< Luka 24 >
1 Mapema sana siku ya kwanza ya juma, walikuja kaburini, wakileta manukato ambayo walikuwa wameyaandaa.
Now on the first day of the week, very early in the morning, they came to the tomb, bringing the spices which they had prepared.
2 Wakakuta jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
And they found the stone rolled away from the tomb;
3 Wakaingia ndani, lakini hawakuukuta mwili wa Bwana Yesu.
and on entering they found not the body of the Lord Jesus.
4 Ilitokea kwamba, wakati wamechanganyikiwa kuhusu hili, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi ya kung'aa.
And it came to pass, as they were much perplexed about this, lo! two men stood by them in glittering apparel;
5 Wanawake wakiwa wamejaa hofu na wakiinamisha nyuso zao chini, wakawaambia wanawake, “Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
and when they were terrified, and bowed their faces to the earth, the men said to them, Why seek ye the living among the dead?
6 Hayupo hapa, ila amefufuka! Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa angali Galilaya,
He is not here, but hath risen. Remember how be spoke to you while yet in Galilee,
7 akisema kwamba Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe, na siku ya tatu, afufuke tena.”
saying, The Son of man must be delivered up into the hands of sinners, and be crucified, and rise again on the third day.
8 Wale wanawake wakakumbuka maneno yake,
And they remembered his words.
9 na wakarudi kutoka kaburini na wakawaambia mambo haya yote wale kumi na moja na wengine wote.
And returning from the tomb, they told all these things to the eleven, and to all the rest.
10 Basi Maria Magdalena, Joana, Maria mama wa Yakobo, na wanawake wengine pamoja nao wakatoa taarifa hizi kwa mitume.
It was Mary the Magdalene, and Joanna, and Mary the mother of James; and the other women with them told these things to the apostles.
11 Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaha tu kwa mitume, na hawakuwaamini wale wanawake.
And these words seemed to them as an idle tale, and they did not believe them.
12 Hata hivyo Petro aliamka, na akakimbia kuelekea kaburini, na akichungulia na kuangalia ndani, aliona sanda peke yake. Petro kisha akaondoka akaenda nyumbani kwake, akistaajabu nini ambacho kimetokea.
13 Na tazama, wawili miongoni mwao walikuwa wakienda siku hiyo hiyo katika kijiji kimoja kiitwacho Emmau, ambacho kilikuwa maili sitini kutoka Yerusalemu.
And lo! two of them were going the same day to a village called Emmaus, distant a hundred and sixty furlongs from Jerusalem.
14 Wakajadiliana wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotokea.
And they were conversing together about all those things which had taken place.
15 Ikatokea kwamba, wakati walipokuwa wakijadiliana na kuulizana maswali, Yesu akasogea karibu akaambatana nao.
And it came to pass, while they were conversing and reasoning, that Jesus himself drew near, and went with them.
16 Lakini macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye.
But their eyes were restrained from knowing him.
17 Yesu akawaambia, “Nini ambacho ninyi wawili mnakiongelea wakati mnatembea?” Wakasimama pale wakionekana na huzuni.
And he said to them, What discourse is this which ye have one with another, as ye are walking? And they stood sad.
18 Mmoja wao, jina lake Cleopa, akamjibu, “Je wewe ni mtu pekee hapa Yerusalemu ambaye hajui mambo yaliyotokea huko siku hizi?”
And one, whose name was Cleopas, answering said to him, Art thou the only sojourner in Jerusalem that doth not know the things which have come to pass there in these days?
19 Yesu akawaambia, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo kuhusu Yesu Mnazareti, ambaye alikuwa nabii, muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote.
And he said to them, What things? And they said to him, The things relating to Jesus the Nazarene, who was a prophet mighty in word and deed before God and all the people;
20 Na kwa jinsi ambayo wakuu wa makuhani na viongozi wetu walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha.
and how the chief priests and our rulers delivered him up to be condemned to death, and crucified him.
21 Lakini tulitumaini kwamba yeye ndiye atakaye waweka huru Israeli. Ndiyo, mbali na haya yote, sasa ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
But we are hoping that it is he who is to redeem Israel; moreover, besides all this, it is the third day since these things were done.
22 Lakini pia, baadhi ya wanawake kutoka katika kundi letu walitushangaza, baada ya kuwapo kaburini asubuhi na mapema.
And furthermore certain women of our company have amazed us; for going early to the tomb,
23 Walipoukosa mwili wake, wakaja, wakisema kwamba waliona pia maono ya malaika waliosema kwamba yu hai.
they did not find his body, and came, saying that they had even seen a vision of angels, who said that he was alive.
