’Esprit du Seigneur est sur moi; c’est pourquoi il m’a consacré par son onction, et m’a envoyé pour évangéliser les pauvres, guérir ceux qui ont le cœur brisé,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
Annoncer aux captifs leur délivrance, aux aveugles le recouvrement de la vue, rendre à la liberté ceux qu’écrasent leurs fers, publier l’année salutaire du Seigneur, et le jour de la rétribution.
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
Ayant replié le livre, il le rendit au ministre, et s’assit: Et tous, dans la synagogue, avaient les yeux attachés sur lui.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
Or il commença à leur dire: C’est aujourd’hui que cette Ecriture que vous venez d’entendre est accomplie.
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
Et tous lui rendaient témoignage, et admirant les paroles de grâce qui sortaient de sa bouche, ils disaient: N’est-ce pas là le fils de Joseph?
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
Alors il leur dit: Assurément vous m’appliquerez ce proverbe: Médecin, guéris-toi toi-même, et me direz: Ces grandes choses faites à Capharnaüm et dont nous avons ouï parler, fais-les ici dans ta patrie.
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
Et il ajouta: En vérité, je vous dis qu’aucun prophète n’est accueilli dans sa patrie.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
Je vous le dis, en vérité, il y avait aux jours d’Elie beaucoup de veuves en Israël, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et six mois, et qu’il y eut une grande famine sur toute la terre;
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
Et Elie ne fut envoyé à aucune d’elles, mais à une femme veuve, à Sarepta de Sidon.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
Et il y avait en Israël beaucoup de lépreux au temps du prophète Elisée, et aucun d’eux ne fut guéri, sinon Naaman le Syrien.
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
En entendant ces paroles, ils furent tous remplis de colère dans la synagogue;
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
C’est pourquoi ils se levèrent, le jetèrent hors de la ville, et le menèrent au sommet du mont sur lequel leur ville était bâtie, pour l’en précipiter.
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
Mais Jésus passant au milieu d’eux, s’en alla.
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
Et il descendit à Capharnaüm, ville de Galilée, et là il les enseignait aux jours du sabbat.
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
Et ils s’étonnaient de sa doctrine, parce qu’il leur parlait avec autorité.
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
Or il y avait dans la synagogue un homme ayant en lui un démon impur, et il cria d’une voix forte,
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
Disant: Laissez-nous! Qu’importe à nous et à vous, Jésus de Nazareth? Êtes-vous venu pour nous perdre? Je sais qui vous êtes: le saint de Dieu.
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
Et Jésus le gourmanda, disant: Tais-toi, et sors de cet homme. Et le démon l’ayant jeté à terre au milieu de l’assemblée, sortit de lui et ne lui fit aucun mal.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
Et l’épouvante les saisit tous, et ils se parlaient entre eux, disant: Qu’est-ce que ceci: il commande avec puissance et force aux esprits impurs, et ils sortent?
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
Et sa renommée se répandit de tous côtés dans le pays.
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
Etant sorti de la synagogue, Jésus entra dans la maison de Simon. Or la belle-mère de Simon avait une grosse fièvre; et ils le prièrent pour elle.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
Alors étant debout auprès d’elle, il commanda à la fièvre, et la fièvre la quitta. Et se levant aussitôt, elle les servait.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
Lorsque le soleil fut couché, tous ceux qui avaient des infirmes atteints de diverses maladies, les lui amenaient. Or Jésus, imposant les mains sur chacun d’eux, les guérissait.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
Et les démons sortaient d’un grand nombre, criant et disant: Vous êtes le fils de Dieu; et les gourmandant il ne leur permettait pas de dire qu’ils sussent qu’il était le Christ.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
Lorsqu’il fit jour, il sortit et s’en alla en un lieu désert, et la foule le cherchait; et ils vinrent à lui, et ils le retenaient, de peur qu’il ne les quittât.
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
Il leur dit: Il faut que je prêche aux autres villes le royaume de Dieu, car c’est pour cela que j’ai été envoyé.
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
Et il prêchait dans les synagogues de Galilée.

< Luka 4 >