< Luka 23 >
1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And the whole assembly of them arose, and brought him to Pilatos.
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
And they began to accuse him, saying, We have found this who deludeth our people, and forbiddeth that tribute unto Caesar we should give, saying of himself that he is the King Meshicha.
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
But Pilatos asked him, and said to him, Art thou the king of the Jihudoyee? He saith to him, Thou hast said.
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
And Pilatos said to the chief priests and to the assembly, I find no occasion against this man.
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they cried out and said, He commoveth our people while he teacheth throughout all Jihud, beginning from Galila unto this place.
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
Pilatos, however, when he heard the name of Galila, asked if the man were a Galiloya.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And when he knew that he was from the limit of the jurisdiction of Herodes, he sent him unto Herodes, because that in Urishlem he was in those days.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
And Herodes, when he saw Jeshu, was very glad; for he had desired to see him of a great time: for he had heard concerning him many things, and hoped that some sign he should see from him.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
And many words he asked him; but Jeshu gave him no answer whatever.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
And the chief priests and scribes stood and strenuously accused him.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
Then Herodes and his soldiers treated him as a fool; and when he had derided him, he dressed him in a robe of crimson, and sent him to Pilatos.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
And in that day Pilatos and Herodes were friends with each other; for before there had been enmity between them.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
And Pilatos called the chief priests and the rulers of the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
and said to them, You have brought to me this man as a perverter of your people; and, behold, I have examined him in your sight, and have found no cause in this man of all that you accuse him:
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
nor also Herodes; for I sent him unto him, and, behold, nothing worthy of death is done to him:
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
I will therefore chastise him, and dismiss him.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
For a custom had he to release to them one at the festival.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
But all the multitude cried out, saying, Take this, and release to us Baraba;
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
he who, for insurrection and murder which had been done in the city, had been thrown into the house of the chained.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
But Pilatos spake with them again, being willing to release Jeshu.
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
But they cried out, saying, Crucify him! Crucify him!
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
He the third time also said to them, Why, what evil hath this done? Cause whatever that is worthy of death, I find not in him: I will therefore chastise him, and dismiss him.
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they were urgent with a high voice, demanding that they might crucify him; and theirs and the voices of the high priests prevailed.
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
And Pilatos commanded that their requirement should be done.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
And he released to them him who, for insurrection and murder, had been thrown into the house of the chained, whom they had asked: but Jeshu he delivered to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
AND as they led him away, they laid hold on Shemun Kurinoya, who was coming from the country, and they laid on him the cross, that he might bear (it) after Jeshu.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
And there followed him much people, and those women who mourned and wailed for him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
And Jeshu turned to them, and said, Daughters of Urishlem, weep not for me, but for yourselves weep, and for your children.
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
For, behold, coming are the days in which they shall say, Blessed are the barren, and the wombs which have not borne, and the breasts that have not suckled.
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then shall they begin to say to the mountains, Fall on us! and to the heights, Cover us!
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
For if to the tree which is good they do these things, unto the dry what shall be?
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
And there went with him two others, workers of evil, to be put to death.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
And when they came to a certain place called Karkaphtha, there they crucified him, and those workers of evil, one on his right hand, and one on his left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
BUT Jeshu himself said, Father, forgive them; for they know not what they do. And they divided his garments, and cast for them lots.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
But the people stood beholding, and the rulers also, mocking him, and saying, He saved others, let him save himself, if he be the Meshicha, the Chosen of God.
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
And the soldiers also, deriding him, approaching him, and offering to him vinegar,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
said to him, If thou art the King of the Jihudoyee, save thyself.
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
And there was also an inscription which was written over him in Greek and Roman and Hebrew, THIS IS THE KING OF THE JIHUDOYEE.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
And one of those workers of evil who were hanged with him, blasphemed against him, saying, If thou art the Meshicha, deliver thyself, and deliver us also.
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
And his companion rebuked him, and said to him, Dost thou not fear (even) Aloha? for thou also art in this judgment.
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
And we righteously, forasmuch as we have been deserving, and as we are punished for that which we have done;
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
but this hath done nothing that is abominable. And he said to Jeshu, Remember me, my Lord, when thou art come into thy kingdom!
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Jeshu saith to him, Amen I say to thee, That to-day with me thou shalt be in Paradise.
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
NOW it was about six hours, and there was darkness over all the earth until nine hours.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
And the sun darkened, and rent was the vail of the temple through the midst of it.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
And Jeshu cried with a high voice, and said, My Father, in thy hands I place my spirit. This he said, and completed.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
But when the centurion saw what was done, he glorified Aloha, saying, Assuredly this was a just man.
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
And all the multitude, they who were assembled to see this, when they saw what was done, returned, smiting upon their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
And there were standing afar off all the acquaintances of Jeshu, and those women who came with him from Galila; and they saw these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
BUT a certain man, whose name was Jauseph, a senator from Rometha, a city of Jehud, a man (who) was good and just:
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
(this had not consented to the counsel and deed of them; and he was waiting for the kingdom of Aloha: )
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
this approached Pilatos, and begged the body of Jeshu;
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
and he took it down, and wrapped it in a cloth of linen, and laid it in a hewn sepulchre, in which no one had hitherto been laid.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
And it was the day of the preparation; and the shabath had lighted.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
And the women also drew near, they who had come with him from Galila; and they saw the sepulchre, and where the body was laid;
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
and, returned, they prepared balsams and aromatics, and on the shabath rested, as it is commanded.