< Luka 23 >

1 Mkutano wote wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
And the assembly broke up, and conducted Jesus to Pilate:
2 Wakaanza kumshutumu, wakisema, “Tumemkuta mtu huyu akipotosha taifa letu, kwa kukataza tusitoe kodi kwa Kaisari, na akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, Mfalme.”
and they accused him, saying, We found this man perverting the nation, and forbidding to give tribute to Cesar, calling himself Messiah the King.
3 Pilato akamuuliza, akisema, “Je wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Na Yesu akamjibu akisema, “Wewe wasema hivyo”.
Then Pilate, asking him, said, You are the King of the Jews? He answered, You say right.
4 Pilato akamuambia kuhani mkuu na makutano, “Sioni kosa kwa mtu huyu”.
Pilate said to the chief priests and the multitude, I find nothing criminal in this man.
5 Lakini wao wakasisitiza, wakisema, “Amekuwa akiwachochea watu, akifundisha katika Uyahudi yote, kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa.”
But they became more vehement, adding, He raised sedition among the people, by the doctrine which he spread through all Judea, from Galilee, where he began, to this place.
6 Pilato aliposikia haya, akaulizia kama mtu huyo ni wa Galilaya?
When Pilate heard them mention Galilee, he asked, whether the man were a Galilean.
7 Alipotambua kuwa alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka Yesu kwa Herode, ambaye naye alikuwa Yerusalemu kwa siku hizo.
And finding that he belonged to Herod's jurisdiction, he sent him to Herod, who was also then at Jerusalem.
8 Herode alipomuona Yesu, alifurahi sana kwasababu alitaka kumuona kwa siku nyingi. Alisikia habari zake na alitamani kuona moja ya miujiza ikifanywa na yeye.
And Herod was very glad to see Jesus: it was what he had long desired; having heard much of him, and hoping to see him perform some miracle.
9 Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi, lakini Yesu hakumjibu chochote.
He, therefore, asked him many questions, but Jesus returned him no answer.
10 Makuhani wakuu pamoja na waandishi walisimama kwa ukali wakimshitaki.
Yet the chief priests and the scribes, who were present, accused him with eagerness.
11 Herode pamoja na maaskari wake, walimtukana na kumdhihaki, na kumvika mavazi mazuri, kisha akamrudisha Yesu kwa Pilato.
But Herod and his military train despised him: and having, in derision, arrayed him in a splendid robe, remanded him to Pilate.
12 Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo, (kabla ya hapo walikuwa maadui).
On that day, Pilate and Herod became friends; for, before, they had been at enmity.
13 Pilato akawaita pomoja makuhani wakuu na watawala na umati wa watu,
Pilate, having convened the chief priests, the magistrates and the people,
14 Akawaambia, “Mmeniletea mtu huyu kama mtu anaye waongoza watu wafanye mabaya, na tazama, baada ya kuwa nimemhoji mbele yenu, sikuona kosa kwa mtu huyu kuhusu mambo yote ambayo ninyi mnamshitaki yeye.
said to them, You have brought this man before me, as one who excites the people to revolt; yet, having examined him in your presence, I have not found him guilt of any of those crimes of which you accuse him.
15 Hapana, wala Herode, kwa maana amemrudisha kwetu, na tazama hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo.
Neither has Herod; for I referred you to him. Be assured, then, that he has done nothing to deserve death.
16 Kwahiyo basi nitamuadhibu na kumuachilia.
I will therefore chastise him, and release him.
17 (Sasa, Pilato anawajibika kumuachilia mfungwa mmoja kwa wayahudi wakati wa sikukuu).
For it was necessary that he should release one to them at the festival.
18 Lakini wote wakapiga kelele pamoja, wakisema, “Mwondoe huyo, na tufungulie Baraba!”
Then all cried out together, Away with this man, and release to us Barabbas.
