< Luka 23 >
1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Msambi wa vandu voha vevakonganiki pala, vakayima na kumpeleka Yesu palongolo ya Pilatu,
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
Vakatumbula kumtakila vakajova, “Tamkolili mundu uyu avayaganisa vandu vitu na kavili akuvabesa vandu vakotoka kumpela kodi nkosi wa ku Loma na kujikemela ati mwene ndi Kilisitu Msangula Nkosi.”
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
Pilatu akamkota Yesu, “Veve ndi Nkosi wa Vayawudi?” Yesu akamyangula, “Veve wamwene ndi ujovili, veve Nkosi wa Vayawudi.”
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Pilatu akavajovela vakulu va kuteta na msambi wa vandu, “Nakuchiwona chindu cheabudili mundu uyu.”
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
Nambu vene vakajova chinganga, “Akuvakulukisa vandu kwa mawuliwu gaki mumulima woha wa Yudea, atumbwili ku Galilaya na hinu avi penapa.”
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
Pilatu peayuwini genago, akakota, “Wu, mundu uyu ndi mkolonjinji wa ku Galilaya?”
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
Peamanyili Yesu ihuma mumulima wewilongoswa na Helodi, ndi ampeliki kwa Helodi muni lukumbi lwenulo mewa avi ku Yelusalemu.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
Helodi akavya na luheku neju peamuweni Yesu. Muni amali kuyuwana mambu ga Yesu, ndi magono gamahele anogelayi kumlola Yesu cheikita gachinamtiti.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
Helodi amkotili Yesu makotesi gamahele, nambu Yesu nakumyangula chindu.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
Vakulu va kuteta na vawula va malagizu ga Chapanga geampeli Musa vakayima kulongolo na kumtakila chinganganga.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
Helodi pamonga na vamanjolinjoli vaki vakampeli soni Yesu na kumvevesa, kangi vakamuwalika ligwanda la unkosi na kumuwuyisa kwa Pilatu.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
Magono gamumbele Helodi na Pilatu vatamanila cha umakoko, nambu kutumbula ligono lenilo vakavya vankozi.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
Pilatu akavakemele pamonga, Vamteta vakulu na vachilongosi va Chiyawudi na vandu,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
akavajovela, “Mumletili mundu uyu mwijova akuvayaganisa vandu. Hinu myuwanila! Nimali kulola muhalu uwu palongolo yinu kawaka chindu cheabudili mu mambu goha gemumtakili.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
Lepi nene ndu, nambu hati Helodi mewa, amuwuyisi kavili, ndava kawaka chindu cheabudili cheachiwene, kwa mundu uyu hati ahamuliwa lifwa.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Yati nilagazila atovewa michapilu ya miinga, na kumulekekesa.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
Mselebuko wa Pasaka, Pilatu yamganili kuvadindulila mundu mmonga kuhuma muchifungu.”
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
Nambu voha vakaywanga, “Mkoma mundu uyu! Utidindulilayi Balaba!”
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
Balaba asopiwi muchifungu ndava ya kukulukisa vandu muchitutu na muchitutu chenicho mundu mmonga akomiwi.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Pilatu aganili kumulekekesa Yesu, ndi akalongela nawu kavili vandu vevamtakili Yesu.
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
Nambu vene vakaywanga vakajova, “Mvambayi pamsalaba, mvambayi pamsalaba!”
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
Pilatu akavajovela mala ya datu, “Chindu gani cheabudili mundu uyu? Nichiwona lepi chindu cheabudili hati ahamuliwa kukomiwa! Nene yati nilagiza atovewayi michapilu na kumlekekesa.”
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
Nambu vene vakayonjokesa kuywanga neju, Yesu yiganikwa avambiwayi pamsalaba, lwami zavi pamwishu zayuwaniki.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
Hinu, Pilatu akahamula gahengeka.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
Akamulekekesa kuhuma muchifungu yula mweakukingiwi ndava ya kuvya pamonga na vandu muchitutu na kukoma mundu mmonga, ndi akamgotola Yesu vamukita ngati chevigana.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
Pevavi mukupeleka, vakakonganeka na mundu mmonga liina laki Simoni mkolonjinji wa Kulene, mweahumayi kumgunda waki, ndi vakamkamula na kumgegesa msalaba wula mumbele ya Yesu.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
Vandu msambi kwa msambi, wamulandili, pagati yavi vavi vadala vevamuvembelayi Yesu ndava ya lipyanda.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
Yesu akavang'anamukila, akajova, “Vamawu va Yelusalemu! Mkoto kunivembela nene, nambu mujivembela mwavene na vana vinu.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
Muni chakaka walabwela lukumbi, yati mwijova, ‘Mbanga yavi vadala, vangali vana na vangavaleke, amala vanganyong'esa vana!’
