< Luka 3 >

1 Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
In the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar—while Pontius Pilate was governor of Judea, Herod was tetrarch of Galilee, his brother Philip was tetrarch of the region of Ituraea and Trachonitis, and Lysanias was tetrarch of Abilene,
2 na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
during the high priesthood of Annas and Caiaphas—the word of God came to John son of Zechariah in the wilderness.
3 Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
He went into all the region around the Jordan, preaching a baptism of repentance for the forgiveness of sins.
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
As it is written in the book of the words of Isaiah the prophet, “A voice of one calling out in the wilderness, 'Make ready the way of the Lord, make his paths straight.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
Every valley will be filled, and every mountain and hill will be made low, and the crooked roads will be made straight, and the uneven places will be built into roads,
6 Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
and all flesh will see the salvation of God.'”
7 Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
So John said to the crowds who were coming out to be baptized by him, “You offspring of vipers! Who warned you to run away from the wrath that is coming?
8 Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
Therefore, produce fruits that are worthy of repentance, and do not begin to say within yourselves, 'We have Abraham for our father,' for I tell you that God is able to raise up children for Abraham from these stones.
9 Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
Even now the ax is set against the root of the trees. So every tree that does not produce good fruit is chopped down and thrown into the fire.”
10 Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
Then the crowds kept asking him, saying, “What then are we to do?”
11 Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
He answered and said to them, “If someone has two tunics, he should share it with a person who has none, and the one having food should do the same.”
12 Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
Tax collectors also came to be baptized, and they said to him, “Teacher, what must we do?”
13 Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
He said to them, “Do not collect more money than you have been ordered to collect.”
14 Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
Some soldiers also asked him, saying, “What about us? What must we do?” He said to them, “Do not take money from anyone by force, and do not accuse anyone falsely. Be content with your wages.”
15 Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
Now as the people were eagerly expecting the Christ to come, everyone was wondering in their hearts concerning John, whether he might be the Christ.
16 Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
John answered by saying to them all, “As for me, I baptize you with water, but someone is coming who is more powerful than I, and I am not worthy even to untie the strap of his sandals. He will baptize you with the Holy Spirit and with fire.
17 Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
His winnowing fork is in his hand to thoroughly clear off his threshing floor and to gather the wheat into his storehouse. But he will burn up the chaff with fire that can never be put out.”
18 Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
With many other exhortations also, John preached good news to the people.
19 Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
When Herod the tetrarch had been reproved for marrying his brother's wife Herodias, and for all the other evil things that Herod had done,
20 Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
he added this to them all, that he locked John up in prison.
21 Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
Now it came about, when all the people were baptized, Jesus also was baptized, and while he was praying, the heavens opened,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
and the Holy Spirit in bodily form came down on him like a dove, and a voice came from heaven, “You are my Son, whom I love. I am pleased with you.”
23 Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
When Jesus began his ministry, he was about thirty years of age. He was the son (as it was assumed) of Joseph, the son of Heli,
24 mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
the son of Matthat, the son of Levi, the son of Melchi, the son of Jannai, the son of Joseph.
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
Joseph was the son of Mattathias, the son of Amos, the son of Nahum, the son of Esli, the son of Naggai,
26 mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
the son of Maath, the son of Mattathias, the son of Semein, the son of Josech, the son of Joda.
27 mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
Joda was the son of Joanan, the son of Rhesa, the son of Zerubbabel, the son of Salathiel, the son of Neri,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
the son of Melchi, the son of Addi, the son of Cosam, the son of Elmadam, the son of Er,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
the son of Joshua, the son of Eliezer, the son of Jorim, the son of Matthat, the son of Levi.
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
Levi was the son of Simeon, the son of Judah, the son of Joseph, the son of Jonam, the son of Eliakim,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
the son of Melea, the son of Menna, the son of Mattatha, the son of Nathan, the son of David,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
the son of Jesse, the son of Obed, the son of Boaz, the son of Salmon, the son of Nahshon.
33 mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
Nahshon was the son of Amminadab, the son of Admin, the son of Arni, the son of Hezron, the son of Perez, the son of Judah,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
the son of Jacob, the son of Isaac, the son of Abraham, the son of Terah, the son of Nahor,
35 mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
the son of Serug, the son of Reu, the son of Peleg, the son of Eber, the son of Shelah.
36 mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
Shelah was the son of Cainan, the son of Arphaxad, the son of Shem, the son of Noah, the son of Lamech,
37 mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
the son of Methuselah, the son of Enoch, the son of Jared, the son of Mahalaleel, the son of Cainan,
38 mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.
the son of Enos, the son of Seth, the son of Adam, the son of God.

< Luka 3 >