19 Baraba alikuwa ni mtu ambaye amewekwa gerezani kwa sababu ya uasi fulani katika jiji na kwa kuua.
Now Barabbas had been imprisoned for raising sedition in the city, and for murder.
20 Pilato akawaambia tena, akitamani kumwachilia Yesu.
Pilate, willing to release Jesus, again, expostulated.
21 Lakini wao wakapiga kelele, wakisema, “Msulibishe, msulibishe.”
But they cried, saying, Crucify! crucify him!
22 Akawauliza kwa mara ya tatu, “kwa nini, huyu mtu amefanya maovu gani? Sikupata kosa linalostahili adhabu ya kifo kwake. Kwahiyo nitakapo maliza kumuadhibu nitamuachilia.”
A third time he repeated, Why? What evil has this man done? I do not find him guilty of any capital crime; I will therefore chastise him, and release him.
23 Lakini wakasisitiza kwa sauti ya juu, wakitaka asulubiwe. Na sauti zao zikamshawishi Pilato.
But they persisted, demanding, with much clamor, that he might be crucified. At last, their clamors, and those of the chief priests, prevailed:
24 Hivyo Pilato akaamua kuwapatia matakwa yao.
and Pilate pronounced sentence, that it should be as they desired.
25 Akamuachilia yule waliyemtaka ambaye alifungwa kwa kusababisha ghasia na kuua. Lakini akamtoa Yesu kwa matakwa yao.
Accordingly, he released a man who had been imprisoned for sedition and murder; whom they required; and gave up Jesus to their will.
26 Walipokuwa wakimpeleka, walimkamata mtu mmoja aitwaye Simoni wa Ukirene, akitokea katika nchi, wakamtwika msalaba ili abebe, akimfuata Yesu.
As they led him away, they laid hold of one Simon, a Cyrenian, coming from the country, and laid the cross on him, that he might bear it after Jesus.
27 umati mkubwa wa watu, na wanawake ambao walihuzunika na kuomboleza kwa ajili yake, walikuwa wakimfuata.
And a great multitude followed him, amongst whom were many women, who lamented and bewailed him.
28 Lakini akawageukia, Yesu akawaambia, 'Mabinti wa Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ya ajili watoto wenu.
But Jesus, turning to them, said, Daughters of Jerusalem, weep not for me, but weep for yourselves, and for your children:
29 Tazama, siku zinakuja ambazo watasema, “Wamebarikiwa walio tasa na matumbo yasiyozaa, na matiti ambayo hayakunyonyesha.
for the days are coming, in which they shall say, Happy the barren, the wombs which never bare, and the breasts which never gave suck!
30 Ndipo watakapo anza kuiambia milima, 'Tuangukieni,' na vilima, 'Mtufunike.'
Then they shall cry to the mountains, Fall on us; and to the hills, Cover us:
31 Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje ukiwa mkavu?”
for if it fare thus with the green tree, how shall it fare with the dry?
32 wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe.
And two malefactors were also led with him to execution.
33 Walipofika mahali paitwapo Fuvu la kichwa, ndipo wakamsulubisha pamoja na wale wahalifu, mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto.
When they came to the place called Calvary, they there nailed him to a cross, and the malefactors also; one at his right hand, the other at his left.
34 Yesu alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. “Nao wakapiga kura, kugawa mavazi yake.
And Jesus said, Father, forgive them, for they know not what they do. And they parted his garments by lot.
35 Watu walikuwa wamesimama wakiangalia huku watawala wakimdhihaki, wakisema, “Aliwaokoa wengine. Sasa ajiokoe mwenyewe, kama yeye ni Kristo wa Mungu, mteule”.
While the people stood gazing, even their rulers joined them in ridiculing him, and saying, This man saved others; let him save himself, if he be the Messiah, the elect of God.
36 Askari pia walimdharau, walimkaribia yeye na wakumpa siki,
The soldiers likewise mocked him, coming and offering him vinegar,
37 wakisema, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi jiokoe mwenyewe”
and saying, If you be the King of the Jews, save yourself.
