< Luka 23 >

1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
Then the whole assembly arose and led Jesus to Pilate.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
They began to accuse him, saying, “We found this man perverting the nation and forbidding us to pay taxes to Caesar, declaring himself to be Christ, a king.”
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
So Pilate asked Jesus, “Are yoʋ the king of the Jews?” Jesus answered him, “Yoʋ have said it yoʋrself.”
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Then Pilate said to the chief priests and the crowd, “I find no fault in this man.”
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they kept insisting, “He stirs up the people, teaching throughout all Judea. He started from Galilee and has come even to this place.”
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
When Pilate heard mention of Galilee, he asked whether the man was a Galilean.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And when he found out that Jesus was under Herod's jurisdiction, he sent him over to Herod, who was also in Jerusalem in those days.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
When Herod saw Jesus he was very glad, for he had long desired to see him, because he had heard many things about him and was hoping to see him perform some sign.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
So he questioned him at great length, but Jesus gave him no answer.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
Meanwhile, the chief priests and the scribes stood there, vehemently accusing him.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
Herod also treated him with contempt and mocked him, as did his soldiers. Then, after dressing Jesus in fine clothing, Herod sent him back to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
That very day Pilate and Herod became friends with one another; before this they had been enemies.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
Then Pilate called together the chief priests, the rulers, and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
and said to them, “You brought me this man as one who was misleading the people. And behold, after examining him before you, I have found no fault in this man with respect to the accusations you are making against him,
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
and neither has Herod, for I sent you to him. Clearly he has done nothing that deserves death.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
Therefore I will have him flogged and then release him.”
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
Now each year at the feast Pilate was obligated to release one prisoner for the people.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
So they all cried out together, “Away with this man, and release for us Barabbas!”
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
(This was a man who had been thrown into prison for an insurrection that had taken place in the city, and for murder.)
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Wishing to release Jesus, Pilate addressed them again,
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
but they kept on shouting, “Crucify, crucify him!”
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
A third time he said to them, “Why? What evil has he done? I have found in him no grounds for death. So I will have him flogged and then release him.”
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they continued insistently with loud voices, demanding that he be crucified, and their voices prevailed, along with those of the chief priests.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
So Pilate rendered his decision that their demand be granted.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
He released the man they had been asking for, who had been thrown into prison for insurrection and murder, but he handed Jesus over to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
As the soldiers led him away, they took hold of Simon, a Cyrenian man who was coming in from the countryside, and they laid on him the cross, forcing him to carry it behind Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
A great multitude of people followed along behind, including women who were mourning and lamenting for Jesus.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
But Jesus turned to them and said, “Daughters of Jerusalem, do not weep for me, but weep for yourselves and for your children.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
For behold, the days are coming when people will say, ‘Blessed are the barren, the wombs that have not given birth, and the breasts that have not nursed!’
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then they will begin to say to the mountains, ‘Fall on us!’ and to the hills, ‘Cover us!’
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
For if they do these things when the wood is green, what will happen when it is dry?”
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
Now two others, who were criminals, were also being led away to be put to death with Jesus.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
When they came to the place called the Skull, the soldiers crucified him there along with the criminals, one on his right and one on his left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
But Jesus said, “Father, forgive them, for they do not know what they are doing.” Then they cast lots to divide his garments.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
The people stood there looking on, and the rulers who were with them ridiculed him, saying, “He saved others; let him save himself if he is the Christ, the Chosen One of God.”
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
The soldiers also mocked him, coming up to him and offering him sour wine,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
saying, “If yoʋ are the king of the Jews, save yoʋrself!”
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
There was also an inscription over him written in Greek, Latin, and Hebrew letters, which read: “This is the King of the Jews.”
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
One of the criminals who was hanging there reviled him, saying, “If yoʋ are the Christ, save yoʋrself and us!”
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
But the other rebuked him, saying, “Do yoʋ not even fear God, seeing that yoʋ are under the same condemnation?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
The two of us are justly condemned, for we are receiving the appropriate punishment for the things we have done, but this man has done nothing wrong.”
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
Then he said to Jesus, “Remember me, Lord, when yoʋ come in yoʋr kingdom.”
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Jesus said to him, “Truly I say to yoʋ, today yoʋ will be with me in Paradise.”
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
Now it was about the sixth hour, and there was darkness over the whole land until the ninth hour.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
The sun was darkened, and the veil of the temple was torn down the middle.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
Then Jesus cried out with a loud voice, “Father, into yoʋr hands I commit my spirit.” After saying this, he breathed his last breath.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Now when the centurion saw what had happened, he glorified God and said, “Surely this man was righteous.”
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And when all the crowds who had gathered together for this spectacle saw what had happened, they returned home beating their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
But all those who knew Jesus stood at a distance watching these things, including the women who had followed him from Galilee.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
Now there was a good and righteous man named Joseph, who was a member of the council
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
but had not consented to their decision and action. He was from Arimathea, a town of the Jews, and was himself also waiting for the kingdom of God.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
He went to Pilate and asked for Jesus' body.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
Then he took it down, wrapped it in a linen cloth, and laid it in a tomb hewn in the rock, where no one had ever been laid.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
It was the day of Preparation, and the Sabbath was approaching.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
The women who had come with Jesus from Galilee followed along behind and saw the tomb and how his body was laid in it.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
Then they returned and prepared spices and ointments. But they rested on the Sabbath according to the commandment.

< Luka 23 >