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Lukumbi lwenulo, yati vandu vakuvijovela vidunda, mutigwilila na tudunda, ‘Mutigubika!’
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
Ngati vandu vakunikitila nene chenicho mwenivili ngati mkongo uvisi, yati yivya wuli kwa nyenye mwemuvi ngati mkongo uyumu?”
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Mewa vavatoli vandu vangi vavili vanyagaji vavapeliki, kukomiwa pamonga na Yesu.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
Pavahikili pandu pepikemelawa, “Libangu la Mutu,” Ndi vakamvamba Yesu pamsalaba pamonga na vanyagaji vavili vala mmonga upandi waki wa kulyela na yungi upandi wa kumangeya.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
Yesu akajova, “Dadi, valekekesa, muni nakumanya chevikita.” Kangi, vakagavana nyula zaki kwa kuhagula kwa gudugudu.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
Vandu vayimili kulolokesa kuni vakulu va Vayawudi chevamvevisi vijova, “Avasangwili vangi, hinu ajisangula mwene ngati mwene ndi Kilisitu mwehaguliwi na Chapanga!”
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
Manjolinjoli mewa vamvevisi, vamhambili Yesu na kumpela divayi yivavanu,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
Vakumjovela, “Ngati chakaka veve ndi Nkosi wa Vayawudi, ujisangula wamwene!”
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
Panani ya msalaba vavikili chibawu chechayandikiwi, “Mwenuyu ndi Nkosi wa Vayawudi.”
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
Mmonga wa vanyagaji vala vevavambiwi pamsalaba akamliga Yesu, akajova “Wu, lepi chakaka kuvya veve ndi Kilisitu Msangula? Jisangula wamwene, utisangula na tete!”
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
Nambu mnyagaji yungi yula, akamuywangila muyaki akamjovela, “Veve ukumuyogopa lepi Chapanga hati padebe? Veve uhamuliwi mewawa.
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
Veve na nene yikutigana tihamuliwa ndava ya kunyaga kwitu. Nambu mundu uyu kawaka hati chimonga cheabudili.”
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
Kangi akamjovela Yesu, “Veve Yesu! Ukoto kunikosiwa peuyingila Munkosi waku!”
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Yesu akamyangula, “Chakaka nikujovela lelu yati tivya na nene kupaladiso.”
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
Kutumbula saa sita muhi, chitita chikagubika mulima woha mbaka saa tisa,
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
na lilanga likakotoka kulangasa na lipazia lelakovikwi mu Nyumba ya Chapanga likapapuka vipandi vivili.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
Yesu akavemba kwa lwami luvaha, “Dadi! Mumawoko gaku nigotola mpungu wangu!” Akadumuka mpungu.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Mkulu wa manjolinjoli yula peagawene gegahumalili, akamulumba Chapanga akajova, “Chakaka mundu uyu avi mbwina!”
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
Na vandu voha vevakonganiki penapo ndava ya lijambu lenilo pavagawene gegahumalili gala, vakawuya kunyumba zavi, kuni vakujitova nganga cha ngolongondi.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
Vankozi vaki voha pamonga na vadala vealongosini nawu kuhuma ku Galilaya, vayimili cha kutali kulola mambu genago.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
Kwavi na mundu mmonga liina laki Yosefu, avi mmonga wa vachilongosi wa libanji likulu la Vayawudi. Avi mundu mbwina na kukita geigana Chapanga,
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
mwene nakuyidakilana gevapangili na kugakita vachilongosi vayaki va libanji likulu la Vayawudi. Yosefu avi mkolonjinji wa Alimatei, ndi avi mukulindila kubwela kwa Unkosi wa Chapanga.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
Mundu mwenuyo akahamba kwa Pilatu kumuyupa atola higa ya Yesu.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
Akayihulusa higa kuhuma pamsalaba, akayitindisila nyula ya msopi na kuvika mulitinda lelahongoliwi pamhana ya litalau, lavi langavikiwa mundu.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
Lavi ligono la kutendelekeha, Ligono la Kupumulila ndi latumbukana.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
Vadala vevalongosini na Yesu kuhuma ku Galilaya vakamulanda Yosefu na kuliwona litinda na higa ya Yesu cheuvikiwi.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
Kangi vakawuya kunyumba, vakatendelekela mahuta geginungalila bwina ga kunyala higa ya Yesu. Ligono la Kupumulila vapumulili ngati malagizu ga Chapanga geampeli Musa chegilagiza.