38 Kulikuwa pia na alama juu yake iliyoandikwa “HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.”
There was also an inscription over his head in Greek, Latin, and Hebrew, THIS IS THE KING OF THE JEWS.
39 Mmoja wa wahalifu aliyesulubishwa alimtukana akisema, “Wewe si Kristo? jiokoe mwenyewe na sisi”
Now, one of the malefactors who suffered with him, reviled him, saying, If you be the Messiah, save yourself and us.
40 Lakini yule mwingine akajibu, akimkemea na akisema, “Je wewe humuogopi Mungu, nawe uko katika hukumu hiyo hiyo?
The other, rebuking him, answered, Have you no fear of God, you who are undergoing the same punishment?
41 Sisi tupo hapa kwa haki, kwa maana sisi tunapokea kile tunachostahili kwa matendo yetu. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
And we, indeed, justly; for we receive the due reward of our deeds: but this man has done nothing amiss.
42 Na aliongeza, “Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.”
And he said to Jesus, Remember me, Lord, when thou comest to thy kingdom.
43 Yesu akamwambia, “Amini nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”
Jesus answered, Indeed, I say to you, To-day you shall be with me in paradise.
44 Hapo ilikuwa karibu saa ya sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa ya tisa,
And, about the sixth hour, there was darkness over all the land, which lasted till the ninth.
45 Mwanga wa jua ulizimika. Kisha pazia la hekalu likagawanyika katikati kuanzia juu.
The sun was darkened, and the vail of the temple was rent in the midst.
46 Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, “Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,” baada ya kusema haya, akafa.
And Jesus said with a loud voice, Father, into thy hands I commit my spirit; and having thus said, he expired.
47 Wakati Akida alipoona yaliyotendeka alimtukuza Mungu akisema, “Hakika huyu alikuwa mtu mwenye haki.”
Then, the centurion, observing what had happened, gave glory to God; saying, Assuredly, this was a righteous man.
48 Wakati umati wa watu waliokuja pamoja kushuhudia walipoona mambo yaliyofanyika, walirudi huku wakipiga vifua vyao.
Nay, all the people who were present at this spectacle, and saw what had passed, returned, beating their breasts.
49 Lakini marafiki zake, na wanawake waliomfuata toka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiangalia hayo mambo.
And all his acquaintance, and the women who had followed him from Galilee, standing at a distance, beheld these things.
50 Tazama, palikuwepo na mtu aitwaye Yusufu, ambaye ni mmoja wa baraza, mtu mzuri na mwenye haki,
Now, there was a senator, named Joseph, a good and just man,
51 (alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao), kutoka Armathaya, mji wa Kiyahudi, ambao ulikua ukisubiria ufalme wa Mungu.
from Arimathea, a city of Judea, who had not concurred in the resolutions and proceedings of the rest; and who himself, also expected the Reign of God.
52 Mtu huyu, alimkaribia Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
This man went to Pilate, and begged the body of Jesus.
53 Alimshusha, na akauzungushia sanda, na akaumweka katika kaburi lililokuwa limechongwa katika jiwe, ambalo hakuna aliyewahi kuzikwa.
And having taken it down, he wrapped it in linen, and laid it in a tomb cut in stone, in which no man had ever been deposited.
54 Ilikuwa ni siku ya maandalizi, na Sabato inakaribia.
Now that day was the preparation, and the Sabbath approached.
55 Wanawake, waliokuja nao kutoka Galilaya, walimfuata, na wakaona kaburi na jinsi mwili wake ulivyolazwa.
And the women, who had accompanied Jesus from Galilee, followed Joseph, and observed the tomb, and how the body was laid.
56 Walirudi na kuanza kuandaa manukato na marashi. Kisha siku ya sabato walipumzika kwa mujibu wa sheria.
When they returned, they provided spices and ointments, and then rested the Sabbath, according to the commandment.

< Luka 23 >