< Luka 4 >

1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
Now Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the wilderness,
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
where he continued forty days, and was tempted by the devil. Having eaten nothing all that time, when it was ended he was hungry:
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
and the devil said to him, If thou be God's Son, command this stone to become bread.
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
Jesus answered him, saying, It is written, "Man does not live by bread only, but by whatever God pleases."
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
Then the devil, having brought him to the top of a high mountain, showed him all the kingdoms of the world in an instant,
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
and said to him, All this power and glory I will give thee; for it is delivered to me, and to whomsoever I will, I give it;
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
if, therefore, thou wilt worship me, it shall all be thine.
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
Jesus answering, said, It is written, "Thou shalt worship the Lord thy God, and shalt serve him only."
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
Then he brought him to Jerusalem, and placing him on the battlement of the temple, said to him, If thou be God's Son, throw thyself down hence;
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
for it is written, "He will give his angels charge concerning thee, to keep thee;
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
and, in their arms they shall uphold thee, lest thou dash thy foot against a stone."
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Jesus answered, It is said, "Thou shalt not put the Lord thy God to the proof."
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
When the devil had ended all the temptation, he departed from him for a time.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
Then Jesus, by the impulse of the Spirit, returned to Galilee, and his renown spread throughout the whole country,
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
and he taught in their synagogues with universal applause.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
Being come to Nazareth, where he had been brought up, he entered the synagogue, as his custom was, on the Sabbath day, and stood up to read.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
And they put into his hands the book of the Prophet Isaiah, and having opened the book, he found the place where it is written,
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
"The Spirit of the Lord is upon me, inasmuch as he has anointed me to publish glad tidings to the poor, to announce liberty to the captives, and recovery of sight to the blind, to release the oppressed,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
to proclaim the year of acceptance with the Lord."
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
And having closed the book, and returned it to the servant, he sat down. And the eyes of all in the synagogue were fixed upon him.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
And he began with saying to them, This very day, the scripture which you have just now heard, is fulfilled.
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
And all extolled him; but being astonished at the gracious words which he uttered, they said, Is not this Joseph's son?
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
He said to them, You will doubtless apply to me this proverb, "Physician, cure yourself." Do as great things here in your own country, as we hear you have done in Capernaum.
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
But in fact, added he, No prophet was ever well received in his own country.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
I tell you of a truth, there were many widows in Israel in the days of Elijah, when heaven was shut up for three years and a half, so that there was great famine throughout all the land;
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
yet to none of them was Elijah sent, but to a widow in Sarepta, of Sidonia.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
There were likewise many lepers in Israel, in the days of Elisha the prophet; and Naaman the Syrian was cleansed, but none of those.
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
On hearing this, the whole synagogue were enraged,
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
and breaking up, drove him out of the city, and brought him to the brow of the mountain on which their city was built, that they might throw him down headlong.
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
But he, passing through the midst of them, went away.
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
Then he came to Capernaum, a city of Galilee, and taught them on the Sabbath.
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
And they were struck with awe at his manner of teaching; for he spoke with authority.
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
Now there was in the synagogue a man possessed by the spirit of an unclean demon, who roared out, saying,
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
Ah! Jesus of Nazareth, what hast thou to do with us? Art thou come to destroy us? I know who thou art--the Holy One of God.
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
And Jesus rebuked him, saying, Be silent, and come out of him. On this, the demon, having thrown him into the middle of the assembly, came out without harming him.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
And they were all in amazement, and said one to another, What does this mean, that with authority and power he command the unclean spirits, and they come out?
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
From that time, his fame was published in every corner of the country.
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
When he was gone out of the synagogue, he entered the house of Simon, whose wife's mother had a violent fever, and they entreated him on her behalf.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
Jesus, standing near her, rebuked the fever, and it left her, and she instantly arose, and served them.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
After sunset, all they who had any sick, of whatever kind of disease, brought them to him; and he, laying his hands on every one, cured them.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
Demons also came out of many, crying out, Thou art the Son of God. But he rebuked them, and would not allow them to speak, because they knew that he was the Messiah.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
When it was day, he retired into a desert place; and the multitude sought him out, and came to him, and urged him not to leave them;
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
but he said to them, I must publish the good tidings of the Reign of God in other cities also, because for this purpose I am sent.
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
Accordingly, he made this publication in the synagogues of Galilee.

< Luka 4 >