< Luka 24 >

1 Mapema sana siku ya kwanza ya juma, walikuja kaburini, wakileta manukato ambayo walikuwa wameyaandaa.
Very early on the first day of the week, the women went to the tomb, taking the spices they'd prepared.
2 Wakakuta jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
They found that the stone had been rolled away from the entrance to the tomb,
3 Wakaingia ndani, lakini hawakuukuta mwili wa Bwana Yesu.
but when they went in they didn't find the body of the Lord Jesus.
4 Ilitokea kwamba, wakati wamechanganyikiwa kuhusu hili, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi ya kung'aa.
While they were wondering what was going on, two men suddenly appeared dressed in clothes that shone brilliantly.
5 Wanawake wakiwa wamejaa hofu na wakiinamisha nyuso zao chini, wakawaambia wanawake, “Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
The women were terrified and bowed down, their faces on the ground. They said to the women, “Why are you looking for someone who is alive among the dead?
6 Hayupo hapa, ila amefufuka! Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa angali Galilaya,
He's not here; he's risen from the dead! Remember what he told you while you were still in Galilee:
7 akisema kwamba Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe, na siku ya tatu, afufuke tena.”
‘The Son of man must be betrayed into the hands of evil men, be crucified, and on the third day rise again.’”
8 Wale wanawake wakakumbuka maneno yake,
Then they remembered what he'd said.
9 na wakarudi kutoka kaburini na wakawaambia mambo haya yote wale kumi na moja na wengine wote.
When they returned from the tomb they reported all that had happened to the eleven disciples and to all the others.
10 Basi Maria Magdalena, Joana, Maria mama wa Yakobo, na wanawake wengine pamoja nao wakatoa taarifa hizi kwa mitume.
Those who told the apostles what had happened were Mary Magdalene, Joanna, Mary the mother of James, and other women with them.
11 Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaha tu kwa mitume, na hawakuwaamini wale wanawake.
But it seemed like nonsense to them, so they didn't believe the women.
12 Hata hivyo Petro aliamka, na akakimbia kuelekea kaburini, na akichungulia na kuangalia ndani, aliona sanda peke yake. Petro kisha akaondoka akaenda nyumbani kwake, akistaajabu nini ambacho kimetokea.
However, Peter got up and ran to the tomb. Bending down, he looked in and saw only the linen grave-clothes. So he went back home, wondering what had happened.
13 Na tazama, wawili miongoni mwao walikuwa wakienda siku hiyo hiyo katika kijiji kimoja kiitwacho Emmau, ambacho kilikuwa maili sitini kutoka Yerusalemu.
The same day two disciples were on their way to a village called Emmaus, about seven miles from Jerusalem.
14 Wakajadiliana wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotokea.
They were talking about all that had happened.
15 Ikatokea kwamba, wakati walipokuwa wakijadiliana na kuulizana maswali, Yesu akasogea karibu akaambatana nao.
As they discussed and debated, Jesus came up and fell into step with them.
16 Lakini macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye.
But they were kept from recognizing him.
17 Yesu akawaambia, “Nini ambacho ninyi wawili mnakiongelea wakati mnatembea?” Wakasimama pale wakionekana na huzuni.
“What are you discussing as you walk along?” he asked them. They stopped, their faces sad.
18 Mmoja wao, jina lake Cleopa, akamjibu, “Je wewe ni mtu pekee hapa Yerusalemu ambaye hajui mambo yaliyotokea huko siku hizi?”
One of them, called Cleopas, replied, “Are you just visiting Jerusalem? You must be the only person who doesn't know the things that have happened in the past few days.”
19 Yesu akawaambia, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo kuhusu Yesu Mnazareti, ambaye alikuwa nabii, muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote.
“What things?” Jesus asked. “About Jesus of Nazareth,” they replied. “He was a prophet who spoke powerfully and performed great miracles before God and all the people.
20 Na kwa jinsi ambayo wakuu wa makuhani na viongozi wetu walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha.
But our high priests and leaders handed him over to be condemned to death, and they crucified him.
21 Lakini tulitumaini kwamba yeye ndiye atakaye waweka huru Israeli. Ndiyo, mbali na haya yote, sasa ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
We had hoped he was the one who was going to rescue Israel. It's been three days now since all this happened.
22 Lakini pia, baadhi ya wanawake kutoka katika kundi letu walitushangaza, baada ya kuwapo kaburini asubuhi na mapema.
But then some of the women in our group surprised us.
