< Luka 4 >
1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
Jésus, rempli de l'Esprit saint, revint des bords du Jourdain; l'Esprit le poussait au désert.
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
Il y passa quarante jours; il était tenté par le diable. Durant ces quarante jours, il ne mangea rien, et quand ils furent achevés, il eut faim.
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
Le diable lui dit: «Si tu es Fils de Dieu, dis à cette pierre de se changer en pain»;
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
et, Jésus lui répondit: «Il est écrit: «Ce n'est pas de pain seulement que vivra l'homme.»
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
Puis le diable l'emmena, et lui montrant en un instant tous les royaumes de la terre:
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
«Je te donnerai, lui dit-il, toute cette puissance et la gloire de ces royaumes, car elfe m'a été livrée, et je la donne à qui je veux.
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
Donc, prosterne-toi en adoration devant moi et tout cela est à toi.»
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
Et Jésus lui fit cette réponse: «Il est écrit: «Tu adoreras le Seigneur ton Dieu et c'est à lui seul que tu rendras un culte.»
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
Le menant à Jérusalem, le diable le plaça sur le faîte du Temple et lui dit: «Si tu es Fils de Dieu, jette-toi d'ici en bas,
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
car il est écrit: «A ses anges il donnera l'ordre de te garder
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
Et de te soutenir de leurs mains, De peur que ton pied ne se heurte contre une pierre.»
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Jésus lui répondit par ces mots: «Il est dit: «Tu ne tenteras point le Seigneur ton Dieu.»
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
Toute espèce de tentation étant achevée, te diable s'éloigna de lai, jusqu'à une autre occasion.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
Puissant par l'Esprit, Jésus retourna en Galilée; sa renommée se répandit dans toute la contrée;
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
il enseignait dans les synagogues du pays et tous célébraient ses louanges.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
Étant allé à Nazareth, où il avait été élevé, il entra dans la synagogue le jour du sabbat, selon sa coutume, et il se leva pour faire la lecture.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
On lui présenta le livre du prophète Ésaïe. Il l'ouvrit et trouva un passage où il était écrit:
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
«L'Esprit du Seigneur est sur moi; m'a consacré par son onction pour annoncer l'Évangile aux pauvres, Il m'a envoyé pour annoncer aux captifs leur délivrance, Aux aveugles qu'ils vont recevoir la vue, Pour renvoyer les opprimés affranchis,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
Pour annoncer une année de faveur de la part du Seigneur.
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
Il ferma le livre, le rendit au servant et s'assit. Tout le monde, dans la synagogue, avait les yeux fixés sur lui.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
Il commença ainsi: «Aujourd'hui s'accomplit ce passage de l'Écriture que vous venez d'entendre...»
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
Tous lui rendaient témoignage et étaient ravis des paroles de grâce qui sortaient de sa bouche. «N'est-ce pas là, disait-on, le fils de Joseph?» —
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
«Vous irez jusqu'à m'appliquer ce proverbe, reprit-il: Médecin, guéris-toi toi-même. Tout ce que tu as fait à Capharnaüm et dont nous avons entendu parler, fais-le donc également ici même dans ta patrie.»
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
Puis il ajouta: «Je vous le dis en vérité, nul prophète n'est accepté dans sa patrie.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
Il y avait, aux jours d'Élie, ce que je vous dis là est la vérité, beaucoup de veuves en Israël, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et demi, et qu'il y eut une grande famine sur toute la terre;
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
et cependant Élie ne fut envoyé à aucune d'elles, mais bien à une veuve de Sarepta, dans le pays de Sidon.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
Il y avait aussi, en Israël, beaucoup de lépreux au temps du prophète Élisée, et cependant aucun d'eux ne fut guéri. Celui qui fut guéri ce fut un Syrien: Naaman.»
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
Ces paroles remplirent de colère tous ceux qui étaient dans la synagogue.
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
Ils se levèrent et ils le chassèrent hors de la cité; puis ils le menèrent jusqu'au sommet de la montagne sur laquelle leur ville avait été bâtie, pour le jeter en bas.
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
Mais lui, passant au, milieu d'eux, s'en alla
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
et descendit à Capharnaüm, ville de Galilée. Il y enseignait aux jours de sabbat.
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
Et ils étaient extrêmement frappés de son enseignement, car sa parole était pleine d'autorité
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
Dans la synagogue il y avait un homme possédé de l'Esprit d'un démon impur. Il se mit à jeter de grands cris:
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
«Ah! qu'y a-t-il entre nous et toi, Jésus de Nazareth? Tu es venu pour nous perdre; je sais qui tu es: le Saint de Dieu!»
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
Jésus alors le menaça: «Tais-toi, dit-il, sors de cet homme!» Le renversant par terre au milieu de l'assemblée, le démon sortit de lui sans lui faire aucun mal.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
Tous furent terrifiés, et ils se parlaient les uns aux autres: «Qu'est-ce donc, disaient-ils, que cette parole? Il commande avec autorité et puissance aux Esprits impurs, et ils sortent!»
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
Dans tout le pays environnant il n'était bruit que de lui.
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
En sortant de la synagogue, il entra dans la maison de Simon. Or, la belle-mère de Simon était malade d'une forte fièvre. On implora Jésus en sa faveur.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
Il se pencha vers elle, commanda à la fièvre, et la fièvre disparut. Immédiatement cette femme se leva et se mit à les servir.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
Après le coucher du soleil, tous ceux qui avaient des malades, quels que fussent leurs maux, les lui amenèrent. Imposant les mains à chacun d'eux, Jésus les guérit.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
Des démons sortaient aussi d'un grand nombre, en s'écriant: «Tu es le Fils de Dieu!» Mais il les menaçait et leur défendait de parler ainsi; car ils savaient qu'il était le Christ.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
Lorsqu'il fit jour, il sortit et s'en alla dans un lieu solitaire. Les multitudes se mirent à sa recherche; elles arrivèrent jusqu'à, lui et elles le retenaient, ne voulant point qu'il les quittât.
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
Mais il leur dit: «Il me faut annoncer dans d'autres villes aussi l'Évangile du Royaume de Dieu, car c'est pour cela que j'ai été envoyé.»
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
Et il prêchait dans les synagogues de la Galilée.