24 Baadhi ya wanaume ambao walikuwa pamoja nasi walienda kaburini, na kukuta ni kama vile wanawake walivyosema. Lakini hawakumuona yeye.”
And some of those who were with us went to the tomb, and found it to be as the women had said; but him they saw not.
25 Yesu akawaambia, “Ninyi watu wajinga na wenye mioyo mizito ya kuamini yote ambayo manabii wamesema!
And he said to them, O dull of apprehension, and slow of heart to believe all that the Prophets have spoken!
26 Je haikuwa lazima Yesu kuteseka kwa mambo haya, na kuingia katika utukufu wake?”
Was it not necessary that the Christ should suffer these things, and enter into his glory?
27 Kisha kuanzia kutoka kwa Musa na manabii wote, Yesu akawatafsiria mambo yanayomuhusu yeye katika maandiko yote.
And beginning with Moses and all the Prophets he explained to them in all the Scriptures the things concerning himself.
28 Walipokaribia kile kijiji, huko walikokuwa wakienda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea mbele.
And they drew near to the village whither they were going; and he made as though he would go further.
29 Lakini walimlazimisha, wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana inaelekea jioni na siku ni kama imeisha.” Hivyo Yesu akaingia kwenda kukaa nao.
But they constrained him, saying, Abide with us, for it is towards evening, and the day is now far spent. And he went in to stay with them.
30 Ilitokea kwamba, wakati amekaa nao kula, alichukua mkate, akaubariki, na kuuvunja, akawapa.
And it came to pass, as he was at table with them, that he took the bread, and blessed it, and broke and gave it to them.
31 Kisha macho yao yakafunguliwa, wakamjua, na akatoweka ghafla mbele ya macho yao.
And their eyes were opened, and they knew him; and he vanished out of their sight.
32 Wakasemezana wao kwa wao, “Hivi mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipoongea nasi njiani, wakati alipotufungulia maandiko?”
And they said one to another, Did not our hearts burn within us while he talked with us on the way, while he opened to us the Scriptures?
33 Wakanyanyuka saa hiyo hiyo, na kurudi Yerusalemu. Wakawakuta wale kumi na mmoja wamekusanyika pamoja, na wale waliokuwa pamoja nao,
And they rose up the same hour, and returned to Jerusalem; and they found the eleven and those who were with them gathered together,
34 wakisema, “Bwana amefufuka kwelikweli, na amemtokea Simoni.”
saying, The Lord hath risen indeed, and hath appeared to Simon.
35 Hivyo wakawaambia mambo yaliyotokea njiani, na namna Yesu alivyodhihirishwa kwao katika kuumega mkate.
And they told what had happened on the way, and how he became known to them in the breaking of the bread.
36 Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
And while they were thus speaking, he himself stood in the midst of them.
37 Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
But they were terrified and affrighted, and supposed that they beheld a spirit.
38 Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
And he said to them, Why are ye troubled? and why do doubts arise in your hearts?
39 Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
See my hands and my feet, that it is I myself. Handle me, and see; for a spirit hath not flesh and bones, as ye see me have.
40 Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
41 Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
And while they still disbelieved for joy, and wondered, he said to them, Have ye anything here to eat?
42 Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
And they gave him a piece of a broiled fish.
43 Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
And he took and ate it before them.
44 Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
And he said to them, These are my words which I spoke to you, while I was yet with you, that all things must be fulfilled which are written in the Law of Moses, and the Prophets, and the Psalms, concerning me.
45 Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
Then he opened their understanding, that they might understand the Scriptures.
46 Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
And he said to them, Thus it is written, that the Christ should suffer, and should rise from the dead on the third day,
47 Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
and that repentance for the remission of sins should be preached in his name among all the nations, beginning at Jerusalem.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
Ye are witnesses of these things.
49 Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
And I send forth upon you that which hath been promised by my Father; but do ye tarry in the city, until ye are endued with power from on high.
50 Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
And he led them out as far as to Bethany; and he lifted up his hands and blessed them.
51 Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
And it came to pass, while he blessed them, that he parted from them.
52 Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
And they returned to Jerusalem with great joy,
53 Waliendelea kuwepo hekaluni, wakimbariki Mungu.
and were continually in the temple, praising God.