23 Walipoukosa mwili wake, wakaja, wakisema kwamba waliona pia maono ya malaika waliosema kwamba yu hai.
At dawn they went to the tomb and they didn't find his body. They came back saying that they'd seen a vision of angels who told them he's alive.
24 Baadhi ya wanaume ambao walikuwa pamoja nasi walienda kaburini, na kukuta ni kama vile wanawake walivyosema. Lakini hawakumuona yeye.”
Some of us went to the tomb, and found it just as the women said—but they didn't see him.”
25 Yesu akawaambia, “Ninyi watu wajinga na wenye mioyo mizito ya kuamini yote ambayo manabii wamesema!
Jesus told them, “You're so dull! How slow you are to trust in all that the prophets said!
26 Je haikuwa lazima Yesu kuteseka kwa mambo haya, na kuingia katika utukufu wake?”
Didn't the Messiah have to suffer before he could enter into his glory?”
27 Kisha kuanzia kutoka kwa Musa na manabii wote, Yesu akawatafsiria mambo yanayomuhusu yeye katika maandiko yote.
Then, starting with Moses and all the prophets, he explained to them everything that was said in Scripture about himself.
28 Walipokaribia kile kijiji, huko walikokuwa wakienda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea mbele.
As they approached the village they were going to, Jesus made it seem as if he was going farther.
29 Lakini walimlazimisha, wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana inaelekea jioni na siku ni kama imeisha.” Hivyo Yesu akaingia kwenda kukaa nao.
But they urged him, saying, “Please come and stay with us. It's getting late—the day is almost over.” So he went to stay with them.
30 Ilitokea kwamba, wakati amekaa nao kula, alichukua mkate, akaubariki, na kuuvunja, akawapa.
When he sat down to eat with them, he took the bread and gave thanks, broke it, and gave it to them.
31 Kisha macho yao yakafunguliwa, wakamjua, na akatoweka ghafla mbele ya macho yao.
Their eyes were opened, and they recognized him. Then he disappeared from view.
32 Wakasemezana wao kwa wao, “Hivi mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipoongea nasi njiani, wakati alipotufungulia maandiko?”
The two disciples said to each other, “Weren't our thoughts on fire when he spoke to us, as he explained the Scriptures to us?”
33 Wakanyanyuka saa hiyo hiyo, na kurudi Yerusalemu. Wakawakuta wale kumi na mmoja wamekusanyika pamoja, na wale waliokuwa pamoja nao,
They got up right away and returned to Jerusalem. There they found the eleven disciples and those who were with them meeting together,
34 wakisema, “Bwana amefufuka kwelikweli, na amemtokea Simoni.”
who said, “The Lord has really risen again! He has appeared to Simon.”
35 Hivyo wakawaambia mambo yaliyotokea njiani, na namna Yesu alivyodhihirishwa kwao katika kuumega mkate.
Then those who had just arrived explained to the other disciples what had happened to them on the road, and how they had recognized Jesus when he broke bread.
36 Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
While they were talking, Jesus himself stood among them, and said, “Peace to you!”
37 Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
They were startled and afraid, thinking they were seeing a ghost.
38 Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
“Why are you frightened? Why are you doubting?” he asked them.
39 Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
“Look at my hands and my feet—you can see it's me. Touch me and you'll be certain, for a spirit doesn't have flesh and bones, as you see I have.”
40 Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
Having said this, he showed them his hands and feet.
41 Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
But they still couldn't believe it because they were so elated and amazed. He asked them, “Do you have anything to eat?”
42 Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
They gave him a piece of cooked fish,
43 Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
and he took it and ate it in front of them.
44 Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
Then Jesus said to them, “This is what I explained to you while I was still with you. Everything written about me in the law of Moses, the prophets, and the psalms, had to be fulfilled.”
45 Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
Then he opened their minds so they were able to understand the Scriptures.
46 Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
He told them, “It was written like this: the Messiah would suffer and rise from the dead on the third day, and in his name
47 Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
repentance for the forgiveness of sins would be preached to all nations, beginning in Jerusalem.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
You are witnesses of all this.
49 Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
Now I'm going to send you what my Father promised—but wait in the city until you receive power from heaven.”
50 Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
Then he led them out until they were near Bethany, and lifting up his hands, he blessed them.
51 Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
While he was blessing them, he left them, and was taken up to heaven.
52 Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
They worshiped him, and then they returned to Jerusalem full of joy.
53 Waliendelea kuwepo hekaluni, wakimbariki Mungu.
They spent all their time in the Temple praising God.

< Luka 24 >